Habari za Punde

Chen, Daktari wa Kichina anaetamani kubakia kisiwani Pemba milele Aongoza madaktari saba kutoa huduma Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani

Mwandishi Haji N. Mohamed Pemba.
“Jina langu ni Chen Er Dong, nimezaliwa mwaka 1975 kijiji cha Nan Jing nchini China”.
Tokea niko skuli nilikuwa napenda niwe daktari, hivyo baada ya kumaliza masoma, kwa vile nilikuwa na sifa za kusomea udaktari, nilifanikiwa na kujiunga na chuo nchini China.
“Chuo nilichosoma kinaitwa ‘Nan Jing Medical College’ na mapema mwaka 2002 nilimazalia masomo yangu ya udaktari, na hapo nikaanza kazi kwenye hospitali ya ‘Nan Jing First Hospital”,

Dr.Chen, anasema aliamua kujitupa kwenye fani ya udakatari kutokana na mahaba na kupenda kwakwe kuihudumia jamii moja kwa moja, badala ya kuwa mhandishi ujenzi au kazi ya uwalimu kama alio nayo mama yake mzazi.

“Mama yangu yeye ni mwalimu wa lugha ya kichina na baba ya anajishughulisha kazi zake binafsi, ingawa mimi sikupenda kazi za wazazi wangu, niliamua niwe daktari na sasa ndio mimi nimekuwa’’,anasema.

Anasema maisha ya China nayo sio mepesi sana kama wasiokuwa wachina wanavyofikiria, bali ni kupambana kama ilivyosehemu nyengine duniani.

“Kila kitu ni mapambano, na kila eneo ulilozaliwa lina mapambano yake ya kimaisha kwa mujibu wa mahitaji ya anaepambana na maisha, hata China unabidi upambane ili upate maisha”,anasema.

Ukurasa huu wa makala, ulimuuliza Dr. Chen, iwapo taaluma ya shahada ya pili ya koo, pua na skio, ‘Master Degree’ alionayo kama alisomeshwa na Serikali ya watu wa China, hilo alililipinga.

“Tena afadhali nyinyi huku Tanzania na Zanzibar, nasikia mna bodi za mikopo ya elimu ya juu, ambayo wanafunzi wanaomba na kisha kukukopeshwa fedha za kusoma, lakini mimi China hiyo sijaona na hakuna”,anaeleza.

Hivyo Dr. Chen, ambae kwa sasa ndio kiongozi wa madaktari saba waliopo kwenye Hospitali ya Mkoa wa Abdalla Mzee Mkoani kisiwani Pemba, anasema alisomeshwa na familia yake (baba na mama).

“Kwetu mtoto mmoja kwa familia moja, na pengine ndio faida ya wazazi wangu kumudu kunisomesha hadi leo hii, kuwa daktari ninaetambulika na serikali ya watu wa China na hata Zanzibar’,anafafanua huku akicheka.

Sera ya mtoto mmoja nchini China, ambayo ipo kwa baadhi ya miji, anaamini ni mwarubaini kwa familia yengine nchini humo, kuwapatiwa haki nzuri ya malezi, elimu na hata uangalifu wa kina kwa mtoto wao.

Chen anasema, hakutarajia kwenye maisha yake kupanda ndege kutoka nje ya jiji la China lenye wakaazi zaidi ya billion moja, ingawa mwaka huu wa 2017, ulimuwezesha kutua Tanzania na kisha Zanzibar.

Daktari huyu ambae na yeye ameshatekeleza sera ya kuwa na mtoto mmoja mwenye umri wa miaka mitatu sasa, anasifia sana visiwa vya Zanzibara na hasa Pemba anakofanyia kazi kwa muda wa ammoja ujao.

“Juzi nilikwenda Unguja, nikakaa kwa siku kadhaa, lakini baada ya kurudi Pemba, hapa ni patamu sana na kama sio utaratibu wa nchi yangu, basi natamani nishi na familia yangu milele”,anaeleza.

Chen, kilichomvutia kisiwani Pemba, ni mambo kadhaa moja ni utulivu, pili ukarimu wa watu uliopindukia mipaka, tatu ni wananchi waliopo kupenda wageni na hasa wanapokuwa wanazunguruka mitaani.

