Habari za Punde

"Eco Schools": Programu Inayoshajihisha Utunzaji Mazingira Endelevu Maskulini

Na Mwashamba Juma.
JAMII bado inauelewa mdogo kuhusu taka, sio wengi wenye uelewa kama taka ni muhimu na zina faida kubwa kwa maisha ya kila siku.
Badala yake huchukuliwa kama ni uchafu wenye kukirihisha kiasi ya kutothaminiwa na kutunzwa kwenye mazingira mazuri kwa kuamini kutokua na matumizi wala faida kwao.
Wanamazingira wanaamini hakuna kisichofaida kinachotokana na taka taka ziwe za majumbani, maskulini hata viwandani, ikiwa zitajengewa mazingira yakutumika tena la kuleta faida kwa jamii na uchumi.
Jamii inatambua suluhisho pekee la taka ni kuchomwa moto na kuangamizwa, suala ambalo linapingwa na wanamazingira, ambao wanaeleza moshi unaotokana na takataka ni sumu kwa afya za binaadamu na viumbe anuai (bio diversity).
Mradi wa Ikolojia katika skuli za ukanda wa bahari ya Hindi maarufu kama "Eco Schools" unaratibiwa na Kamisheni ya Bahari ya Hindi (IOC) chini ya ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya (EU).
Ulianzishwa kwa awamu ya kwanza mwaka 2011 ambao unatekelezwa na skuli 45,000 kutoka nchi sita za visiwa duniani, zikiwemo Re- Union, Visiwa vya Comoro, Madagascar, Maurituis, Syschelles na Zanzibar kwa Tanzania.
Zanzibar mradi uliletwa na Wizara ya Ardhi Maji Nishari na Mazingira nakuratibiwa na Jumuiya ya Mandeleo ya Vijana, Elimu na Mazingira, Zanzibar (ZAYEDESA) chini ya utekelezaji wa kamati ya kitaifa ya ZNSC iliyozishirikisha taasisi mbalimbali za umma na binafsi kwa ushirikiano na Wiraza ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Zanzibar.
Itakumbukwa kuwa mwezi Oktoba mwaka jana, Mwenyekiti wa ZAYEDESA Mama Shadya Karume alizindua rasmi mradi wa "Eco- schoosl" kwa Zanzibar, pale skuli ya "Stone Town Internation" Migombani mjini Unguja.
Katika uzinduzi wake, Mama Shadya alisisitiza suala la utunzaji mazingira endelevu kwamba hujengwa na jamii hasa vijana ambao aliwaelezea kama ni nguvu kazi ya udhibiti wa mazingira, ili yasiharibike kwani vijana ni wadau wakubwa.
Akitoa ufafanuzi kuhusu mradi wa Ikolojia (Eco Schools) kupelekwa mashuleni kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Mama Shadya alisema anaamini elimu ina uwezo mkubwa wa kufanya mabadiliko. Sambamba nakueleza kuwa elimu ndio chanzo cha maendeleo endelevu.
Mama Shadya ambae pia ni mke wa rais wa Zanzibar mstaafu awamu ya tano, Mhe. Amani Abeid Karume anawaelezea vijana na watoto kwamba wanahitaji kupatiwa elimu ya kutosha kuhusu athari za uchafuzi wa mazingira.
Kamati ya taifa ZNESC imeteua skuli 30 za uma na binafsi kwa msingi na sekondari kwa Unguja na Pemba ambapo Unguja skuli 20 zikiwemo 13 za umma na saba binafsi wakati Pemba skuli 10, nane za umma na mbili binasi kwajili ya majaribio ya mradi wa "Eco Schools"
L: Sifa za skuli kujiunga kwenye programu ya "Eco Schools"
Ili skuli iingie kwenye mchakato wa ikolojia, nilazima ifuate muuongozo uliotolewa na Kamisheni ya Bahari ya Hindi (IOC) ambao unalazimisha skuli kutekeleza njia saba muhimu za "Eco" ikiwemo kujisajili kwenye tovuti ya kimataifa ya "Eco Schools" ambayo inaunganisha skuli zote zinazotekeleza mradi huo duniani, ukiwa na lengo la kubadilishana uzoefu na kujuana.
Aidha skuli hulazimika kuwa na miongoni mwa shughuli zinazotekelezwa na programu ya Eco ikiwemo miradi ya taka, umeme, maji, afya, viumbe hai, miradi inayohusisha bahari na fukwe zake, miti asilia, bustani, misitu, upepo, matumbawe na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kuanza na walo mitatu na kuitekeleza.
