STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 07.12.2017
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amewaapisha Wakuu wa Mikoa wapya pamoja na Naibu Katibu Mkuu,
Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto (anaeshughulikia
masuala ya Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto),viongozi ambao aliwateua hivi
karibuni kushika nyadhifa hizo.
Viongozi walioapishwa hivi
leo katika ukumbi wa Ikulu mjini Zanzibar ni Hassan Khatib Hassan kuwa Mkuu wa
Mkoa wa Kusini Unguja, Hemed Suleiman Abdalla kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba
na Mwanajuma Majid Abdalla kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Kazi, Uwezeshaji,
Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto (anaeshughulikia masuala ya Wazee, Vijana,
Wanawake na Watoto).
Miongoni mwa viongozi
waliohudhuria hafla hiyo ni Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali
Maulid, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said, Mawaziri na Manaibu
Waziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na
Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee.
Wengine ni Mufti Mkuu
wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji,
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub
Mohamed Mahmoud, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib,
Washauri wa Rais wa Zanzibar, Wakuu wa Vikosi vya SMZ, pamoja na viongozi
wengine wa Serikali.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment