Habari za Punde

Mkufunzi Kutoka Sweden Awapiga Msasa TAEKWON-DO Zanzibar.

Mkufunzi kutoka Nchini Sweden Niklas Enander akimkabidhi vifaa vya mazoezi mmoja wa washiri wa mafunzo hayo yanayofanyika katika ukumbi wa Judoka Amaan Zanzibar,ni mkufunzi anayetambulika na Shirikisho la Taekwon-do Duniani (ITF)
Niklas Enander ni mkufunzi anayetambulika na Shirikisho la Taekwon-do Duniani (ITF) akitowa mafunzo kwa wakufunzi wa mchezo huo Zanzibar 
Na: Abubakar Khatib “Kisandu”, Zanzibar.
Chama cha mchezo wa Taekwon-do visiwani Zanzibar, kimeandaa semina maalum ya siku moja kwa wachezaji wa mchezo huo ambapo mkufunzi wa mafunzo hayo ametoka nchini Sweden.

NIKLAS ENANDER ni mkufunzi anayetambulika na Shirikisho la Taekwon-do Duniani (ITF) ndie aliyeendesha Mafunzo hayo ya siku moja, Mafunzo ambayo yamefanyika Jana Amani mjini Unguja katika ukumbi wa Judo kuanzia saa 3:00 asubuhi na kumalizika saa 11:00 za jioni.

NIKLAS amefurahishwa sana kuona idadi ya wachezaji imezidi tofauti na mwaka jana alipokuja hivyo amezidi kupata moyo wa kuwa karibu na Wazanzibar.

“Nimefurahi sana kuona Wazanzibar wanapenda michezo, mwaka jana nilipokuja wachezaji walikuwa kidogo, lakini mwaka huu idadi imeongezeka, ukweli nimefurahi sana”. Alisema Mkufunzi huyo.

Mchezo wa Taekwon-do asili yake ni nchini Korea kwa lugha nyepesi unaweza ukauwita sanaa ya mapambano na pia unafanana na mchezo wa karati lakini ni tofauti kabisa licha ya kuwa mchezo huo pia wanatumia kupiga mateke na kurusha ngumi .

Mchezo huo unafundishwa katika ukumbi wa Judo Amani Mjini Zanzibar na kocha Maxmiliana Kailangana kwa kila siku ya Jumatatu, Jumatano na Alhamis kuanzia saa 1:00 usiku hadi 3:00 usiku huku kocha huyo akiwataka wadau wengine kujitokeza kushiriki mchezo huo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.