Na Haji
Nassor, Pemba
MACHI 24 mwaka jana, Jaji mkuu wa Zanzibar
Omar Othman Makungu, kwa mamlaka aliyonayo kikatiba, alimuapisha rais mteule wa
Zanzibar dk: Ali Mohamed Shein, kwenye uwanja wa Amani mjini Unguja.
Sherehe si
haba zilinoga, na kubahatika kuhudhuriwa na pia na rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania dk: John Pombe Mgufuli, makamu wake Samia Suluh Hassa, pamoja na
viongozi kadhaa samba mba na mabalozi.
Kama
siokufutwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa Zanzibar uliofanyika awali Oktoba 25
mwaka jana, na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Jecha Salim Jecha,
basi rais ambae engeshinda, angekuwa amaeshatimiza mwaka mmoja na miezi mitano sasa,
ndani ya Ikulu ya Zanzibar.
Baada ya
kufutwa kwa matokeo hayo, na kuitishwa tena uchaguzi, uliopewa jina la uchaguzi
mkuu wa marudio, ambao uligomewa na baadhi ya vyama kikiwemo cha kikuu cha
upinzani CUF, ulimpa ushindi mnono mgombea wa CCM.
Ndio huyo dk
Shein, ambae aliibuka na ushindi mpana wa asilimia 91.4 na kuwaacha masafa
washindani wenzake wengine 13 ambao walikuba kushiriki uchgauzi huo.
Kuapishwa Machi
24 mwaka jana kwa rais huyo mteule, ni ishara kwamba anaingia Ikulu ya Zanzibar
kwa kipindi chake cha pili na cha mwisho cha miaka mitano mengine, baada ya
kubisha hodi kwa mara ya kwanza Novemba mwa 2010.
Bila shaka
sasa, kazi ya kuiongoza nchi ndio inaendelea na hasa, baada ya kupanga na
kupangua baraza la mawaziri ni utekelezaji wa ahadi.
Si unajua
kuwa, kabla ya kuingia kwenye mchakato wa kupiga kura, alipita majimbo yote 54
ya Zanzibar na kutangaaza sera zake makini, mipango, mikakati na nini atafanya
pindi akirejea Ikulu.
Pamoja na
chama CCM kutawala tokea mwaka 1977, kabla ya ASP Tanzania bara na Visiwani, ilikuwa
kazi rahisi ya kuwashawishi wananchi, ili wakiunge mkono, si unajua imeshafanya
mengi.
Na sasa dk
Shein yuko ndani ya Ikulu ya Zanzibar, akiamini kuwa kuweko huko, ni kutokana na
kutangaaza vyema sera zake na kisha wananchi kuwaminia kura kwa ahadi zake.
Sasa
wafanyakazi wa SMZ, wanakumbuka wakati dk Shein akiwa kisiwani Pemba, kwenye
uwanja wa Gombani ya kale, kwamba aliwaahidi kupandisha mishahara juu.
Aliwaahidi
wafanyakazi hao, akipata ridhaa ya kuongoza tena Serikali kwa kipindi cha miaka
mitano ijayo, atahakikisha ndani ya mwaka mmoja wa kwanza, anaboresha mishahara
ya wafanya kazi kwa kima cha chini, kuanzia na shilingi laki tatu (300,000).
Naamini,
wapo waliovutiwa na ahadi hiyo, na ndio maana leo hii, wanajisifu kwamba
wameshamuweka Ikulu dk Shein, wakiamini kwa uungwana wake, atatimizi hilo ndani
ya mwaka mmoja wa kwanza.
Kwa hesabu
za darasa la saba, tokea rais huyo ale kiapo ‘oath’ Machi 24 mwaka jana, sasa
ameshatimiza mwaka mmoja, na pengine mwezi mmoja hivi, ambapo naamini ndani ya
kipindi hicho wafanyakazi watakuwa tayari wanasaini shilingi laki tatu.
Naamini dk
Shein ambae anamaliza muhula wake wa pili kuiongoza Zanzibar, kilio cha
wafanyakazi, wakiwemo wa Ikulu anayoiongoza kitanyamaza walau kidogo, maana
sasa mwezi huu wa April ndio wanasaini kima alichokiahidi.
Dk Shein
kama kiongozi wa nchi kwake ni mwiko kutoa ahadi kisha asiitekeleze, maana wapo
kwa sasa wanaoshuhudia ujenzi wa miundombini ya barabara na maji safi na salama
kwenye maeneo yao.
Hapa leo
sitaki niwataje wazee wale waliofikia umri wa miaka 70, ambao kila mmoja kwa
kituo chake, anaramba shilingi 20,000 nayo hiyo ni ahadi ya dk Shein.
Nikutajie
nyengine, kupandisha bei ya zao la karafuu shilingi 14,000 ambapo sasa wakulima
ile asilimia 80 inabaki kwao, na asilimia 20 ndio inayoingia serikali.
Sasa na hili
la mishahara wala kwake sio jambo kubwa, maana amaeshafunua ukurasa wa mapato
ya serikali, na sasa mwezi huu wa April ndio wafanyakazi watachekelea shilingi
300,000.
Umakini
wake, wa chama chake na watendaji wanaomsaidia kazi ndio, leo hii amekuwa gwiji
wa kuahidi na kisha kutekeleza ahadi zake taratibu.
Mkame Haji
Juma, yeye ni mfayakazi kwenye taasisi ya mifugo, anasema hajaamini sana,
kwamba ndani ya kipindi cha mwaka mmoja, kima cha chini cha mshahara kitakua
shilingi 300,000.
