VIONGOZI wa Jumuiya ya Sanaa Elimu ya Ukimwi na Mazingira Kisiwa Pemba, wakiwawaonyesha waandishi wa habari eneo ambalo liko wazi na wanakusudia kulipanda miti ya mikoko 400,000 ili kurudisha asili ya eneo hilo(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
BAADHI ya wananchi wa Kisiwa Panza wakipanda miti ya mikoko katika maeneo ya wazi, yaliyoathiriwa kufuatia ukataji wa miti na kupelekea kuwa jangwa.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MITI ya mikandaa au Mikoko ikiwa imenawiri vizuri, katika moja ya maeneo yaliyomo ndani ya kisiwa Panza, miti hiyo imepandwa kwa nguvu za wananchi kwa lengo la kukinusuru kisiwa chao(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.
PEMBA ni miongoni mwa visiwa vilivyozungukwa na bahari,
nacho kikiwa kimezungukwa na visiwa vidogo vidogo vikiwemo Fundo, Njau, Funzi,
Panzi, Misali, Makoongwe, Kisiwa Panza na Kojani.
Kwa
mujibu wa Matokeo ya Sensa ya watu na makaazi Tanzania 2012, Zanzibar inaidadi
ya watu 1,303,568, Unguja ina watu 896,720, Kisiwa cha Pemba kina Wakaazi 406,848 na eneo lenye ukubwa wa 980KM2, katika ramani ya dunia,
pemba ipo baina ya Latitudo 40 80’na 50 30’ s, Longitudo
3900 35’ na 3900 50’E, pia ina urefu wa Mail 40 kutoka
kaskazini hadi kusini.
Suala
la uharibifu wa mazingira, juu ya ukataji wa miti ya mikandaa
na miti ya juu, kwa shuhuli za ujenzi, kuni na upigaji wa tanu ya mkaa, zimeshababisha
maji ya bahari kupanda katika mashamba.
Uharibufu
wa mazingira kwa kiasi kikubwa ndio unaosababisha mabadiliko ya tabianchi, Kisiwa
Panza kipo Chokochoko Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba, kikiwa kwa kiasi
kikubwa kimeathirika kutokana na ukataji wa miti.
Mwaka
1994 makaburi yanayosadikiwa kuwepo tokea mwaka 1880 Yalifukuka
na kupatikana kwa mabaki yake, baada ya kunyesha mvua kubwa na maji ya bahari
kupanda juu. Hali hii ilitokea baada ya wananchi kujisahau na kukata miti bila
ya mpangilio na maji ya bahari kuvamia maeneo ya kilimo.
Mwandishi
wa makala hii alilazimika kufunga safari ya saa moja na nusu, kwa kutumia
usafiri wa daladala ya abira kutoka Chake Chake hadi ChokoCho, baada ya kufika
chokocho likoni ndipo muda wa dakika 5 zikatumika kwa usafiri wa mashua kwenda
Kisiwa Panza.
“Ufahamu
wangu mimi baba yangu alikuwa analima eneo hili, sahivi tizama mwandishi………….
Wewe si umekuja kuona tulivyoathirika na ukataji wa miti……………hata ufanye nini
hapawi kitu hapa”
Mwajuma
Ali Hassan (22) anasema suala la ukataji wa miti limewaathiri sana wakulima, kwani
kwa sasa mazao kutoka mashambani yamepungua kutokana na mashamba hayo kujaa
maji ya bahari.
“Mashamba
yamegeuka majangwa baada ya kuingia maji chumvi, kufuatia
wananchi kukata miti bila ya kikomo na kusahau kuwa kisiwa
kimezungukwa na bahari,” ameleza Mwajuma.
Ukataji
wa miti ovyo umepelekea maisha ya wananchi kuwa rehani, baada
ya eneo lenye ukubwa wa hekta 200 kuingiwa na maji chumvi.
Ndani
ya eneo hilo kuna mashamba, skuli na makaazi ya watu na vyote vimeathirika
kutokana na mabadiliko ya tabianchi.
Naye
Abdalla Khalfan Khamis (59), ananeleza kuwa kisiwa kilikuwa na miti yakutosha,
ardhi iliyojaa rutba na kinachopandwa kinatia, sasa mambo yamekuwa kombo.
“Ukataji
na uvunaji wa miti umekuwa mkubwa, miti mikubwa mikubwa imeteketea
kwa wingi, upandaji wake umekuwa mdogo kutokana na wananchi
kutokuwa tayari kukinusuru kisiwa chao,” anasema Khamis.
