Habari za Punde

Kampuni ya Saruji ya Dongote Yatowa Elimu ya Matumizi ya Saruji yao Kwa Wafanyakazi wa Viwanda Vya Matofali Zanzibar.

Mkurugenzi Mauzo Kanda wa Kampuni ya Dongote Johnson Olaniyi akitowa elimu ya jinsi ya utumiaji na uchanganyaji wa saruji ya Dangote kwa Wafanyakazi wa viwanda vya matofali Zanzibar baada ya kutowa elimu hiyo kwa vitendo katika moja ya viwanja vya ufutuaji wa matofali mtoni Zanzibar mafunzo hayo yamewashirikisha Wafanyakazi na Wamiliki wa Viwanda vya Matofali Zanzibar.
Afisa Mawasiliano wa Kampuni ya Saruji ya Dongote Ferista Masabo akitowa maelezo wakati wa mafunzo hayo kwa vitendo kwa wafanyakazi hao wa viwanda vya matofali Zanzibar.
Mfanyakazin wa kiwanda cha matofali mtoni akionesha jinsi ya uchanganaji wa saruji wakati wa mafunzo hayo.
Wafanyakazi wa viwanda vya upigaji matofali Zanzibar wakifuatilia mafunzo hayo yaliotolewa na kampuni ya saruji ya Dangote Tanzania. 




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.