Na:
Genofeva Matemu – WHUSM
Tarehe:
14/10/2017
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewataka watanzania
wote kuishi maisha aliyoishi Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere
kwa kuacha kuwa wabinafsi na kufanya kazi kwa maslahi ya watanzania wote.
Hayo ameyasema leo
wakati wa sherehe za kilele cha mbio za mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa
Taifa na wiki ya vijana kitaifa iliyoazimishwa katika uwanja wa Amaan Mkoani
Mjini Magharibi Zanzibari.
“Watanzania
wanatakiwa kujenga taifa kwa vitendo vinavyodumisha amani, upendo na mshikamano
kama ambavyo Mwl. Nyerere alipambana kujenga taifa lenye uhuru wa kweli
linalojitegemea na lenye watu wanaojali na kuheshimu utu wa kila mmoja”.
Akizungumzia Mwenge
wa Uhuru Mhe. Magufuli amesema kuwa
mwenge wa uhuru ni alama ya uhuru na utaifa wetu ambao umekua ukiimarisha
muungano wetu kwa kuwaunganisha watanzania na kuchochea maendeleo kwa kujenga na kuimarisha uchumi wa nchi kwa
kuzindua miradi mbalimbali ya kimaendeleo ambayo dhana yake ni kukuza utu na
ustadi wa watanzania.
Kwa upande wake
Kiongozio wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2017 Bw. Amour Hamad Amour amesema
kuwa Mbio za mwenge wa uhuru mwaka huu zimefanya kazi kubwa ya kuwakumbusha
watanzania kuimarisha mshikamano, kujenga umoja wa kitaifa na kuhamasisha
ukamilishaji miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kuhakisi dira ya mwelekeo wa
seriakali ya awamu ya tano kwa kusisitiza uwekezaji katika viwanda ili Tanzania
iweze kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025
Naye Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira, na wenye ulemavu Mhe
Jenista Mhagama amesema kuwa watanzania wote na hasa vijana hawana budi kulinda
urithi wa mwenge wa uhuru kwani ni muhimu kwa mstakabali wa nchi ya Tanzania
Mhe. Jenista amesema
kuwa mbio za mwenge wa uhuru siku zote zimekua ni kichocheo cha maendeleo ya
wananchi katika kuwahamasisha, kubuni, kuandaa na kutekeleza miradi mbalimbali
ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi huku mwenge huo ukitumika kufichua na
kupambana na maaduni wa maendeleo hususani adui rushwa, ufisadi, ubadhirifu wa
rasilimali za umma, mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi, malaria na matumizi
ya dawa za kulevya hadi hapo maadui hawa watakapotokomezwa katika nchi ya
Tanzania.
Mwenge wa uhuru
uliohasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka
1964 ni tunu na alama ya uhuru na utaifa wetu, huleta amani, mshikamano,
uzalendo na umoja wa taifa letu la Tanzania
No comments:
Post a Comment