Miradi hiyo kwa lugha ya "Eco" hujuulikana kama "Eco theme" sambamba na skuli kulazimika kuunda kamati ya ikolojia itakazishirikisha jamii iliyoizunguka mazingira ya skuli husika wakiwemo majirani, walimu na wanafunzi na viongozi wa shehia zao.
Kwamujibu wa mwongozo huo wa kimataifa, Kamati ya "Eco" ni lazima iongozwe na wanafunzi wenyewe pamoja na kuweka kumbukumbu kwenye jalada maalum kutokana  na shughuli zote za Eco zinazofanyika maskulini.
"School code" ni sawa na sera ama sheria mama ambayo skuli teule katika programu ya "Eco Schools" italazimika kuianzisha ambayo itabeba dhima nzima ya "Eco" kutokana na jina la skuli husika.
Hata hivyo mwongozo unalazimisha "code" za skuli ambazo zitaelezea vipaumbele vya kimazingira ambavyo skuli inavitekeleza kwenye program hiyo. Mathali skuli ya "Kwetu Bilingual" iliyoko Nungwi, Wilaya ya Kaskazini "A" Unguja imetoka na code ya (Shajihisha mazingira, kwa kulinda dunia).
Mwongozo wa kimataifa wa programu ya ikolojia maskulini unalazimisha "Code" hiyo kutambulikana kwenye mazingira ya ndani na nje ya skuli zote teuli za Unguja na Pemba, si kwa wanafuzi pekee na walimu hata wanajamii walio karibu na skuli hulazimika kuijua.
Mbali na mafanikio machache yaliyofikiwa na programu ya "Eco schools" kwa kufanikiwa kupatikana kwa skuli tatu tuu za Unguja kati ya 30 teule kwa Unguja na Pemba.
Maalim Hamza Rijaal ambae ni mjumbe wa kamati ya ZNESC kutoka Jumuiya ya Mazingira ya CODECOZ, anaeleza skuli zilizofuzu kwenye program ya "Eco" ni Ben Bella kwa skuli za umma na mbili binafsi zikiwemo "Stone Town Internation School" kwa wilaya ya mjini Magharibi, Unguja na Mahaad Istiqama iliyoko wilaya ya kati, mkoa wa Kusini Unguja.
Aidha alieleza skuli ya "Kwetu Bilingual" iliyoko Nungwi na ile ya umma ya Umoja sekondari huko Wilaya ya Kati mkoa wa Kusini Unguja pamoja na ya "Connecting Continent" huko wilaya ya Wete Mkoa wa kusini Pemba zinashika nafasi ya pili kwa kwenye kuiwakilisja "Eco".
L: Changamoto zinazo ukabili mradi wa "Eco Schools," Zanzibar
Mwenyekiti wa kamati ya taifa ya programu ya "Eco Schools" kwa Zanzibar, ZNESC ambae pia ni Ofisa ufuatiliaji na tathmini sekondari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Zanzibar, Maalim Khamis salum Khamis anaeleza changamoto zinazozikabili skuli za umma katika utekelezaji wa mradi huo.
Anasema kumekuwa na changamoto nyingi kutokana na mradi kupokelewa na walimu wachache wanaousimamia kwa skuli zote za umma na binafsi sambamba na kueleza ikitokea mwalimu kuhamishwa kituo cha kufundishia ama kustaafu, skuli haibebi dhima ya kuusimamia na kuuedeleza mradi huo.
Anasema ikitokea kuwekwa mwalimu mwengine wa kusimamia programu hiyo kwenye skuli, huwa haelewi chochote ndio maana mradi huzorota maskulini.
Mwl. Hamza Rijaal anaeleza uelewa mpana zaidi bado unahitajika maskulini kutokana na kupatikana skuli chache zilizofanya vizuri.
Alisema skuli za umma  zimetoa ushiriki mdogo kwa kupatikana skuli moja ambayo ni Ben bella kati ya 20 zilizoteuliwa na mradi ambapo binafsi alieleza kupatikana skuli mbili za "Stone Town International na Mahaad Istiqama"  
Mkurugenzi kutoka skuli binafsi ya "Stone Town International" ambae pia ni mjumbe wa ZNESC, Bi. Jamila Jafar ambae anaeleza walivyofanikiwa kuzitathmini skuli za unguja zinasotekeleza mradi wa "Eco"
"Tumegundua baadhi ya changamoto maskulini lakini tumewashauri na kuwapa maelekezo jinsi ya kukabiliana na program hii, bila kutumia gharama ya fedha, pia tumewashauri wawe wanabadilisha taaluma na uzoefu kupitia skuli zilizofanya vizuri katika kufikia malengo yaliyokusudiwa". alieleza Bi. Jamila.
