Habari za Punde

Yalijiri Wakati wa Ziara ya Rais wa Zanzibar Dk Shein Kisiwani Pemba

 WAZIRI asiekuwa na wizara maalum Mhe: Said Soud Said, akiwaambia wananchi wa Mgogoni kuwa, hakuna uchaguzi mwengine hadi mwaka 2020, mara baada ya kupewa nafasi na Rais wa Zanzibar, kujitambulisha kwa wananchi, waliohudhuria uzinduzi wa skuli ya Msingi na kati ya Mgogoni, kazi iliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein
Katibu  Mkuu wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Khadija Bakar Juma, akizungumza machache, mara baada ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein, kuifungua skuli ya msingi na kati ya Mgogoni wilaya ya Wete, ikiwa ni sehemu ya zaiara yake ya siku tano Kisiwani Pemba
 WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe: Riziki Pembe Juma, akizungumza kwenye ufunguzi wa skuli ya mpya ya msingi na kati ya Mgogoni wilaya ya Wete kisiwani Pemba, ambapo skuli hiyo, ilizinduliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi, Mhe: Dk Ali Mohamed Shein, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tano kisiwani Pemba
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein, akiwasalimia wanafunzi na waalimu wa skuli ya Msingi na kati ya Mgogoni wilaya ya Wete, mara baada ya kuizindua skuli yao mpya, ikiwa ni sehemu ya ziara yake, ya siku tano kisiwani Pemba
 WANAFUNZI wa  skuli ya Msingi na kati ya Mgogoni wilaya ya Wete, waliohudhuria uzinduzi wa skuli mpya, kazi iliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein, ikiwa ni sehemu ya zaiara yake ya siku tano Kisiwani Pemba

Jengo jipya la skuli ya msingi na kati ya Mgogoni wilaya ya Wete, ambalo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein, alilizindua, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tano kisiwani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.