Habari za Punde

Balozi Seif Azungumza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Ukimwi (UNAIDS)

Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Ukimwi (UNAIDS) ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ndugu Michel Sidibr

Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi akiagana na waziri wa Oman anayeshughulikia Mafuta na Gesi Dkt Mohammed Bin Hamed. Oman imekubali kuyafanyia ukarabati majengo ya kihistoria ya Beit-Al-Ajab na Palace Museum

Na Mwandishi Wetu OMPR.
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amelipongeza Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia ukimwi kwa misaada yake ambayo imesaidia kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi nchini.

Makamo wa Pili wa Rais ameyasema hayo Afisini kwake Vuga wakati wa mazungumza yake na Mkurugenzi Mtendaji wa Shilika la Umoja wa Mataifa linashughulikia Ukimwi ndugu Michel Sidibr

Amesema misaada ya Shirika hilo la UNAIDS imesaidia kuendesha kampeni mbali mbali ambazo zimejenga ualewa miongoni mwa wananchi kuhusu kuwepo kwa ukimwi nchini.
Hata hivyo balozi Seif ametoa wito kwa viongozi kuendelea kuwahimiza wananchi kujiepusha na vitendo vinavyoambukiza ukimwi pamoja na kuwashajihisha kupima mara kwa mara.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema Zanzibar ni kigezo cha kujivunia kwa nchi nyingi kutokana na mafanikio yake ya kupungunza kwa kiwango kikubwa maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto.

Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema mafanikio ya Zanzibar ya kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto yakiendelezwa hakutokuwa na mtoto anayeambukizwa virusi vya ukimwi katika kipindi kifupi kijacho.

Wakati huo huo Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif amekuwa na mazungumzo na Waziri wa Oman anayeshughulikia Mafuta na Gesi Dkt. Mohammed bin Hamed.

Katika mazungumzo yao Balozi Seif ametoa shukrani zake kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa Oman kwa misaada yake katika miradi mbali mbali ya maendeleo.

Balozi Seif ameiomba Oman kusaidia katika upanuzi wa uwanja wa ndege wa Pemba na kuwa wa kimataifa, ombi ambalo Serikali ya Oman imesema italifikiria.

Balozi Seif amesema uwanja huo utasaidia kukuza biashara ya utalii na viungo kati ya nchi hizo mbili pamoja na kuwauganisha kwa karibu zaidi watu wa Zanzibar na Oman ambao kwa asili ni ndugu.

Kwa upande wake Waziri huyo wa Mafuta na Gesi Dkt Mohammed bin Hamed safari yao ya meli kuja kwa ndugu zao wa Zanzibar kuna lengo la kufungua ukurasa mpya wa mashirikiano kati ya pande hizo mbili.

Amesema kuna mambo mengi ya kuwaunganisha watu wa pande hizo mbili kuliko mambo ya kuwatenganisha.

Kuhusu ombi la Zanzibar la kukarabati kumbusho la Beit-al-ajab na kumbusho la Palace, Serikali ya Oman imesema iko tayari kuyafanyia matengenezo makubwa majengo hayo kwani ni rasilimali ya ulimwengu mzima.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.