Na Mwandishi Wetu.
WAJUMBE wa
Baraza la Wawakilishi wamewalalamikia baadhi ya watumishi wa Serikali waliopewa
dhamana ya kuitumikia Serikali badala yake kuweka mbele maslahi yao binafsi
kwenye miradi ya maendeleo, hali waliyoeleza inakwamisha utekelezaji wa miradi
hiyo kwa wakati.
Waliyasema
hayo huko ukumbi wa mikutano wa Z-Ocean, Kihinani wakati wakijadili kuhusu
mradi wa ujenzi wa kijiji cha utalii Matemwe, mkoa wa Kaskazini Unguja ambao
umezusha mvutano mkubwa baina wa mwekezaji na wananchi wa kijiji hicho.
Walisema
kucheleweshwa kwa miradi ya maendeleo nchini kunakwambisha
shughuli za
maendeleo sambamba na kuikosesha serikali mapato yake kutoka kwa wawekezaji.
Aidha
waliilalamikia Mamlaka ya Uwekezaji (ZIPA) kwa kuchelewa kwao kutoa vibali vya
ujenzi kwa baadhi ya wawekezaji nchini, jambo walilolieleza Wawakilishi hao
kuwa linarudisha nyuma juhudi za wawekezaji na serikali kwa ujumla.
Wajumbe hao
pia walimlalamikia wakala wa mradi wa "Penny Royal" unaotarajiwa
kuanza karibuni katika kijiji cha Matemwe, kwa kuchukua kiasi kikubwa cha fedha
zilizotolewa kwaajili ya kuwalipa fidia wananchi wa kijiji hicho na badala yake
wamezitumia kwa maslahi yao binafsi.
"Ni
aibu na fedheha kwa mwekezaji kupigia magoti wajumbe wa Baraza la Wawakilishi,
kulalamikia ubadhirifu wa uwekezaji" alisema Mwakilishi wa jimbo la
Kwamtipura, Hamza Hassan Juma wakati akichangia mjadala wa ucheleweshwaji wa
ujenzi wa kijiji cha utalii Matemwe "Penny Royal" walioulalamikia
kucheleweshwa na baadhi ya watendaji wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Alisema
kijiji cha Matemwe kinakabiliwa na umasikini wa hali ya juu, hivyo alieleza
kuwa ujenzi wa kijiji hicho ni mkombozi wa wananchi wanyonge kijijini hapo.
Alisema
mradi wa "Penny Royal" katika kijiji cha Matemwe ni mradi mkubwa
kuwekezwa katika historia ya visiwa vya Zanzibar kwani unamiradi mingi ndani
yake ikiwemo miundombinu ya barabara, maji safi, umeme, ujenzi wa makazi ya
wanakijiji, uwanja wa ndege pamoja skuli na hospitali za kimataifa, suala
alilolieleza kuwa litatoa nafasi nyingi za ajira kwa wanakijiji cha Matemwe na
maeneo jirani ya Mkoa wa Kaskazini.
"Ndugu
zetu ZIPA msione kama mnasemwa vibaya kwenye hili, bali tunatekeleza malengo ya
rais ya kuwaletea maendeleo wananchi wetu" alisema.
Nae Waziri
asiekuwa na Wizara maalum ambae pia ni Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Said
Soud alisema ni jukumu lao kutetea haki na maslahi ya wananchi ili kuwapa imani
kwa serikali yao.
Alisema
serikali haijakwamisha haki za wananchi bali watu wachache ndio wanaoitia
dosari serikali katika utendaji wake.
Akizungumzia
hatua zilizochukuliwa na BLM katika kutatua mgogoro uliopo baina ya mwekezaji wa
"Penny Royal" na wanakijijiji hicho cha Matemwe Mhe. Soud alisema
imeundwa kamati maalumu ya kukabiliana na changamoto za mradi huo kisha
kumfikishia rais hatua iliyofikiwa.
Alisema rais
wa Zanzibar ni mweledi wa maendeleo nakuongeza kuwa Serikali ya SMZ iko makini
sana katika kukabiliana na watendaji wadanganyifu wa miradi ya maendeleo.
"Uwekezaji
tunaupenda na wananchi tunawapenda pia kwani
wao ndio walioiweka dola madarakani" alisema
Akizungumzia
kuhusu kufeli kwa baadhi ya miradi ya maendeleo nchini, Mwakilishi Hassan
Khamis Diaspora (Welezo) alisema miradi mingi inashindwa kuendelea kutokana na
kuwepo kwa watumishi wa chache serikalini wanaoelekeza mbele maslahi yao
binafsi.
Nae
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kaskazini Unguja, Haji Juma Haji alisema mradi wa
"Penny Royal" uliwahi kutoa kiasi kikubwa cha fedha kwaajili ya
kulipwa fidia wananchi wa kijiji cha Matemwe badala yake fedha hizo zililiwa na
watu wachache waliopewa dhamana ya kusimamia.
Hivyo
aliiomba serikali kusimamia tatizo liliopo ili kulipatia ufumbuzi kwa lengo la
kuendeleza mradi huo na kuepusha migogoro baina ya wenyeji wa Matemwe na
mwekezaji wao.
Kwaupande
wake Ofisa mdhamini Mkoa wa Kaskazini Unguja ambae pia ni mratibu wa polisi
mkoani humo, Ali Abdalla Kitole alieleza mbali ya serikali kulifanikisha suala
la ulipwaji wa fidia kwa wananchi wa jijini cha Matemwe lakini bado mradi
unakabiliwa na changamoto kwa wenyeji wa kijiji hicho kwa kumlalamikia
mwekezaji huyo kwamba hata kazi ndogo ndogo mathalani za kusogeza mawe na
zinazoshabihiana na hizo pia hutumia waajiri wake wakigeni au mashine badala
kuwatumia wazawa ili kupunguza tatizo la ajira linalowakabili.
Naibu wa
Wizara ya Ardhi, Maji Nishati na Mazingira ambae pia ni Mwakilishi wa jimbo la
Matemwe aliitaka kamati ya wilaya iliyoteuliwa na serikali kushughuli mgogoro
huo pamoja na wadau wote wanaohusika katika uwekezaji huo kukaa pamoja na
kujadili jinsi ya kupata suluhu ya mgogoro huo.
Nae
Mwakilishi wa mradi huo wa "Penny Royal", Salim Muhammed Said
aliiomba serikali kuingilia kati mgogoro huo ili kuwabaini wanaostahiki kulipwa
fidia zao kwani alieleza walitoa fedha nyingi kuwalipa wananchi na kadri siku
zinavyoendelea wanaibuka wepya na kudai fidia zao jambo aliloeleza kuwa
palipita udanganyifu katika mgao wa fidia hizo.
Kampuni ya
"Penny Royal" iliyopo chini ya uongozi wa Brian Thomas, kupitia mradi
wao "Amber Reasort" wenye lengo la kujenga kijiji cha utalii kijijini
Matemwe mkoa wa Kaskazini Unguja, umekumbwa na changamoto ya mgogoro wa ardhi
baina yake na wenyeji wa kijiji hicho, jambo linalokwamisha juhudi za ujenzi wa
mradi huo.
No comments:
Post a Comment