Binafsi, anasema hutamani sana muda wa kazi ufike ili akutane na wananchi wa Pemba, ambao anasema wanaonyesha moyo wa tabasamu hata kama, wanaugua.

“Kufanya kazi sehemu yenye utulivu, amani na wenyeji waliopo kupenda wageni, ni jambo jema, na hapa nafikiria siku ambayo nitamaliza muda wangu, sujiui ntakuwa na majonzi kiasia gani moyoni’’,ananisimulia.

Msaidizi wake Dr. Chen, dk He, anasema Chen ni miongoni mwa watu waliokuwa na furaja na furaha, baada ya kupata taarifa ya kwenda Zanzibar kwa ajaili ya kutoa huduma za matibabu.

“Unajua, Chen alikuwa haamini kuwa atafika Zanzibar tena hap Pemba, na baada ya kufika hutamani hata siku zake za mapunziko yeye aweko kazini, maana anawapenda sana watu wa Zanzibar kwa ukarimu na upole wao”,ananieleza Dr.He.

Muda aliofika kisiwani Pemba, kutokana na kujichanganya kwakwe na wazawa, tayari dk Chen anasema anayo maneno zaidi ya 30 ya Kiswahili anayoyajua, ikiwa ni pamoja na “nzuri sana, jambo, hakuna matata, karibu tena.

Maneno mengine ambayo ameshaweka kwenye akili yake ni, wimbo mzima wa malaikaaa…. nakupenda malaikaaa…. hata neno kusema rais za Zanzibar na mengine kadhaa.

Kwa sasa anajiamini kuzungumza sentesi zaidi ya 10 za Kiswahili, anachokiona ni fasaha, mbele ya watu na anasema anajitahidi kila siku ahakikishe ameingiza neno jipya la kiswahili kwenye akili yake.

Dr. huyo, pamoja na wenzake saba, watakuwa kisiwani Pemba kwa siku zisizodi 360, yaani miezi 12, ingawa Chen mwenyewe wala hatamani kuwa, saa 8640 zinazobeba siku za mwaka ziishe na kurudi kwao.

Ingawa kwa timu nyengine za madaktari hao kutoka China tokea walipoanza waka 1972, walikuwa wakikaa miaka miwili, lakini bahati kwa Dr. Chen imekuwa mbaya, maana sasa wanakaa kipindi cha mwaka mmoja tu.

Chen na kundi lake la madaktari wataalamu, linaunda timu ya 27 tokea uhusiano wa China na Zanzibar ulipoanza miaka 45 sasa wa kupokea madaktari, kumbe wakati uhusiano huu unaanza hata Dr. Chen mwenyewe hajazaliwa.

Ndoto zake za kuwa daktari kwa lengo la kuisaidia jamii yake na nyengine, zimeshaanza kudhihirika ndani ya kisiwa cha Pemba, ambapo ndani ya siku 30 tokea wawasili, wameshafika skuli ya Msingi Makombeni wilaya ya Mkoani.

“Juzi tulikwenda Makombeni skuli ya Msingi na tuliwafunza watoto lugha ya kichina kwanza, kisha tukawapa elimu ya kujikunga na athari zitokanazo na ugonjwa wa masikio, pua na koo”,anasema.

Kwa safari ya skuli ya Makombeni, Dr. Chen anasema aliisababisha yeye baada ya kuwepo uhusiano mzuri na mmoja wa madaktari wanaofanya kazi hapo, hadi kumuunganisha na mwalimu Mkuu wa skuli hiyo.

“Wakati tunakwenda Makombeni kutoa huduma hiyo, pia niliwachukulia zawadi wanafunzi hao, ikiwa ni pamoja na penseli, mabuku kwa ajili yao”,anasema.

Mwalimu mkuu wa skuli hiyo, Othaman Machano Mmanga, anasema anafurahia ujio wa madaktari hao kwenye skuli yake, na hasa kuwafanyia vipimo wanafunzi wake.

Anasema, hakuamini jinsi waliovyowaomba madaktari hao bila ya barua au kupita ngazi za juu, na hatimae kuwafanyia vipimo wanafunzi wangu na kisha kuwapa na mabuku na penseli.

