Habari za Punde

Operesheni Tokomeza Viroba Yaingia Siku ya Pili Jijini Dar es Salaam

Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche (kushoto) akikagua nyaraka toka kwa Msimamizi wa Kiwanda cha True Bell (T) Limited Bw. Godwin Mungere mapema leo hii jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
Msimamizi wa Kiwanda cha True Bell (T) Limited Bw. Godwin Mungere (mwenye shati la njano) akionesha baadhi ya vifungashio vya pombe kali aina ya kiroba mapema hii leo Jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika, kulia ni Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche
Baadhi ya Maafisa wa Serikali wakikagua ghala la Kiwanda cha True Bell (T) Limited mapema hii leo Jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.

Msimamizi wa Kiwanda cha True Bell (T) Limited Bw. Godwin Mungere akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mara baada ya ukaguzi wa pombe kali aina viroba katika kiwanda chake cha True Bell (T) Limited wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
Msimamizi wa Kiwanda cha True Bell (T) Limited Bw. Godwin Mungere ambao ni watengenezaji wa pombe ya Viroba aina ya Bonanza akionesha baadhi ya nyaraka kwa Afisa Kodi toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Timoth Mgaya wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
Mkaguzi wa Chakula toka TFDA Bw. John Nzila akitoa maelekezo kwa Mmiliki wa Kiwanda cha Blue Nile Bw. Mohan ambao ni watengenezaji wa pombe za kiroba aina ya Kitoko na Rivella wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika
Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche akiwaonesha waandishi wa habari pombe aina ya Kitoko inayotengenezwa na Kiwanda cha cha Blue Nile wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha Kibo Spirit Bw. Muhidin Mohamed Mwacha (kushoto) akieleza kwa  Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche jitihada walizofanya toka utengenezaji wa pombe kali aina ya viroba na kuanza uzalishaji wa maji wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
Picha zote na Eliphace Marwa - Maelezo
Baadhi ya Maafisa wa Serikali wakiwa nje ya Kiwanda cha Triple S kilichopo Wazo Mivumoni ambacho kinatengeneza pombe za viroba aina ya Signal True kikiwa kimefungwa na wamiliki wake kutoonekana wakati wa  siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika 
Picha zote na Eliphace Marwa - Maelezo

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.