Baadhi ya Nchi zinazoshiriki mashindano ya Riadha kwa vijana waliochini ya miaka 18
yaliyoshirikisha nchi saba za Afrika Mashariki na Kati
yanayofanyika kwa siku mbili katika Uwanja wa Taifa Dar es Salam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.
Dkt Harisson Mwakyembe (katikati) akizungumza leo Jijini Dar es Salaam
wakati alipokuwa anafungua mashindano ya Riadha kwa vijana waliochini ya miaka 18
yaliyoshirikisha nchi saba za Afrika Mashariki na Kati
yanayofanyika kwa siku mbili katika Uwanja wa Taifa Dar es Salam Tanzania
ikiwa ndio mwenyeji wa mashindano hayo.Kushoto ni Mkamu wa Chama cha Riadha Tanzania
Dkt. Hamad Ndee.
Mshiriki wa Riadha kwa vijana walio chini ya miaka 18 wanaoshiriki mashindano ya Afrika Mashariki na Kati Bi Keflin Kipili kutoka Tanzania
akila kiapo cha utii kabla ya kuanza mashindano hayo leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt Harisson Mwakyembe (wa kwanza kulia)akimvalisha medali mshindi wa mchezo wa kurusha mikuki Bi Mwanaamina Hassan kutoka Tanzania katika mashindano ya Riadha kwa vijana walio chini ya miaka 18 yaliyoshirikisha nchi saba za Afrika Mashariki na Kati Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.
Dkt.Harisson Mwakyembe (wa kwanza kulia)
akimvalisha medali mshindi wa mchezo wa kurusha mikuki Bw.Najim Ally
kutoka Zanzibar katika mashindano ya Riadha kwa vijana walio chini ya miaka 18
yaliyoshirikisha nchi saba za Afrika Mashariki na Kati leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.
Dkt.Harisson Mwakyembe (katikati)
akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Riadha na Washindi wa mashindano ya Riadha kwa vijana waliochini ya miaka
18 yaliyoshirikisha nchi saba za Afrika Mashariki na Kati Jijini Dar es Salaam.
Na. Shamimu Nyaki -WHUSM
Mchezo wa Riadha umekuwa na mchango mkubwa katika kukuza na kuimarisha ushirikiano baina ya Afrika Mashariki na
Kati kwa kuwa nchi wanachama wamekuwa wakifanya mashindano mbali mbali yaliyochangia kuleta ukaribu miongoni mwa Jumuiya hiyo.
Hayo yamesemwa leo Jijini
Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.
Harisson Mwakyembe alipokuwa akifungua mashindano ya Riadha kwa vijana wenye umri chini ya Miaka
18 yaliyojumuisha nchi saba za Afika Mashariki na Kati
ambapo ametumia nafasi hiyo kuwahamasisha vijana wenye vipaji na uwezo wa kufanya riadha kutumia mashindano hayo kama njia ya kujifunza na kufanya vizuri.
“Mashindano haya ni mazuri yanatoa hamasa kwenu vijana kuyatumia kama njia ya kujifunza ili mfanye vizuri kama wanariadha wengine waliowahi kufanya vizuri na wanaoendelea kufanya vizuri ndani na nje ya Afrika lakini
pia yametuunganisha sisi wana Afrika Mashariki na Kati
pamoja na kuimarisha uhusiano wetu ”Alisema Mhe. Waziri.
Kwa
upande wake Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Tanzania Bw. Filbert Bayi ameeleza kuwa mchezo wa riadha umeanza kurudi katika hadhi yake ya zamani baada ya vijana wengi kuanza kuupenda na kushiriki mashindano mbali mbali ya riadhaa mbayo yamekuwa yakiwapatia mafanikio.
“Hivi sasa riadha imeanza kupendwa na vijana wengi wanajitokeza katika mchezo huu na mashindano mbali mbali wakiwa na ari kubwa ya kutamani kufika mbali tu nachotakiwa kufanya ni kuwaunga mkono,”
Aliongeza Bw Filbert.
Naye Mshiriki wa Mshindi wa Mita
100 kutoka Tanzania Bi
Keflin Kipili amesema kuwa riadha ni mchezo unaoleta mafanikio hivi sasa Ulimwenguni kwa vijana kama yeye hivyo ni vyema kwa vijana kutumia vipaji walivyonavyo na kutumia kupata mafanikio zaidi.
Katika mashindano hayo Nchi ya
Kenya imekuwa kinara kwa kuibuka kidedea kwa kushinda medali tatu za dhahabu katika mbio za mita
800 Wasichana na Wavulana, pamoja na mita 3000 Wavulana huku Tanzania ikiibuka kidedea katika mbio za mita
100 Wasichana, kubadilishana vijiti (relay)Wasichana na Wavulana.
Mashindano hayo ya siku mbili yanafanyika Jijini
Dar es Salaam yanahusisha Nchi saba za Afrika mashariki na Kati ambazo ni Tanzania
ambao ndio wenyeji, Kenya, Zanzibar, Somalia, Sudan Kusini na Eritrea.
No comments:
Post a Comment