HABIBA ZARALI, PEMBA.
WANAUSHIRIKA wa vikundi mbalimbali vya Saccos Wilaya ya
Mkoani kisiwani Pemba, wamesema katika kuhakikisha Saccos za wilaya
zinafanikiwa ni vyema taasisi husika wakatowa elimu ya kutosha kwa wanavikundi
na wananchi kuhusiana na uanzishwaji huo.
Walisema
iwapo hatuwa ya haraka ya kutoa elimu kupitia vikundi hivo sambamba na
kuvitumia vyombo vya habari kutachangia kwa kiasi kikubwa kuwawezesha wananchi
kuelimika .
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti Wanasacos hao ,walisema ingawa tayari wameshanza kupata
elimu lakini bado hawajafahamu lengo la la ujio wa Saccos hiyo na hawajafahamu
saccos za kawaida zitakuwa katika hali gani baada ya kuja kwa saccos za Wilaya.
Katibu
wa “CHOKOCHO SACCOS” Mohammed Issa Mohammed, alisema wazo la kuja kwa Saccos za
Wilaya ni zuri na linaweza kuwasaidia lakini bado wanahitaji elimu zaidi ya
kujuwa saccos za kawaida zitakuwa na
hali gani hasa ukizingatia zinatoa
huduma kwa wananchi wake.
“Hadi
sasa wananchi hawajakataa kujiunga na Saccos ya Wilaya baada ya kuanzishwa
lakini wanalohitaji ni kufahamu saccos zao za kawaida zitakuwa katika
hali gani”alisema.
Alisema
iwapo itatolewa elimu kupitia vipindi mbali mbali wananchi watajuwa masharti ya kujiunga kwa
vile kuna baadhi ya Saccos zao kwenye masuala ya mikopo hakuna riba.
Mjumbe
wa Saccos hiyo, Juma Khamis Kombo,
alisema uanzishwaji wa saccos za Wilaya ni vyema ukaangalia zaidi umuhimu wa
saccos za kawaida kwani zinawasaidia sana na endapo zitavunjwa na kupelekwa
sehemu nyengine itakuwa bado lengo lao halijafikiwa.
“Katika
Saccos zetu tunajiendesha vizuri na tunajisaidia vyema kupitia mikopo na hali
zetu za maisha zinaimarika”alisema.
Mshika
fedha wa kikundi hicho, Fatma Chum Omar, alisema ili uanzishwaji huo uweze
kufanikiwa ni lazima kuwe na umoja kati ya wanasaccos wa kawaida na taasisi
husika inayoshughulikia saccos hizo .
Hivyo
alisema ni vyema wanasaccos mbali mbali kutowa elimu ndani ya vikundi vyao
pamoja na kwa wanajamii ili uanzishwaji huo uweze kufanikiwa kama ulivyopangwa.
No comments:
Post a Comment