“Unajua
ahadi za kuongezea huwa zipo kila muda, sasa kama Dk Shein ameshaapishwa na
kuingia Ikulu rasmi, twangonjea kwa hamu fedha hizo mwezi huu’’,anasema kwa
furaha.
Lakini
mfanyakazi wa wizara ya elimu Pemba, Maryam Haji Mohamed anasema, hakuna sababu
kwa Dk: Shein kulichelewsha hilo, maana aliliahidi kwa kinywa kipana.
Hashim
Mmanga Muhunzi, ambae nae kwa sasa anapokea shilingi 150,000 ambao ndio kiwango
cha chini cha mashahara wa SMZ, anaamini rais hilo atalitekeleza.
Yeye anasema
kwa sasa chakula kimepanda bei na kufikia wastani wa shilingi 55,000 hadi
shilingi 58,000 kwa kipolo kimoja cha mchele chenye ujazo wa kilo 50.
“Ukishanuanua
mchele, sabuni ambayo kilo moja ni shilingi 2000, sukari ambayo kilo ni
shilingi 2000, hapo hujatokezea kuumwa katikati ya mwezi, wala hujaangalia
dagaa, basi unajikuta mshahara hautoshi’’, alilalamika.
Hata bibi Asha
Omar Makame wa Halmashauri, alisema wafanyakazi waliowengi, wamekosa hamasa ya
kazi kutokana na maisha kupanda na kisha mshahara kuwa mdogo.
“Kama rais
wetu mteule akitekeleza ahadi yake ndani ya mwezi huu kama alivyoahidi kwenye
kampeni yake, basi kidogo nidhamu ya kazi itakuwepo”,anafikiria.
Ussi Salim
Khamis ‘babu’, yeye anasema wakati serikali inayoongozwa na Dk Shein, ikitaka kutimiza ahadi yake hiyo, lazima iwe
karibu mno na wafanyabiashara maana wamekuwa na tabia kupandisha bei za bidhaa.
“Mwaka mmoja
wakati SMZ, baada ya kuongezea asilimia 25 kwa wafayakazi, kila mfanyabiashara
alipandisha bei za bidhaa na hawakuulizwa, sasa na mwaka huu, uangalifu
unahitajika’’, alishauri.
Walishasema
wahenga kuwa haba na haba hujaza kibaba, na bandu bandu huusha gogo, hata kama
fedha haitoshi, lakini wafanyakazi wanaamini kama kiwango kikiwa kama
kilichoahidwa, kibaba kitajaa.
Wazee wa
kijiji cha Micheweni Pemba, kila siku husema hakuna kupata kidogo, wala apewaye
hawi sawa na arambishwaye, maana kupewa unaongeza.
Wafanyakazi
wa SMZ kupitia shirikisho la vyama vya wafanyakazi Zanzibar ZATUC, na Katibu Mkuu
wao Khamis Mwinyi Mohamed, wamekuwa wakilalamikia kila uchao, maslahi bora kwa
wafanyakazi.
Hazipiti
sherehe za siku ya wafanyakazi ‘Mei day’ bila ya ZATUC kuililia serikali kutaka
kuwanawirishia maslahi mazuri wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na vitendea kazi.
Kama Dk
Shein atatekeleza ahadi yake hiyo, itakuwa hii ni mara ya pili katika kipindi
kifupi, kwa serikali kupandisha mishahara ya wafanyakazi, ambapo awali
ilipandisha kwa asilimi 25, ambapo wakati huo walikuwa wakipokea shilingi
100,000
Hapo
ulifikia shilingi 125,000 na kisha kujivuta tena hadi shilingi 150,000, ambapo
kama ndani ya mwezi huu dk Shein, atatekeleza tena ahadi yake, itakuwa ni kwa
asilimia mia moja, na kufikia shilingi 300,000.
Marekebish yaliofanywa na SMZ ni yale mwanzoni mwa wa mwaka
2011, pia mwishoni mwa mwaka 2013 na mwanazoni mwa mwaka 2014, ambapo ilipandisha
kima cha chini cha mshahara kutoka shilingi 125,000 hadi shilingi 150,000 sawa
na asilimia ishirini (20).
Lakini SMZ imekuwa haiangalii tu kupandisha mishahara kwa
wafanyakazi, bali hata kuimarisha utendaji wa kazi kwa kuwapatia vifaa vya
kazi, mafunzo, afya na usalama, kutunga sera, sheria na kanuni za utumishi bora
pamoja na kukuza ushirikiano na Shirikisho la Vyama huru vya wafanayakazi.
Yote kwa
yote wafanyakazi wa SMZ sasa wanakaa vinywa wazi wakisubiri ahadi ya dk Shein, ya
kupandisha mshahara wa shilingi 300,000
ndani ya mwezi huu kutoka shilingi 150,000 wa sasa hadi shilingi
300,000.
Wakati
akitoa ahadi hiyo, alisindikiza na maneno kwamba, lazima nao uwajibikaji kwenye
sehemu za kazi kwa wafanyakazi uimarike, ili wananchi wapate huduma kwa wakati
wanapofika kwenye sekta za umma.
Kiwango
hicho cha fedha, ambacho atakiongeza kwenye mishahara kinawezekana ikiwa uchumi
wa Zanzibar nao utakuwa na kuongezeka, kwani
Serikali anayoiongoza imepiga hatuwa katika ukusanyaji wa mapato kutoka asilimia
4.5 hadi kufikia asilimia 7.2 kwa mwaka.
No comments:
Post a Comment