Habari za Punde

Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan Afanya Mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bi,Bella Bird.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkaribisha ofisini kwake Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Bi. Bella Bird.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Bi. Bella Bird ambaye alimtembelea Makamu wa Rais ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Bi. Bella Bird mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam.
(Picha na Makamu wa Rais)

Makamu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo amkutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Bi. Bella Bird, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais na Mkurugenzi huyo  walizungumzia masuala mbalimbali ya Lishe kwa akina Mama na namna ukosefu wa lishe bora unavyopelekea vifo vya akina mama na watoto wakati na baada ya kujifungua.

Aidha wamesisitiza suala la Elimu ya Lishe Bora kwa wakina mama hao ili kukabiliana na tatizo.

Makamu wa Rais aliishukuru Benki ya Dunia kwa  kuwasaidia wakina mama wa Kitanzania na kuitaka iendelee kufanya hivyo hasa wakati huu ambapo nchi inaenda kwenye uchumi wa viwanda.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.