Takriban
yapata miaka 20 tokea maji ya bahari kuvamia mashamba ya kilimo, kusababisha
wananchi kukosa sehemu za kulima na hivyo kuingia katika shughuli za uvuvi wa kaure, ukulima wa mwani na uvuvi wa Pweza.
Tashdidi
Zubeir (75) ambaye kwa asili alikuwa mkulima, anaeleza kuwa chumvi kuvamia
maeno ya kilimo, kumesababisha wakulima kuhama katika mashamba yao na kuingia
katika shuhuli nyengine za kujitafutia kipato.
“Wakulima
walikuwa wanapata mazao mengi, ya aina
mbali mbali, lakini kwasasa hali imekuwa tofauti kutokana na ukataji wa miti, hakuna
tena kinachopatikana, ndiyo maana watu wengi wameamua kujishughulisha na
uvuvi,” anasema mzee Zuberi.
Anaelezakuwa
umaskini umechangia kwa kiasi kikubwa, kwa wananchi kuharibu Mazingira, “Vijana
wanakata miti ovyo, wanapiga tanu za chokaa, wanakata kuni na miti ya kujengea
kwa madai kuwa wamekosa ajira.”
“Wasiwasi
wangu uko katika daraja lililotenganisha Ndooni na Panza,
mwandamo wa mwezi maji hufunika daraja na kuzuwia wananchi kupita kwa
muda,”alisema.
Wanafunzi
nao hawakuwa nyuma kuzungumzia athari ya ukataji wa miti katika kisiwa hicho, Abdullhalim
Abdalla Abdalla (20) ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika skuli ya Sekondari
Kisiwa Panza, anasema athari kubwa imetokeakwa
kuwa maeneo mengi yameingi maji ya bahari, ikiwemo maeneo ya skuli.
“Tulichukua
juhudu ya kupanda miti 2,000, katika maeneo ya skuli ikiwemo mikoko, Zamani
maji yalikuwa mbali lakini sasa hivi yameanza kuingia katika eneo la skuli,
Ingawa serikali imejenga ukuta kwa saruji bado maji yamebuni sehemu nyengine
yakuingia”alisema.
Mwanafunzi
mwingine, Amina Hamad Makame (17), anaeleza kuwa mabadiliko ya tabia nchi
yameathiri sana sehemu za skuli, kwani wakati wa bamvua kubwa
wanafunzi hushindwa hata kupita darajani kwa ajili ya kwenda skuli.
“Ni
vema wananchi waache tabia ya ukataji
miti ovyo, ili kunusuru kisiwa chetu, watoto wanaokuja nao waweze kuona matunda
na sio kuwatupia lawama wazazi wao.”
Mwalimu
wa mazingira katika skuli ya Kisiwa Panza Msingi, Salti Salim Abdalla (32)
amesema inafika miaka mitatu wakuliama wanakosa sehemu za kulima, ameshauri
jamii kupanda miti kwa wingi
karibu na eneo la skuli, ili kupunguza athari za kimazingira zinazotokana na
mabadiliko ya tabia nchi.
“Sisi
tuliweza kupanda miti ya mikoko 3000, mivinje na mikungu, Miti hii imesaidia
kupunguza kasi ya maji kupanda juu katika
eneo la skuli,”alisema.
“Miaka
10 iliyopita maji yalikuwa umbali wa kati ya mita 150 na 170 kufika eneo la
skuli, sasa yapo mita 100, Shughuli za kilimo zimeathiriwa kwa kiasi kikubwa na
maji chumvi,” aliongeza.
Akizungumzia
athari za mabadiliko ya tabianchi, Shekh Faki Makame Faki(56) ambaye ni imamu
wa msiki katika kisiwa Panza, anansema Kisiwa Panza kimeathirika kutokana na ukataji
wa miti.
Kuongezeka
kwa maji kumepelekea makaburi kufufuka, ikiwa ni athari nyingine ya mabadiliko
ya tabianchi, athari nyingine iko upande wa kilimo, ambako hakuna mazao
yanayostawi kwani kila kinachopandwa hakioti, baada ya maji ya chumvi kuingia
katika mashamba.
