Habari za Punde

Tangazo la nafasi za kazi Wizara ya Fedha na Mipango

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa ajili ya Wizara ya Fedha na Mipango Unguja na Pemba kama ifuatavyo:-

NAFASI ZA UNGUJA

IDARA YA BAJETI:
1. Afisa Kodi Daraja la II “Nafasi 2” - Unguja 
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu elimu ya Shahada ya kwanza katika fani ya Usimamizi wa kodi ‘Taxation Management’ au inayolingana na hiyo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

IDARA YA MHASIBU MKUU WA SERIKALI:
1. Afisa uchumi Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uchumi’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

2. Wahasibu Daraja la II “Nafasi 13” – Unguja 
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uhasibu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

3. Msaidizi Muhasibu Daraja la III “Nafasi 1” - Unguja 
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Stashahada katika fani ya ‘Uhasibu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

4. Mkaguzi Daraja la II “Nafasi 2” - Unguja 
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uhasibu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

IDARA YA MIPANGO SERA NA UTAFITI:
1. Afisa Sera Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Sera na Mipango’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 



2. Afisa Utafiti Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Mipango’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

3. Afisa Takwimu Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Takwimu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

IDARA YA UENDESHAJI NA UTUMISHI:
1. Afisa Tehama Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘IT’ au ‘Computer science’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2. Dereva Daraja la III “Nafasi 2” – Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu elimu ya Sekondari.
Awe amepata mafunzo ya udereva kutoka katika Chuo cha mafunzo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

3. Taarishi Daraja la III “Nafasi 2” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu elimu ya IV na kufaulu.

4. Afisa Msaidizi Ukutubi Daraja la III “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Stashahada katika fani ya ‘Ukutubi’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

IDARA YA UHAKIKIMALI NA MITAJI YA UMMA:
1. Afisa Mahitaji ya Umma Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uchumi’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2. Msaidizi Afisa Uhakikimali Daraja la III “Nafasi 2” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Stashahada katika fani ya ‘Ununuzi’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

IDARA YA FEDHA ZA NJE:
1. Afisa Uchumi Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uchumi’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2. Afisa Sheria Daraja la I “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Pili katika fani ya Sheria na Uhusiano wa Kimataifa (Master of Law in International Relation’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

NAFASI ZA PEMBA:

1. Mlinzi Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Muombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amemaliza elimu ya Sekondari.
Awe amepata mafunzo ya Ulinzi (Mgambo au JKU)

2. Muhudumu Daraja la III ‘Nafasi (1) - Pemba
Sifa za Muombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu elimu ya Sekondari na kupata cheti cha uhudumu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

3. Muhasibu Daraja la II “Nafasi 1” – Pemba 
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uhasibu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

4. Muhakikimali Msaidizi Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba 
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Stashahada katika fani ya ‘Ununuzi na Ugavi’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

5. Afisa Utumishi Daraja la II “Nafasi 1” – Pemba 
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Utawala’ au ‘Rasilimali Watu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

6. Karani Masjala Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba 
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Stashahada katika fani ya ‘Utunzaji Kumbukumbu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

Jinsi ya Kuomba:
Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU, 
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.