Habari za Punde

Rais wa Zanzibar Dk Shein Ziarani Nchini Djibout

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar                                                                06.05.2017
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein anaondoka nchini leo kwenda Jamhuri ya Djibouti kwa ziara ya siku tatu kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Ismail Omar Guelleh.

Ziara hiyo ya Dk. Shein inatarajiwa kuanza kesho tarehe 7 na kumaliza tarehe 9 nchini humo ambapo ataanza ziara yake kwa kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais wa Djibout Ismail Omar Guelleh.

Aidha, katika ziara yake hiyo, Dk. Shein atatembelea miradi mbali mbali ya maendeleo nchini humo ambapo miongoni mwa miradi hiyo atakayoitembelea ni Bandari ya  Doraleh, Bandari ya Ziwa Assal, Maeneo Huru ya Uchumi pamoja na Kampuni ya Simu na Mawasiliano “Djibouti Telecom Haramous”.

Katika ziara hiyo, Dk. Shein amefuatana na viongozi mbali mbali akiwemo Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafiri,  Balozi Ali Abeid Karume, Waziri wa Afya Mahamoud Thabit Kombo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afika Mashariki Dk. Susan Alphonce Kolimba.

Wengine ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Uwekezaji Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA) Salum Khamis Nassor, Mshauri wa Rais Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa, Uchumi na Uwekezaji Balozi Mohamed Ramia Abdiwawa pamoja na watendaji wengine wa Serikali. 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein anatarajiwa kurejea nchini Jumaatano Mei 10, 2017.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.