Habari za Punde

Taarifa Kwa Vyombo vya Habari Kutoka PENNYROYAL GIBRALTAR LIMITED


Kampuni ya Pennyroyal (Gibraltar) Limited ina furaha kubwa kuutangazia umma kupitia vyombo vya habari kwamba, imesaini Mkataba wa muda mrefu wa Uhandisi, Ujenzi na Manunuzi (ECP Agreement) na Kampuni ya MCC Overseas Ltd (MCCO)” kutoka China kujenga mradi wa Pennyroyal wa “Zanzibar Amber Resort”. 

Sherehe hizi za utiaji saini zilifanyika leo tarehe 14 Disemba 2016 katika Hoteli ya Park Hayatt, Mji wa Mawe Zanzibar.  Mkataba huo ambao una gharama/thamani ya dola za kimarekani milioni 330.  Kupitia Mkataba huo, Kampuni ya MCCO itakuwa na jukumu la kuwa Mkandarasi wa mradi wa “Amber Resort” amabao watajenga villa za kifahari, majengo ya makaazi (apartments), hoteli 5 kubwa zenye hadhi ya nyota tano, marina, visiwa vya kifahari, kiwanja kikubwa cha kimataifa cha mchezo wa golf na huduma zinazoendana na mji wa kitalii.  Awamu ya kwanza ya ujenzi huo inatarajiwa kuanza katika kipindi kifupi kijacho na kumalizika mwaka 2020.

Ujenzi wa mji huu wa kitalii ambao unakusudiwa kutekelezwa katika eneo lenye ukubwa wa hekta 411 katika mwambao wa bahari ya kijiji cha Matemwe, Kaskazini Mashariki ya Kisiwa cha Zanzibar, utachangia sana jitihada za serikali za kuleta mabadiliko ya kiuchumi hususan katika sekta ya utalii na uwekezaji wa nyumba za biashara (real estate development). 

Mradi huu utatekelezwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa, vyombo, mashine na utaalamu wa hali ya juu ambao utazingatia kwa makini uhifadhi wa mazingira kwa kufuata taratibu na miongozo iliyowekwa ya serikali na ile ya kimataifa ya kulinda mazingira ya ardhi na bahari na masharti ya Hati ya Tathmini ya Athari za Kimazingira (Environmental Impact Assessment – E.I.A) iliyotolewa na serikali kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu.   Aidha, maisha ya jamii katika vijiji vinavyozunguka mradi huu yataimarika kwa kiwango kikubwa.

Tukio hili limeweka historia kwa kampuni binafsi ya Pennyroyal kuithibitishia dunia kuwa uwekezaji mkubwa kama huu utaleta mafanikio makubwa yatakayoibadilisha Zanzibar katika ramani ya dunia kwa kuwa na utalii wenye hadhi ya juu, maendeleo ya uwekezaji wa ujenzi wa nyumba za kibiashara na kuifanya Zanzibar kuwa eneo vutivu duniani.

Mradi huu utakapomalizika utaongoza kwa miradi ya sekta binafsi kwa kutoa ajira kwa takriban watu 2000 ambao watafanya kazi katika hoteli tano kubwa zenye hadhi ya nyota tano, ajira katika viwanja vyenye vya golf vyenye hadhi ya mashindano ya kimataifa, katika nyumba zenye apartments 3500, villa za kifahari 1900, na katika visiwa na maeneo yanayotoa huduma mbalimbali kama vile maduka, mabenki na huduma za kijamii. 

Katika kusaidia jamii, Pennyroyal ina mpango maalum (corporate social responsibility) wa kuwajenga uwezo wanavijiji katika maeneo mbalimbali ikiwemo sekta ya elimu, mafunzo stadi, kilimo endelevu na miradi mengine ya kuwafikia wananchi ya kunyanyua maendeleo ya kuchumi na kupunguza umasikini

Mkataba huu na kampuni ya MCC Overseas Ltd ya China, ambayo imo katika orodha ya kampuni 500 kubwa duniani, ni kielelezo kikubwa cha urafiki wa kihistoria kati ya China na Tanzania.   Ushiriki wa MCCO ni tija iliyo wazi kwa Zanzibar kupata fursa ya kuongeza uzoefu na ubunifu katika ujenzi wa eneo kubwa utakaotekelezwa na mmoja kati ya wakandarasi  wakubwa duniani


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.