STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar
03.11.2017
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameipongeza Ofisi ya Rais,
Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora na kueleza azma ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi ili kuutekeleza
Utawala Bora kwa vitendo.
Dk. Shein aliyasema hayo leo, Ikulu mjini Zanzibar
alipokutana na uongozi wa Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala
Bora ilipowasilisha utekelezaji wa Mpango
Kazi wake kwa Mwaka 2016/2017, Mpango
Kazi wa Utekelezaji kwa mwaka 2017/2018 na Utekelezaji wake kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Julai hadi
Septemba, 2017.
Alieleza kuwa furaha yake kwa kuonesha mafanikio makubwa
yaliopatikana katika utendaji wa kazi uliowasilishwa na Ofisi hiyo na kueleza
kuwa Ofisi hiyo ambayo inashugulikia Katiba, Sheria na Utawala Bora ina
changamoto nyingi lakini hata hivyo ni vyema zikapatiwa ufumbuzi.
Aliongeza kuwa mbali ya kuwa na Utawala Bora
lakini lengo la Serikali ni kutoa huduma bora na zenye kiwango kizuri ili
wananchi wasinungunike na kuitaka Ofisi hiyo kuendelea kufanya vizuri zaidi
katika kuwatumikia wananchi na kuwapa huduma zilizo bora.
Alileza kuwa katika nchi za Afrika Zanzibar ni
miongoni mwa nchi za mwanzo zilizoanzisha Wizara ya Utawala Bora ambapo kwa
hivi sasa Wizara hiyo imepata mafanikio makubwa sana hivyo, ni vyema
ikaimarisha ubora na weledi wake.
Dk. Shein aliueleza uongozi huo kuwa pale wanaposikia
malalamiko ya wananchi ni vyema wakayafanyia kazi na kuitaka Ofisi hiyo kuwasikiliza
wananchi mawazo yao kwani ni njia moja wapo ya kufuata Utawala Bora.
Pia, alisisitiza suala zima la uwajibikaji
sambamba na kuimarisha na kuendeleza ushirikiano na umoja miongoni mwa viongozi
hao na watendaji wa Ofisi hiyo na kuitaka kuendelea kufanya kazi kwa kasi ili
tija iweze kupatikana.
Nae Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif
Ali Idd aliipongeza Ofisi hiyo kwa mafaniko iliyoyapata huku akisisitiza haja
ya kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya suala zima la kupambana na vitendo
vya rushwa na uhujumu wa uchumi.
Nae Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee aliupongeza uongozi wa Ofisi hiyo kwa
uwasilishaji mzuri wa Mpangokazi wake na kusifu mashirikiano mazuri anayoyapata
kutoka Wizara hiyo ambayo yanamsaida katika utendaji wake wa kazi.
Waziri wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Katiba,
Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman alitoa shukurani
kwa Dk. Shein kwa uongozi wake thabiti na shupavu unaowafanya wasaidizi
aliowateua kwa imani kubwa kusimamia na kutekeleza majukumu yao kwa mujibu na
sheria na taratibu zilizopo.
Alieleza kuwa utaratibu aliouanzisha wa
Bangokitita ambao huwakutanisha na watendaji wakuu wa Wizara mbali mbali ni
mzuri na unastahiki kupigiwa mfano kwa sababu unajenga kivitendo misingi ya Utawala
Bora ambayo inahimiza masuala mazima ya uwazi na uwajibikaji.
Aidha, Waziri Haroun alisema kuwa Mfumo wa kisasa wa usimamizi wa kesi kwa njia
ya kielektroniki umewekwa katika Mahkama Kuu Vuga kwa maajiribio na utawekwa
katika Mahkama nyengine zote Unguja na Pemba kufikia mwaka 2020.
Katika kusimamia maadili yaa viongozi Waziri
Haroun alaileza kuwa katika kusimamia maadili ya viongozi wa Umma elimu imetolewa
kwa viongozi wa Umma kuhusu umuhimu wa maadili ya viongozi wa Umma, sheria ya
Maadili ya Umma na utaratibu wa kujaza fomu za tamko la mali na madeni.
Aliongeza kuwa katika kuzuia vitendo vya
rushwa na uhujumu wa uchumi mikutano
iliyolenga kukuza uelewa wa jamii kuhusu majukumu ya Mamlaka na umuhimu wa
kuepuka vitendo vya rushwa ilifanyika kwa taasisi za Serikali Unguja na Pemba.
Nao uongozi huo ulipongeza hatua hizo za Rais za
kukutana na viongozi na kujadili Mipangokazi ya Mawizara na kueleza kuwa mfumo
huo umeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa na kupelekea baadhi ya nchi jirani
kuufuatilia na kuanza kuuiga mfumo huo ambao Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
umeuanza kwa miaka sita hivi sasa.
Wakati huo
huo, Dk.
Shein alikutana na uongozi wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ambapo Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed alimpongeza Rais
Dk. Shein kwa namna anavyoiongoza Zanzibar ambapo kila mmoja anashuhudia
mageuzi makubwa ya utendaji wa kazi kwa watumishi hasa katika sekta ya umma.
Aliongeza kuwa mageuzi hayo yamechochea kwa kiasi
kikubwa maendeleo ya nchi katika sekta zote ambapo wasaidizi wake wote
wanazingatia sana miongozo na maelekezo yake katika kutekeleza majukumu yao ya
kusimamia shughuli za Srrikali katika maeneo yao.
Nae Rais Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuipongeza
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais kwa mafanikio iliyoyapata pamoja na kuwasilisha
vyema Mpangokazi wake.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment