Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar balozi Seif Ali Iddi akizungumza na uongozi wa jumuiya ya walimu wa madrasa wanaopiga vita vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia Zanzibar afisini kwake Vuga
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Balozi wa Saudi Arabia Mohammed Al Malik, alipofika Ofisini kwake kwa Vuga kwa mazungumzo leo
Na.Mwandishi wa OMPR
Makamo wa pili wa Rais wa
Zanzibar balozi Seif Ali Iddi amezitaka Jumuiya zisizo za kiserikali (NGO)
nchini kufanya kazi ambazo wameruhusiwa kwa mujibu wa katiba zao.
Makamo wa pili wa rais
ameyasema hayo afisini kwake Vuga alipokuwa akizungumza na uongozi wa Jumuiya
ya walimu wa madrasa wanaopinga vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia.
Amesema zipo baadhi ya
Jumuiya zimeazishwa kwa malengo ya kijamii lakini baada ya muda mfupi jumuiya
hizo hujiingiza kwenye siasa na kuacha kazi zao za msingi.
Balozi Seif ametoa onyo kwa
jumuiya hizo kuacha tabia hiyo mara moja vyenginevyo Serikali itazifuta mara
moja.
Akizungumza kuhusu
udhalilishaji wa kijinsia nchini Balozi Seif amewapongeza wanajumuiya walimu wa
madrasa wanaopinga vitendo vya udhalilishaji kwa uamuzi wao wa kuunga mkono juhudi
za Serikali za kupambana na vitendo vya ubakaji nchini.
Amesema ametiwa moyo wa
walimu hao wa madrasa kwa kuwa mstari wa mbele kupambana na ubakaji unaofanywa
na baadhi ya wenzao hapa nchini.
Balozi Seif amesema juhudi
hizo za walimu wa madrasa za kupambana na ubakaji nchini zinawatia moyo wazazi
na kuwaomba wanajumuiya kujenga umoja miongoni mwao katika kupambana na
udhalilishaji.
Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya walimu wa madrasa wanaopinga
vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia mwalimu Shabaan Rashid Ndondole amesema
Jumuiya yao imeundwa baaada ya kuona baadhi ya walimu wa madrasa wanaipaka
matope kwa vitendo vyao vibaya kada hiyo ya ualimu wa madrasa.
Mwalimu Shaaban imeiomba
Serikali na wahisani mbali mbali
kuisaidia Jumuiya hiyo kwa kuipatia vifaa vya afisini pamoja na usafiri
kwani lengo lao ni kupambana na ubakaji nchi nzima.
Wakati huo huo Makamo wa
Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi amekutana na Balozi wa Saudi Arabia Balozi
Mohammed Almalik aliyekuja kuwasilisha ujumbe wa Serikali yake.
Katika mazungumzo yao
Balozi Seif ameipongeza Serikali ya Saudia kwa misaada yake ambayo inasaidia
kusukuma mbele maendeleo ya kiuchumi ya Zanzibar.
Viongozi hao wawili pia
wamezungumzia suala la kuimarisha utaratibu wa kwenda Hija kwa mwakani na
kukubaliana suala hilo kulifanyia kazi zaidi.
No comments:
Post a Comment