Habari za Punde

Sailors yachapwa na Chuoni, Leo ni Daraja la kwanza katia ya Mlandege na Kizimkazi



Na: Abubakar Khatib “Kisandu”, Zanzibar.

Mzunguko wa kwanza wa Ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja umekamilika jioni ya leo kwa kupigwa mchezo mmoja katika uwanja wa Amaan ambapo Maostadh wa Chuoni wakaichapa Black Sailors bao 1-0.

Bao pekee la Chuoni limefungwa na Hafidh Juma Haji dakika ya 50 ya mchezo.

Baada ya kuchezwa mzunguko mmoja kwa kila timu kwenye ligi kuu soka ya Zanzibar Kanda ya Unguja sasa ligi hiyo itakwenda mapumziko hadi Oktoba 15 kuendelea tena mzunguko wa pili.

Ratiba ya mzunguko wa Pili kama zifuatazo ambapo michezo yote itapigwa katika uwanja wa Amaan.

Jumapili 15/10/2017 saa 8:00 za mchana JKU vs Chuoni
Jumapili 15/10/2017 saa 10:00 za jioni Miembeni City vs Mafunzo

Jumatatu 16/10/2017 saa 8:00 za mchana Taifa ya Jang’ombe vs Polisi
Jumatatu 16/10/2017 saa 10:00 za jioni KVZ vs Zimamoto

Jumanne 17/10/2017 saa 8:00 za mchana Kipanga vs Charawe
Jumanne 17/10/2017 saa 10:00 za jioni KMKM vs Kilimani City

Jumatano 18/10/2017 saa 10:00 za jioni Black Sailors vs Jang’ombe Boys

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.