Habari za Punde

-Mfungo wa Ramadhani, Mwezi Mwafaka wa Kuihasimu Sigara -Njia Sahihi za Kutengana na Sigara Milele Hizi.

Na. Haji Nassor. Pemba.
WAUMINI wa dini ya kiislamu duniani kote, wanaendelea na mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhan, ikiwa ni nguzo ya nne kati ya zile tano za kiislamu.
Mwezi huu mtukufu wa ramadhani, huja mara moja kila mwaka, nao kama ilivyo miezi mengine, huwa na makumi matatu, ingawa ya mwezi huu, hutaja kuwa ni ya thamani zaidi.
Maana maandiko yasiokuwa na shaka, yanaeleza wazi wazi kuwa, siku kumi za kwanza huwa ndio za rehma, wakati za pili huwa ndio za maghufira na mwisho ni touba, (maarufu kama kuachiwa huru na moto).
Hakuna shaka kuwa, ubora wa mwezi huu au tofauti kubwa na miezi mengine ni kwamba, huu ndio uliotajwa kushushwa maadiko matakatifu ya ku-ran.
Kumbe, mwezi huu ni mtakatifu na wenye kheir na neema kadhaa, hadi masheikh na wanazuoni kutuelezwa kuwa, hata ukifanya jambo jema, basi malipo yake ni mara dufu.
Kama hivyo ndivyo, waislamu wenzetu hasa wanaotumia miuriji ya uvutaji wa sigara, hawajiskii ovyo na wapotevu kuendelea kurusha moshi ndani ya mwezi huu mtakatifu?
Tena mchana mzima, kwa maana zaidi ya saa 12 inawezekana wapo wanaojizuia na uvutaji wa sigara, kwa sababu za kuwa na swaumu, ingawa baada ya futari huendelea na kazi yao.
Huu muda wa kujiweka mchana pasi na kuvuta sigara kwa saa kadhaa, kwanini isiwe sababu kwa wavutaji kuacha moja kwa moja, hasa kwa vile faida yake haionekani.
Chakupendeza zaidi kama sio cha kufurahisha, hakuna dini hata moja iliorasmi, ambayo inasisitiza na kuhalalisha uvutaji wa sigara, maana hasa sigara, imebeba magonjwa zaidia 300.
“Utampendeza Muumba wako, wapendwa acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili.” ( wakorintho 2 7:1) “mtoe miili yenu ikiwa takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu.”waroma 12:1.
Ndivyo ukiristo ulivyonadi, juu matumizi ya sigara, lakini hata dini ya kiislamu nayo, umeshatamka kuwa “ wanakuuliza wamehalalishiwa nini, sema mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri (Al-Maaidah, 5:4)
Mwezi huu mtukufu wa ramadhani, ndio adhimu na adimu kwa mwenye kutaka kuacha matumizi ya moshi wa sigara, na zipo njia na mikakati kadhaa, ambayo kama ukiyafuata basi waweza kufanikiwa.
NIA: kila jambo kwanza linahitaji nia ya kweli, maana pasi na kuweka na kuufunga moyo wako na nia wala mvutaji hatoweza, kufikia lengo lake.
Kupanga muda: kwa mfano kwa mwezi huu mtukufu wa ramadhani, ndio mahasusi na adhimu, maana wavutaji waliowengi na hasa waislamu, ambao wameshaambiwa kuwa, wanapata madhara, basi ni wakati ndio.
Mwezi huu mtukufu wa ramadhani, huja mara moja kwa mwaka, na siku zake hazizidi 30, sasa lazima wanaotaka kuacha moja kwa moja, wajipunguzie dozi, kwa mfano wanaovuta sigara 12 kwa siku, waanze kupunga mmoja moja.
Au kama wanakawaida ya kuvuta sigara miongo minne kwa siku, sasa wanze kujivuta kwenye mitatu na kuelekea miwili, ili ubakie mmoja na kisha kuacha kabisa.
Ingawa, wapo wataalamu na watafiti, wanapinga suala la kujipunguzia idadi ya sigara kwa siku, wakisema inaweza kupandisha nikotini juu, na wanashauari baada ya kujipangia ikifika tarehe ni kuacha moja kwa moja.
Kuimarisha azimio la kucha: kwa mwenye kuacha sigara hasa ndani ya mwezi huu mtukufu wa ramadhani, ni rahisi kama ataendelea kuimarisha azimio lake, ikiwa ni pamoja na kumuomba Muungu hasa nyakati za usiku.
Kukaa na waliofaulu: kwa muachaji wa sigara inapendeza azimio na kusudio lake na kuacha kutumia sigara, basi kukaa na wale waliofanikiwa kucha, maana ndio ambao wameanza na kufanikiwa.
Si vyema kiushauri kwa mwenye kuacha sigara, kubakia na rafiki wa kweli anetumia sigara, na anapaswa sasa abadili marafiki na kuachana na marafiki watumiaji.
Kujiandaa na madhara mengine: Wataalamu wanakubali kabisa kuwa asilimi 90 ya wale wanaocha sigara, hupata dalili za ajabu, mfano hamu ya kutumia nikotini.