Mbali ya changamoto zilizoonekana na kamati ya ZNESC, walimu kwa skuli zote za umma na binafsi wanaeleza kuwa ushirikiano mdogo wanaoupata kwenye skuli wanazozifundishia huchangia kurudisha nyuma juhudi za "Eco" pamoja na morali ya walimu kufikia malengo ya mradi ikiangaliwa kuwa ni wa kujitolea zaidi kuliko maslahi.
Mwalimu Adam Shaaban Khatib kutoka skuli ya Umoja sekondari anaeleza kuwa hajawahi kupata usaidizi kutoka kwa mwalimu yeyote katika skuli yake.
Awali ZAYEDESA ilitoa mafunzo kwa walimu 21 wa skuli za majaribio ili kuendana sambamba na mradi wa "Eco Schools" mapema mwezi Julai mwaka huu.
Tatizo la lugha pia limetajwa kuwa kikwazo cha kupiga hatua mbele mradi wa "Ikolojia" maskulini, hali iliyotajwa kurejesha nyuma juhudi za programu hiyo ambayo tageti yake kubwa imeelekezwa kwa wanafunzi wa msingi na sekondari.
Maalim Rijaali anaeleza kuwa mradi umefanikiwa zaidi kwenye skuli binafsi kutokana na kuzungumzwa zaidi lugha ya kiiengereza ikilinganishwa na skuli za umma ambazo mara nyinngi huzungumza lugha mama ya kiswahili.
Aidha Walimu wanaosimamia mradi huo maskuli wameiomba kamati ya taifa, ZNESC kufanya uwezekano wa kuwapatia muongozo wa kiswahili "Eco manual" kutokana na jamii kubwa kuzungumza lugha ya kiswahili.
L:Mafanikio ya mradi maskuli / kwenye jamii
Mradi umeleta uweledi kwa wanafunzi kujifunza utunzaji mazingira endelevu kwa vitendo.
Mwanafunzi Habil Hilal wa kidato cha pili kutoka skuli ya Mahaad Istiqama anaeleza alivyojifunza jinsi ya kuzibagua takataka  na manufaa yake ambapo alieleza kwenye skuli yao, wameweka sehemu nne tofauti za kuhifadhia taka.
Anaeleza wamefanikiwa kuzibagua taka ngumu kama vigae, mabati mabovu, karatasi, chupa na majani kwa kila taka kuwekwa sehemu yake.
Sambamba na kuzielezea taka zinazoweza kutumika kwa matumizi mbadala hufanywa hivyo.
"Tunazitumia taka za majani kwa kufanya decomposition, pia tunatumia taka za majani kwaajili ya mbolea ya bustani ya skuli yetu"
Anaeleza mti ulioekewa taka za majani makavu unapata ubora kwa kuhifadhi maji  kwenye miti hasa wakati wa kiangazi ambapo jua hua kali na kuathiri mimea wakati wa joto kali.
Nae mwanafusi Aisha Ali anaeleza taka za maji zinapozungushwa kwenye mmea husaidia kuweka kivuli kwenye mmea, pamoja na kuondeza rutuba na kulinda "bio deversity" kwenye udongo.
Aidha Mwalimu mkuu kutoka skuli ya msingi kwetu "Bilingual" anaeleza mafaniniko yao ya kuzigawanya taka kama walivyofanya Mahaad Istiqaama, Ben bella na Stone Town International na ile ya "Conecting continent iliyoko wilaya ya Chake chake, mkoa wa kusini - Pemba.
Mwalimu mkuu kutoka skuli yamsingi Kwetu Bilingual, Mwanahamis Suleiman anaeleza taka za chupa na plastiki huziuza kwa kampuni ya .....na fedha zinazopatikana huziingiza kwenye mfuko wa skuli kwa maendeleo ya skuli hiyo.
Nae mwalimu mkuu wa skuli ya "Stone Town International", Ingrid Verhulst anasema wanafunzi skulini hapo hutumia karatasi kwa kuzifanyia mkaa ambao hutumika kwa matumizi ya skuli kama kupikia.
Alielezea "theme" nne zinazofanywa na wanafuzi wa skuli hiyo kwa mujibu wa mwongozo wa program hiyo ya ikoloji ya mashuleni.
