Habari za Punde

Bonanza la michezo kisiwani Pemba lafana

Wananchi wakishiriki katika mchezo wa ngombe wakati wa Bonaza la Tamasha la Weekend Pemba lililofanyika kwa michezo mbalimbali kisiwani humo. Na kurushwa moja kwa moja na Kituo cha TV cha Azam. Moja kati ya wachezaji wa mchezo wa Ng’ombe akikosea hatua ya kupiga ngea na kujikuta akigaragazwa na Ng’ombe mwenye hasira
Baadhi ya Wananchi Kisiwani Pemba wakifuatilia mchezo wa resi za ngalawa wakiwa katika ufukwe wa pwani ya vumawimbi kujionea burudani mbali mbali
Mshindi wa kwanza wa mchezo wa mbio za baskeli wakati wa Tamasha hilo la Bonaza Kisiwani Pemba Ndg .Othman Said Khamis Mshindi wa kwanza wa mchezo wa resi za baiskeli aliejinyakulia Tsh 500,000/=

Viongozi waalikwa waunga mkono juhudi za Rafiki Network.                                              
Washindi na washiriki wa michezo mbali mbali wazawadiwa.

AZAM TV washangwazwa na ukubwa wa matukio.

Na.Ali Othman Ali
Tamasha kubwa la kimichezo Kisiwani Pemba lijulikanalo  kwa jina la Pemba weekend Bonanza limefikia kilele chake leo katika Fukwe za vuma wimbi ambako washindi na 
washiriki wa michezo mbali mbali wame kabidhiwa zawadi.

Akikabidhi zawadi zilizoandaliwa na Kampuni ya Rafiki Network kwa washindi 30 wa mchezo wa resi za baiskeli ambao waliingia hatua ya fainali na kupambana kishujaa 
kutafuta mshindi wa kwanza, wapili na watatu ambao waliahidiwa kuzawadiwa 500000/=, 300000/= na 200000/= 
kwa mpangilio, Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Mheshimiwa Rashid Ali Juma ameahidi kwamba mbali na zawadi hizo Wizara yake itawapatia fedha taslim Tsh 50000/=  washiriki wengine 27.

Aidha Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Mh.Mmanga Mjengo Mjawiri ametoa fedha taslim  Tsh 20000/= kwa waogeleaji wote walioshiriki mashindano ya kuogelea 
mara baada ya kukabidhi Ts 300000/= kwa mshindi wa kwanza 200000/= kwa mshindi wa ili na 100000/= kwa mshindi wa tatu kutoka kwa kamuni ya Rafiki Network.

Mchuano mkali wa resi za Ngalawa ulichomoza katika usawa wa bahari ya vumawimbi kutokea bandari ya Tumbe na kusababisha taharuki na hamu yakutaka kujua nahodha gani ataibuka mshindi wa michuano hiyo ya kihistoria abapo Ngalawa ijulikanayo kwa jina “Tutaonana juu” ikiongozwa na nahodha Hassan Abdallah kutoka makangale iliibuka mshindi nakujinyakulia fedha Taslim Tsh 300000/=.
Kwaunde mwengine Meneja wa Ufundi na Uzalishaji wa 

AZAM TV Nd. Said Meb amesema hakutegemea kwamba tukio la Pemba weekend Bonanza lingekua na ukubwa alioushuhudia nakwamba amesikitishwa na maandalizi yake 
akidai kwamba hayakuweza kukidhi ukubwa wa tukio hilo.

“Kabla nilijua ni matukio machache na madogo lakini hali imekua tofauti kwani ni shughuli kubwa ambayo ingehitaji tuchukue zana na vifaa zaidi ya tulivyokuja navyo” amesema 
bwana Meb

Tamasha hili lilizinduliwa rasmi siku ya Ijumaa ya 28 Julai katika viwanja vya skuli ya Chwale  Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini pemba ambapo mamia ya mashabiki waliohudhuria walishuhudia wataalamu wakionesha umahiri wa kupiga ngea.

Hili nitamasha la kwanza kufanyika likiandaliwa na Kampuni ya Rafiki Network na linatarajiwa kuwa endelevu kwa kufanyika kila mwishoni mwa wiki ya mwisho ya mwezi Julai kila mwaka.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.