Aidha wajielewa kuwa wanaoacha sigara, pia wanaweza kukumbwa na dalili za kuchefua chefua moyo, kujiskia mgonujwa, kichwa kuuma au hata kutokwa na subra.
Dalili hizi hutajwa kujitokeza kutokana na mwili, kukosa nikotini iliokuwa ya kawaida mwilini kwa mvutaji wa sigara, ambapo hujitokeza ndani ya saa 12 hadi saa 24, baada ya kucha, ambpo ni ndani ya wiki mbili hadi sita.
Usikate tamaa: Inawezekana ndani ya mwezi huu mtukufu wa ramadhani, mvutaji akashindwa kuacha kwa sababu moja ama nyengine, basi sio vyema kukata tamaa.
Wapo wanaokata tamaa mara moja, hasa wanaposhindwa kwa mara ya kwanza, hali hiyo haishuriwi na inatakiwa kuendelea kung’ang’ania kuacha.
Kwa mwezi huu pekee, ndio rahisi kwa wavitaji wa sigara au watumiaji wengine wa vilevi, kuacha kutokana na waliowengi mchana mzima kutotumoa viburudishaji hivyo kwao.
Maana Khamis Haji Makame wa Wawi Chakechake, yeye sasa anatimiza miaka 12 tokea alipoacha sigara, ingawa alishautumia miaka kama hiyo.
Yeye anasema alishauriwa kuacha sigara mwezi kama huu mwaka 2005, na alikaribia kushindwa hasa kwa vile alipata magonjwa kadhaa, ikiwa ni pamoja na kichwa kuuma sana.
“Mimi nia ya kuacha sigara ndio ilionifanya, leo nisherehekee miaka 12 ya kuihasimu sigara, sasa kila aliweke nia ya kweli ya kucha basi atafanikiwa”,alishauri.
Hassina Haji Mohamed wa Kengeja, anasema yeye alitumia nguvu kiasia fulani mwezi kama huu, mwaka juzi kwa kuzitupa sigara za mumewake, na sasa anatimiza miaka miwili bila ya kutumia.
“Tuligombana sana na mume wangu juu ya matumizi ya sigara, lakini kwa vile alinikubalia, sasa ameshaacha kwa msaada wangu na yeye kutaka”,anasema.
Mume huyo ambae kwa sasa yuko Unguja kwenye shughuli zake za biashara ya ndizi, Kombo Omar Kombo akizungumza na ukurasa huu anasema nia ya kuacha matumizi ya sigara, alishaijaribu mara nne bila ya mafanikio.
“Mimi mke wangu ndie mwalimu wangu wa mimi kuacha sigara, maana ndani ya ramadhani ya mwaka juzi, namuuliza sigara zanguza ziko wapo, akanijibu amezitupa tena kwa ukali, lakini leo nimeashanikiwa kuihasimu sigara”,anaeleza.
 Hali ya kiafya ya watu ambao wanavuta sigara inazidi kuwa mbaya baada ya Shirika la Afya Duniani (WHO), kutoa ripoti ambayo inaonyesha, hivi karibuni kutakuwa na watu milioni nane (8), ambao watakuwa wanakufa kila mwaka kwa sababu ya uvutaji sigara.
Vifo hivyo vimeripotiwa kuwa, vitakuwa vikitokana na magonjwa ambayo watumiaji wa sigara wanakuwa nayo kutokana na matumizi ya sigara, kuonekana kuongezeka ambapo kwasasa inakadiriwa kuwa zaidi ya dola trilioni moja, kutumika kila mwaka kwa ajili ya kununua sigara.
Vifo vya watu ambao wanatumia bidhaa ambazo zinatokana na tumbaku itapanda kutoka watu milioni sita, hadi milioni nane ifikapo mwaka 2030, nchi ambazo zitaathirika zaidi ni zenye uchumi mdogo na wa kati,” ilisema ripoti hiyo.
Wataalamu wa afya wanasema kuwa bidhaa za tumbaku ni moja ya vitu hatari kwa afya, na ambavyo vimekuwa vikisababisha vifo vya watu wengi, lakini bado idadi ya watumiaji wake inazidi kuongezeka kwa kasi katika maeneo mbalimbali duniani.
Kuvuta moshi wa sigara inayotumiwa na mtu mwingine kumechangia pakubwa, katika mjadala juu ya madhara na udhibiti wa bidhaa za tumbaku.
Tangu mapema miaka ya 1970, sekta ya tumbaku imekuwa na wasiwasi kuhusu kuvuta moshi wa sigara, inayotumiwa na mtu mwingine kama tishio kubwa kwa maslahi ya biashara yake.
Aidha taarifa hiyo, ikaenda mbali na kwamba, sigara moja inakemikali zaidi ya 480,069 kati ya hizo zinasababisha kansa ingawa pia asilimia 69 ya wavuta sigara, wanatamani kuacha kabisa, ingawa wameshindwa.

Taarifa inaeleza kuwa, sigara billion 15 huvutwa kila siku dunia kote ikiwemo hapa Zanzibar, ingawa bwana Adolf Hitler wa Marekeani ndio mtu wa kwanza, kuanzisha kampeni ka kuzuia uvutaji sigara katika historia ya hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.