Alisema skuli inafanya programu ya taka, fukwe za bahari ambapo kila Ijumaa huenda ufukweni kuokota taka taka, programu ya nishati kwa kuwashajihisha wanafunzi juu ya matumizi sahihi ya vifaa vya umeme wakiwepo skuli na hata majumbani mwao kwa kuwakataza kutokutia taa wakati wa mchana ama feni sehemu isiyo watu.
"Wanafunzi pia wanaimarisha kilimo cha mchaichai ambacho kimesanifiwa kama bustani inayopendeza machoni pia hutumiwa kwa chai ya wanafunzi na wageni wanaofika skuli hapo" alieleza.
Alisema pia wanatumia boksi zilizotumika ambazo huzisanifu kwenye mwonekano mzuri  na kuziweka kila darasa ambako wanafunzi huhufadhia taka taka hasa za makaratasi.
"Tunamshirikisha jirani yetu hapa muuza madafu kama sehemu ya mazingira yetu, tunatumia mafuu ya madafu, tunayasanifu kwenye mwonekano mzuri kwaajili ya urembo wa mazingira ya skuli yetu" alifahamisha Mwl. Verhulst
Aidha anaeleza kuwa pia huzisanifu cd mbovu, kwa kutengeneza vibakuli vya kuhifadhia vifaa vidogo vya skuli kama peni, raba na penseli za wanafunzi madarasani.
Skuli ya "Stone Town International", ni moja kati ya skuli zinazohifadhi mbao chakavu zinazotokana na thamani za skuli. 
Programu ya "Eco Schools" mbali na kutumiwa kwa mualama wa mazingira maskulini, pia inaweza kutumika kama mitaala ya masomo ya kawaida yakiwemo ya masomo maskuli.
Mathalani kupitia masomo ya lugha kama Kiingereza,  kiswahili au kiarabu wanafunzi wataweza kuandika insha, mashairi au uandishi wa barua zao kwa kuielezea "Eco".
"Eco School" pia ina nafasi pana ya kuelezewa kwenye masmo ya jiografia, masomo ya uraia, kupitia mada za mazingira kama ongezeko la idadi ya watu ama mada za mabadiliko ya hali ya hewa na uchafuzi wa mazingira.
Mwl. Hamza Rijaal, anaeleza hata masomo ya sayansi kama fizikia biolojia, kemia na hesabati yananafasi kubwa kwa wanafunzi kuielezea na kuifanya "Eco" kiviitendo kupitia michoro ya "Pie chati na magrafi" ambayo hutoa tafsiri nyepesi kwenye maelezo ya mada husika.
Skuli 30 teule za programu ya ikolojia  mashuleni kwa Zanzibar ni pamoja na Ben Bella, Muungano msingi, Kijichi msingi, Kiembe samaki sekondari na Mikindani kwa wilaya ya mjini Magharibi kwa skuli za umma.
Ambapo mkoa wa Kaskazini ni pamoja na Potoa msingi, Mlimani sekondari, Donge msingi na Muanda sekondari.
Mkoa wa kusini Unguja, skuli ya Dunga msingi, Mtende msingi, Umoja sekondari na Mtule sekondari.
Kusini Pemba Makombeni msingi, Vitongoji msingi, Kangani sekondari na Fidel Castro sekondari.
Kaskazini Pemba, Chwaka - tumbe sekondari, Makangali msingi na Wete sekondari.
Kwa upande wa skuli binafsi ni pamoja na Stone town International, Lauriate Internatinal, Rainbow, Hifadhi na Francis Maria kwa wilaya ya njini Magharibi.
Mahad Istikama pekee kwa mkoa kusini Unguja, skluli za Kwetu Bilingual na Unique Learning kwa mkoa wa Kaskazini.
Kwa upande wa Pemba ni skuli ya Connecting Continet kwa Kusini na Ikra kwa mkoa wa Kaskazini.
ZNSC iliyozishirikisha taasisi za umma na binafsi, wakiwemo Wizara ya Ardhi, Maji Nishati na Mazingira, Wizara ya Elimu, Idara ya mazingira, Jumuiya ya skuli binafsi, Zanzibar (ZAPs).
Wengine ni Kisiwa cha Chumbe, jumuiya ya Mazingira ya CODECOZ, Jumuiya ya wakulima  wenye viwanda na masoko (ZNCCIA), mahoteli, wadau wa elimu, vyombo vya habari.
mwashambajuma55@hotmail.com

+255 776 808 093

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.