NA HAJI NASSOR, PEMBA
WANAWAKE wajasiriamali kisiwani Pemba, wamesema sasa
wakati wa kusubiri uamuzi kutoka kwa wanaume, hata kwenye vikao vya harusi,
umemalizika na lazima wanawake wenyewe wafanye uamuzi kwa mambo yanayowahusu.
Wamesema
ule utamaduni wa zamani kuwa wanaume ndio kila kitu, umepitwa na wakati na kwa
karne hii, lazima wanawake wajitokezea na kujibebesha ujemedari wa kufanya
uamuzi.
Wakizungumza
na mwandishi wa habari hizi wanawake hao wajasiriamali, walisema utamaduni wa
miaka 30 nyuma kuwa waanume ndio kila kitu hasa kwenye uamuzi, sasa haupo tena.
Mwenyekiti
wa ushirika wa upandaji migomba ‘tumeamua ‘shehia ya Kiuyu kigongoni wilaya ya
Wete Pemba, Fatma Said Juma, alisema sasa wanawake lazima wathubutu kuendesha
vikao na kutoa uamuzi.
Alisema
haipendezi na wala haingii akili, kuona wanawake wanashindwa kufanya vikao
mbali mbali vikiwemo vya harusi, uamuzi wa kumsomesha mtoto, vikao vya asasi
vya kiarai pasi na kuwepo wanaume.
Mwenyekiti
huyo alieleza kuwa, sasa wanawake wameshaelimika na kupata ujasiri kwa kufanya
shughuli zao mbali mbali za maendeleo, hivyo wasishindwe na kuendesha vikao na
mikutano yao.
“Inawezekana
wazazi na walezi wetu, sisi wanawake walitunyima haki yetu ya kushiriki na
kushirikishwa kwenye vikao mbali mbali, kwa dhana kwamba hatuwezi, lakini sio
sahihi’’,alilamika.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Jumuia ya Kuhifadhi Mazingira Vitongoji VECA wilaya
ya Chakechake Sifuni Ali Haji, alisema wanawame wanauwezo mkubwa na kupelekea
maendeleo makubwa.
“Mimi
ni mwenyekiti wa VECA mbona tumeshapata miradi miengi, ingawa kuwa kushirikiana
na wenzangu, lakini wenyewe tumekuwa watundu wa kuendesha vikao vyetu.
Alieleza
kuwa, uwezo waliojaaliwa na Muumba wa kufanya kazi na kutoa uamuzi, laiti kama
hata hao wazazi waliopita wengewashirikisha vya kutosha, leo hii kusingekuwa na
wanamke anaelilia kuporwa haki yake.
Nae
mwanaharakati wa maendeleo ya wanawake kisiwani Pemba Nassra Salum Khamis,
alisema baada ya wanawake kujitumbukiza kwenye ujasiriamali na kujipatia
maendeleao, hawana sababu ya kushindwa ya kuendesha mambo mengine.
Alifahamisha
kuwa, wanawake wamekuwa na mchango mkubwa ndani ya familia na hata serikali
kuu, hivyo lazima nafasi yao hiyo, wasiiache na kuona kuwa wanaume wanaweza
kila kitu.
“Yapo
mambo ya asili yake lazima wanaume wawe juu, mfano wa mirathi, lakini hakuna ulazima
wala sheria kuwa, vikao na mikutano mbali mbali kwamba wanaume ndio wawe wasemaji
wa kuu na waamuzi’’,alifafanua.
Nae
Maulid Saleh Hamad wa Kiuyu Jimbo la Kojani, alisema wapo wanawake
waanaoendesha familia zao, kutokana na kuamua kujiingiza kwenye ujasiriamali,
na kupata mafanikio.
“Sasa
wanawake lazima tuachane na utamaduni wa zamani kwamba kila kikao na kila jambo
eti wasubiriwe wanaume, na kama hawakuja kivunjike, hili sasa sio
sahihi”,alifafanua.
Hata
hivyo hivyo Mwenyekiti wa ushirika wa wasusi wa mikoba na utengenezaji sabuni
wa “subira njema” uliopo Changaweni Mkoani, Amina Said alieleza kuwa, usawa kwenye kujiinua kiuchumi,
uko sawa baina ya jinsia mbili.
Hata
hivyo Mratibu wa TAMWA Zanzibar Mzuri Issa Ali, aliwataka wanawake wasikubali
kutafutiwa haki na uamuzi na wanaume, bali sasa wasimame wenyewe.
“Sisi
tumeshwapa taaluma ya kujielewa na kujiendeleza kiuchumi, sasa kama wameona
kuwa wanauwezo wa kujiendeleza, ndio tunakotaka kwenda huko, kila mmoja asimame
mwenyewe’’,alifafanua.
Kwa
upande wake Hassan Haji Khamis mkaazi wa Machomane Chakechake, alisema wanawake
wakiendelea kupewa elimu na nyenzo za kujiletea maendeleo, wanaweza kujihudumia
wenyewe.
“Inawezekana
hapo zamani wanawake walikuwa hawajapata taaluma na kujielewa kuwa wanahaki sawa
kwenye kutoa uamuzi au kuitisha vikao, pasi na kusubiri wanaume’’,alifafanua.
Hata
hivyo mwanasheria Mohamed Hassan Ali, wakati akiwasilisha mada kwa vikundi vya
wanawake wa mkoa wa kaskazini Pemba, alisema maendeleo hayamsubiri mwanamke eti
mpaka ashirikishwe kwenye uamuzi na wanaume.
“Mwanamke
na mwanamme wako sawa, wote wanaweza kuwa viongozi na kuongoza vikao, na kisha
kufanya uamuzi pasi mmoja kumsubiri mwenzake’’,alifafanua.
Katika
miaka ya hivi karibuni kundi la wanawake hapa Tanzania na visiwani, wamekuwa
wakijitokeza kwenye shughuli mbali mbali za kujieletea maendeleo, ambapo zaidi
ya asilimia 35 ya wanawake ni wafanyabiashara ndogo ndogo.
No comments:
Post a Comment