STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 5.1.2017
![---](file:///C:/Users/user/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image004.gif)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amekifungua kiwanda cha Maziwa cha “Azam Dairy” na kueleza azma ya Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar ilivyokusudia kuimarisha na kuendeleza viwanda ikiwa
ni pamoja na kushirikiana na Sekta binafsi.
Dk. Shein aliyasema
hayo, katika hotuba yake aliyoitoa mara baada ya kukizindua rasmi kiwanda hicho
kinachomilikiwa na Bakhressa Group of
Campanies” inayoongozwa na Mwenyekiti wake Said Salim Bakhressa, kilichopo
Fumba Mkoa wa Mjini Magharibi ikiwa ni miongoni mwa shamrashamra za miaka 53 ya
Mapinduzi ya matukufu ya Zanzibar.
Mapema kabla ya hotuba
yake hiyo Dk. Shein alikitembelea kiwanda hicho na kupata maelezo ya kitaalamu
kutoka kwa Meneja Uzalishaji wa Kampuni ya Azam Dairy Production Limited
(ADPL) Adilson Fagundes,
Katika hotuba yake Dk.
Shein alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeamua kwa makusudi
kuendeleza sekta ya viwanda kwa kutambua umuhimu wake katika maendeleo ya
Zanzibar sambamba na historia yake katika sekta hiyo pamoja na sekta ya
biashara.
Pamoja na hayo, Dk.
Shein alieleza kuwa Serikali ipo katika hatua za mwisho za uandaaji wa Sera
Mpya za Viwanda itakayozingatia zaidi matumizi ya malighafi zinazopatikana
nchini na kueleza azma ya kuunganisha viwanda na sekta ya utalii.
Dk. Shein pia,
alitumia fursa hiyo kueleza historia ya Zanzibar katika sekta ya biashara na
viwanda kapla ya Mapinduzi Matukufu ya Januari 12, 1964 na kueleza kuwa
Zanzibar si mwanagenzi katika sekta hizo.
Adha, Dk. Shein
alitumia fursa hiyo kueleza azma ya Serikali katika kuanzisha kiwanda cha
kusindikizia samaki hasa ikizingatiwa kuwa Zanzibar ni visiwa vilivyozunguikwa
na bahari hvyo malighafi za kiwanda hicho ni rahisi kupatikana.
Dk. Shein
aliwahakikishia wananchi kuwa mji wa Fumba utafumbuka kutokana na mipango
kabambe ya Serikali katika kuliimarisha eneo hilo la uwekezaji kwa upande wa
Unguja na Micheweni kwa upande wa Pemba.
Sambamba na hayo, Dk.
Shein alitoa pongezi kwa Mwenyekiti wa Kampuni ya “Bakhressa Group of
Campanies” Said Salim Bakhressa kwa nia yake thabiti ya kujenga kiwanda hicho
hapa Zanzibar na kuleta maendeleo kwa ajili ya Zanzibar na watu wake sambamba
na juhudi zake za kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa
mipango ya maendeleo.
Dk. Shein alisema kuwa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeandaa Sera maalum katika uwekezaji kwa
kutoa nafasi kwa kila mmoja mwenye uwezo na fedha aje kuekeza haza Zanzibar
huku akieleza umuhimu wa kushirikiana na sekta binafsi ambayo ndio mashine ya
uchumi popote pale duniani.
Dk. Shein alisema kuwa
kiwanda hicho ni cha kisasa na mitambo yake haipo katika nchi za nyingi za bara
hili la Afrkka na hata nje ya bara hili na kusifu hatua hiyo na kusisitiza haja
kwa taasisi husika kuwashajiisha wananchi kunywa mazima hapa nchini kwani
imegundulika wananchi wa Zanzibar si watumiaji wazuri wa maziwa.
Aidha, Dk. Shein
alieleza haja kwa kiwanda hicho kuweka siku moja maalum ya Kitaifa ya kunywa
maziwa hatua ambayo itawashajiisha wananchi wa mbali mbali wa Zanzibar kunywa
maziwa.
Pamoja na hayo, Dk.
Shein aliahidi kutafutiwa ufumbuzi changamoto zote zinazokikabili kiwanda hicho
ikiwemo Sheria za Muungano, utumiaji
mdogo wa bidhaa za maziwa kwa wananchi wa Zanzibar, upatikanaji wa malighafi ya
maziwa na nyenginezo.
Nae Waziri wa Fedha na
Mipango, Dk. Khalid Salum Mohammed
alieleza kuwa sekta ya uwekezaji ina mchango mkubwa katika kuinua uchumi
wa nchi na ndio maana Rais Dk. Shein amekuwa akilisimamia hilo kwa nguvu zake
zote na mafanikio makubwa yanaendelea kupatikana.
Alitumia fursa hiyo
kumpongeza Sheikh Bakhressa kwa uzalendo wake wa kuekeza kiwanda hicho kwani
serikali itapata mapato kubwa kutokana na kiwanda hicho sambamba na kupanua
soko la ajira.
Mkurugenzi Mtendaji wa
Mamlaka ya Uwekezaji Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA0 Salum Khamis Nassor alieleza
mikakati iliyowekwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuanzisha na
kuendeleza maeneo huru huku akieleza namna Mamlaka yake ilivyoshirikiana na
Muwekezaji huyo katika kuanzisha kiwanda hicho.
Mapema Mwakilishi wa
Kampuni hiyo Salim Aziz alieleza kuwa kiwanda hicho kina mitambo ya kisasa ya
kusindika maziwa ambayo husindika maziwa kwa kuyapitisha katika mfumo maalum wa
joto kwa ajili ya kuyahifadhi na kuuwa wadudu ambapo katika kiwanda hicho
uwekezaji wa jumla ya Dola milioni 20 umefanyika.
Alisema kuwa kiwanda
hicho kina uwezo wa kusindika jumla ya lita Laki moja na elfu sitini kwa siku
ambapo kiwanda kinaweza kutumia malighafi ya maziwa safi na maziwa ya unga na
kuelez changamoto iliyopo ya upatikanaji wa maziwa safi.
Sambamba na hayo
alieleza kuwa kiwanda hicho kimetoa ajira za moja kwa moja zipatazo 130 na
nyengine nyingi ambazo si za moja kwa moja ambapo maziwa ya kiwanda hicho
huuzwa hapa Zanzibar kwa asilimi 10 na Tanzania Bara kwa asilimia 90.
Mwakilishi huyo pia alieleza changamoto
zilizopo zikiwemo upatikanaji wa malighafi ya maziwa ambapo maziwa yanazozalishwa
na wakulima wa hapa Zanzibar ni kidogo, Sheria za Muungano, Utumiaji mdogo wa
bidhaa za maziwa na gharama kubwa za uendeshaji wa Boiler ambayo hutumia mafuta
maalum ambayo hapa nchini hayapo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment