Habari za Punde

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi mstaafu apongezwa

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe,Ayoub Mohamed Mahmoud (kulia) wakiwa na  Mkuu wa Mkoa Mstaafu Mhe, Abdalla Mwinyi Khamis katika sherehe za Kumpongeza Mstaafu huyo na kumzawadia zawadi mbali mbali ikiwemo Gari aina ya Noah yenye thamani Millioni kumi na Mbili ,katika hafla iliyofanyika  jana katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Mnazi Mmoja Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]31/12/2016.
 Baadhi ya Viongozi mbali mbali waliohudhuria katika hafla ya kumpongeza Mkuu wa Mkoa Mstaafu wa Mjini Magharibi Mhe, Abdalla Mwinyi Khamis katika sherehe za Kumpongeza kwa Utumishi wa muda mrefu uliotukuka na kumzawadia zawadi mbali mbali ikiwemo Gari aina ya Noah yenye thamani Millioni kumi na Mbili,katika hafla iliyofanyika  jana katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Mnazi Mmoja Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]31/12/2016.
Viongozi mbali mbali waliohudhuria katika hafla ya kumpongeza Mkuu wa Mkoa Mstaafu wa Mjini Magharibi Mhe, Abdalla Mwinyi Khamis katika sherehe za Kumpongeza kwa Utumishi wake uliotukuka    na kumzawadia zawadi mbali mbali ikiwemo Gari aina ya Noah yenye thamani Millioni kumi na Mbili,katika hafla iliyofanyika  jana katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Mnazi Mmoja Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]31/12/2016.
 Mkuu wa Mkoa Mstaafu wa Mjini Magharibi Mhe, Abdalla Mwinyi Khamis akipokea Taarifa ya pongezi zake kwa ushirikiano uliotukuka kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Mjini Marina Joel Thomas baada ya kuisoma jana wakati wa sherehe maalum ya kumpongeza na kumzawadia,iliyofanywa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Mnazi Mmoja,(katikati)Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwa mgeni rasmi katika sherehe hiyo,(kulia) [Picha na Ikulu.]31/12/2016.
  Mwimbaji wa Kikundi cha Zanzibar One Marium Juma akiimba wimbo wa "Nadekezwa" wakati wa sherehe ya kumpongeza Mkuu wa Mkoa Mstaafu wa Mjini Magharibi Mhe, Abdalla Mwinyi Khamis zilizofanyika jana katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Mnazi Mmoja,liyofanywa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi chini ya usimamizi wa Mhe,Ayoub Mohamed Mahmoud,[Picha na Ikulu.] 31/12/2016.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi Funguo za Gari aina Mpya ya Noah  Mkuu wa Mkoa Mstaafu Mhe, Abdalla Mwinyi Khamis iliyotolewa na Ofisi ya  Mkoa Mjini Magharibi jana katika sherehe za Kumpongeza kwa Utumishi uliotukuka  katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,hafla iliyofanyika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Mnazi Mmoja Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]31/12/2016.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipena mkono na Mkuu wa Mkoa Mstaafu Mhe, Abdalla Mwinyi Khamis kama ishara ya kumkabidhi  Gari aina Mpya ya Noah iliyotolewa na Ofisi ya  Mkoa Mjini Magharibi  katika sherehe za Kumpongeza Mstaafu huyo kwa Utumishi wake katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,hafla iliyofanyika  jana katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Mnazi Mmoja Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]31/12/2016.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.