Habari za Punde

Kavukavu za Bi Hekima: Basi mpaka Maimaam huachiwa tu!?

Na Bi Hekima

Hizi kavu kavu zinadorora si kwa sababu hakuna ya kuyaandikia au kuyasemea. Yapo mengi. Lakini hakika huwa nazidiwa na kiwango cha ujutar, ulimbukeni, ukavu, ukaidi, usugu, utovu wa adabu ninao ushuhudia kila siku nasawijika na kuishiwa nguvu...inataka stamina kweli si tu kuyahimili lakini pia kuyakabili yote haya.... 

Nataka kurudia suala nililoliandikia mara ya mwisho kwani ni sugu na linatuumiza kwa namna tofauti.

Katika Ramadhan za mwisho nlijaaliwa kusali taraweh moja Msikiti wa Mwembe Shauri. 

Tulipoendelea na sala nilibaini kuwa sala nilojumuika kuisali si tena taraweh bali ni witr maana kuna rakaa tumesalishwa moja tukatoa salamu au tatu tukatoa salamu na kuendelea na mbili.

Baadhi ya maamuma walisimama wakitaraji kuendelea na sala wengine walikaa walipofahamu inayosomwa ni tahiyyatu si suratul fatiha tena. 

Watu wakifuata tu ingawa ilikua wazi kuwa kuna tatizo. Ilipotokea mara ya pili nkauliza kama ni mimi nlosinzia au kama kweli tumesali rakaa kasoro? 

Nikaambiwa naam na si mara ya kwanza  Imam kupitikiwa usiku huo. 

Nkataka kujua kwa nn hajatahadharishwa? 

Nkaambiwa mara ya kwanza alitanabahishwa. Ila kadri alipokosea watu wakaenda naye tu.

Nlijaribu kupiga kofi kwa upande wetu lakini watasikia wapi wanaume waliojitenga mbele na vipaza sauti? Nikaamua siwezi kuendelea na sala. Nkatoka kujaribu kuwapata waumini wanaume karibu na imam wasawazishe mambo lakini haijawezekana. Nkaamua kuondoka

 Hivyo kubwa kwangu tena ni namna tusivyoweza kuzuia au kurekebisha jambo likiharibika hata tukaacha litudhuru sote.

Pili ni kwa yuke anayewaponza wenzako ndo kweli hawezi kujiambia? Kama umechoka au huko 100% tabu gani ukaomba msaada ukae pembeni?

Tatizo jengine ni kuwa mara nyingi hakuna wakumpokea yule anayeonekana ndo 'kiongozi'. 

Haiwezekani Imam kakosea au tuseme kazirai yule alosimama pembeni yake asiwe na ujuzi au ufahamu wa kuongoza sala kutokana na dharura. Lakini inavyoelekea watu wanaunga safu bila kuzingatia ujuzi na uwezo wao. Alimradi kasimama katika mstari na kaja kusali!


Hakika kuna mafunzo mengi hapa mengine hata sijayagusia na inafaa tutafakari tumesimama wapi na tumesimama vipi! 

Tuzinduane na tuelekezane mambo ya msingi si mambo yasiotuongezea thamani yoyote katika ufahamu au uzingatiaji wetu.                        

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.