Na. Haji Nassor - Pemba.
KAMATI ya Ushawishi na Utetezi kutoka
Jumuia ya mtandao wa wakulima wa matunda na mboga mboga Kisiwani Pemba JUMWAMPE,
imesema imegundua changamoto kadhaa zinawazowakabili wakulima wao, ikiwa ni
pamoja na kukosa elimu ya matumizi sahihi ya pembejeo za kilimo.
Kamati hiyo,
ilipita kwa wakulima zaidi ya 100 kisiwani humo, na baada ya kuwajazisha dodoso
maalum, waligundua kuwa wakulima hao, hawana elimu ya matumizi ya dawa za mimea,
hali inayotishia usalama wao na walaji.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi mjini Chakechake mara baada ya kumalizika kwa
safari ya kuwatembelea wakulima, Katibu wa Jumuia Mtandao huo Hamad Ali Mussa,
alisema wapo waliowagundua kutumia dawa ya kuulia kunguni kwa kutumia kwenye
mazao.
Alisema
jengine waliloligua wakati wakiwa na wakulima hao, ni kutokuwa na kipimo sahihi
cha kunyunyizia dawa hizo, kwenye mboga mboga zao, ambpo hupelekea muda mfupi
baada ya kutia dawa kuvunwa na kuuzwa sokoni.
Katibu huyo
alieleza kuwa, hilo pia linaweza kusababisha athari ya kimwili kwao, walaji na
hata wanyama wanaowapa malisho, baada ya kumalizika kwa uvunaji.
“Huu
tuliofanya sio utafiti hasa, ni kama tumewatembelea na kuonana nao, lakini
utafiti hasa tutaufanya baadae, ili kugundua changamoto hasa zinazowakabili
wakulima wetu na wafugaji, maana wao ndio tegemeo letu kwa ajili ya
chakula”,alifafanua.
Makamu
Mwenyekiti wa Jumuia hiyo Mtandao, Zainab Rajab Iddi, alisema kwenye msafara
wao huo, piwa wamegundua baadhi ya wakulima hao, kutokuwa na uhakika wa
matumizi ya maji, kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao.
Alieleza
kuwa, wapo wanaolalamiki bili kubwa ya maji au kukatiwa maji na ZAWA, jambo
ambalo wamesema linawarejesha nyuma, katika sekta hiyo walioichagua.
“Wapo
waliolalamikia kuwa hukatiwa maji na ZAWA hata kama ndio kwanza mazao au mboga
mboga zao hazijapevuka, hali ambayo huwakosesha mwendo wa kufikia maendeleo
yao”,alieleza.
Kwa upande
wake mjumbe wa kamati hiyo ya ushawishi na utetezi kutoka ‘JUMWAMPE’ Saada
Hamad Kombo, alisema ambalo jengine
walioligundua na kuamua kuitafuta sera ya kilimo, ni kuwepo kwa maduka ya wauza
pembejeo bila ya mpangilio, hali inayosababisha na wakulima nao kununua
wapendavyo.
Aliongeza
kuwa, hilo linawapa shida wakulima, kwanza kununua dawa wasizozijua matumizia
yake sahihi wala vipimo vyake, maana muuza pembejeo yeye anachotaka ni biashara
yake iende tu, na sio kuangalia usalama wa anaemuuzia”,alifafanua.
Kufuatia
safari hiyo ya kuwatembelea wakulima, Mjumbe mwengine wa Kamati hiyo, Hassan
Shamis Hassan, alisema sasa wanachotarajia kukifanya, ni kuipitia kwa umakini sera
ya kilimo, ili kuona inasemaje hasa kwa uingiaji, uuzaji na utumiaji wa
pembejeo zenye kimikali.
“Ingawa pia
tulishakwenda ZAWA na kupendekeza tuwe na mikatab, au wizara ya biashara na viwanda
kuahidi kuzitangaaza biashara za wakulima wetu, lakini pia lazima serikali
iangalie uwezekano wa kutupia macho biashara ya pembejeo”,alieleza.
Aidha kamati
hiyo, imeshauri kuwepo kwa umakini mkubwa wa uingiaji wa pembejeo kisiwani
Pemba, aina ya mbegu za matunda na mboga mboga, sambamba na kuwajengea uwezo
mabibi na mabwana shamba, ili wakulima wapate utaalamu na ushauri wao wakati
wote”,alifafanua.
Mkulima wa
mboga mboga shehia ya Vitongoji wilaya ya Chakechake Mkubwa Ali Mkubwa, alisema
kwake yeye kubwa analoliona linamrejesha nyuma ni ukosefu wa soko la uhakika.
Nae mkulima
wa vitango, mchicha na tungule wa Vitongoji Mohamed Khamis Song, alisema hivi
karibuni alikuwa na vitango 700 ambavyo alikosa soko la uhakika na kuviuza
chini ya bei.
“Kitango kimoja
nililazilimika kukiuza kwa bei ya shilingi ya 150 na shilingi 200, maana
tulikosa soko la uhakika, sasa lazima serikali ituangalie sasa tumeshatekeleza
agizo la kujikusanya pamoja”,alifafanua.
Jumuia
Mtandao wa wakulima wa mboga mboga na matunda kisiwani Pemba ‘JUMWAMPE’ ambayo
iliasisi tokea mwaka 2008 kwa kuanza mkoa wa kaskazini Pemba pekee, na sasa
kuwa ya Pemba nzima, inadhamira ya kuwawezesha wakulima hao, ili wazalishe
bidhaa zenye ubora na zinazokubalika sokoni.
No comments:
Post a Comment