Yeye anaona timu zote 27 zilizoanza kuja hospitali ya Mkoa ya Abdalla Mzee Mkoani tokea mwaka 1972, lakini hii ya mwaka 2017, ambayo ndio ya mwanzo itakayokuwepo kwa mwaka mmoja, imefanya kitu tofauti.

“Yule Dr. Chen, alipofika skulini kwangu, kwanza alipenda mandhari, pili alikuwa karibu sana na wanafunzi na wala hakutamani kuandoka na walichelewa kurudi, inaonekana wanapenda sana kucheza na watoto”,ansema.

Dr. Chen kwa sasa ndie mtaalamu pekee kwenye timu hiyo ya madaktari saba, akiwemo yeye wa nane, kwa matibabu ya pua, koo na masikio na lengo lake hasa ni kuwa daktari bingwa na mahasusi hapo baadae ”specialist”.

Anasema hata alipokuwa hospital ya “Nan Jing Fisrt hospital” nchini China, ambayo anayofanyia kazi, anakumbuka kumfanyia mwanamme mmoja matibabu ya giota, na ndani ya siku 10, bila ya kuja juu.

“Siku hiyo ndio pekee ambayo sitoisahau kwenye kazi yangu hii ya udaktari, maana nilimfanyia mtu ‘operation’ ya goita, na siku 10 hajazinduka, lakini siku ya 11, alikuja juu na kuvuta puumzi”,anasema.

Anakumbuka pia hata ndani ya Kisiwa cha Pemba, tayari alishamfia mwanamke mmoja, kuondoa goita kwenye shingo yake, ingawa baada ya siku mbili tu, aliivuta pumzi na kuwa na hali yake ya kawaida.

Kubwa aliloligundua kwa wanafunzi wa skuli ya Msingi ya Makombeni  pamoja na wananchi wengine wanaofika hospitali ya Mkoa ya Abadalla Mzee Mkoani, anasema jamii ya Pemba, haina utamaduni wa kuchunguuza afya zao.

Anasemna lazima kwa wizara ya afya ya Pemba na Zanzibar ni kuhakikisha, inawapa elimu wananchi juu ya umuhimu wa kuchunguuza afya zao, badala ya kwenda hospitali wakiwa tayari wanaungua.

“Magonjwa mengine ninayoyatibu hospitali, tayari yemeshakomaa, na pengine kama wahusika wengekuwa na utamaduni wa kuchunguuza afya zao, basi kusingekuwa na tatizo kubwa’,anasema.

Hivi karibuni akiwakaribisha madaktari hao, Mganga mkuu wa hospital hiyo Dr.Mwita Haji Mwita, aliwaambia madaktari hao kuhakikisha wanawapa uwelewa wa hali ya juu madaktari wazalendo.

“Dr. Chen na kundi lako, karibuni Zanzibar na karibuni kisiwa cha Pemba, jiskieni huru na muwe nao madaktari wetu wa kizalendo, ili mkiondoka mmeshawapa utaalamu”,aliwaambia.

Hopsitali ya Abdalla Mzee Mkoani Pemba, tayari imeshapandishwa hadhi na sasa kuwa ya Mkoa, baada ya huduma zake kuimarika kwa kuwepo kwa vifaa vya sasa.

Hospitali hiyo, ambayo hivi karibuni ilifanyiwa ukarabati mkubwa na baadhi ya majengo kujengwa upya na serikali ya watu wa China, pia ilipatiwa vifaa vya kisasa kama vya kutibu mfupa bila ya kufanya upasuaji mkubwa.

Dr. Makame Chirau, anauehusika na kitengo hicho kwa upande wa madakatari wazalendo, anasema kwa sasa ule mpango wa kuwekea vyuma au pio pio kwa wanaovunjika, umepungua baada ya kuwa na vifaa vya kisasa.

Vifaa hivyo vya kisasa, vyenye thamani ya shilingi milioni 60, ambavyo kwa Afrika Mashariki vipo kwenye hospitali hiyo pekee, vilitolewa na serikali ya watu wa China miezi minne iliopita.


Dr. Chen Er Dong, aliezwaliwa Disemba, mwaka 1975 kijijni kwao Nan Jing nchini China, ana mke na mtoto mmoja, na kwasasa yeye ni daktari wa masikio, pua na koo akiwa hospitali ya Mkoa wa Abdalla Mzee Mkoani Pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.