“Uharibifu
wa mazingira hasa ukataji ovyo wa miti ni tatizo lililokifikisha
kisiwa kilipo, Mafuvu ya maiti yanafukuka katika makaburi
na saivi eneo hilo limekuwa jangwa tu,”
anaeleza.
Sheikh
Faki ameongeza kuwa wakati umefika wa kutumia mazingira kwa umakini na kwa
namna endelevu, ili kuwafaa na vizazi vijavyo.
Mratib
wa Jumuiko la Mabadiliko ya Tabianchi Zanzibar (ZACCA), Habiba Juma
anasema suala la uhifadhi wa mazingira ni jukumu la kila
mtu na sio taasisi moja tu, amewataka wananchi kuendelea kupanda
miti kwa wingi, ili kuzuwia maji ya bahari kuvamia maeneo ya kilimo.
“Kisiwa
cha Pemba kina maeneo mengi ambayo yameathiriwa na uharibifu wa mazingira, Kasi
ya kukata miti kwa wingi ni kubwa kuliko juhudi za wananchi kupanada miti
mingine,” anaeleza mratib wa ZACCA.
Katika
kukabiliana na hali ya uharibifu wa mazingira, ZACCA kwa kushirikiana
na wananchi wamepanda miti ya mikandaa 25,565 katika
maeneo ya Wambaa, Tumbe na Mgelema.
Katibu
wa Jumuiya ya Sanaa Elimu ya Ukimwi na Mazingira, (JSEUMA) Pemba, Juma Ali
Mati, anasema mwaka 2015 walielimisha wananchi 200 juu ya suala la mabadiliko
ya tabianchi, juu ya ukataji wa Kuni, upigaji wa tanu za chokaa na mkaa,
waliopata mafunzo hayo walitoka kijiji cha Kangani, Chokocho, Makoongwe, Kuku
na Mwambe.
Katika kipindi hicho
miti 6,550 ya mikoko imepandwa kwa hatua ya Kwanza, Katika awamu
ya pili miti 6,800 ilipandwa katika kisiwa cha Matumbilini na ufunguni,
Mwaka 2016 miti ya juu 22,000 na miti mingine
4,000 imepandwa kisiwa cha matumbilini.
“Miti 16,000
ilipandwa kisiwa cha Ufunguni, ambapo miti mingi eneo hilo jamii wanaitumia
vibaya, huku miti 100,000 imepandwa katika maeneo tafauti ya kisiwa Panza,”
aliongeza katibu huyo.
Mwaka 2017 mradi wa LDCF
umeweza kupanda miti 400,000, baada ya uhamasishaji walipanda 650,000 katika
eneo la Mto wa Kae, Madauni, Ufunguni na
Bandarini Juu, huku wakitarajiaa kupanda miti ya juu 300,235,
kabala yam mwaka huu kumalizika.
“Lengo letu ni kudhibiti athari zisiendele kuharibu
kisiwa chetu, Mradi umejenga kuta mbili kubwa katika eneo lililokuwa linaingia
maji chumvi, ambapo kwa miaka 12 mashamba hayo yanayolimwa na kaya 50
hayatumiki kwa kilimo,”alisema Mati.
Naye Mkurugenzi wa
Idara ya Misitu na Mali Zisizorejesheka Zanzibar, Soud Juma Mohamed, alisema kitu cha msingi katika
kudhibiti maji chumvi ni kupanda miti ya mikandaa katika maeno ya baharini, ilikuzuwia
kasi ya maji kuingia mashambani.
Kwa upande wake mkuu
wa idara ya misitu na mali zisizorejesheka Pemba, Said Juma Ali, anasema ni
miaka 10 sasa wamejikita katika upandaji wa miti ya mikandaa na miti mengine,
ikiwemo kuanzisha misitu ya jamii kwa lengo la kuhifadhi mazingira.
“Athari za mabadiliko
ya tabianchi katika Kisiwa Panza ni kubwa, Eneo kubwa lilikuwa na misitu ya
mikandaa ambayo ilikuwa inapunguza nguvu ya maji kuja juu, Miti mikubwa
iliyokuwa na nguvu imekatwa, nguvu ya maji kuja juu imeongezeka, hususan upande
wa kusini kwenye bahari kuu,”alisema.
Kukatwa kwa miti
kumepeleka athari kubwa katika upatikanaji wa maji safi na salama, kwani visima
vya jamii vimekauka na pia kilimo cha mihogo
kimeathirika kutokana na hali hiyo.
Mkuu wa Idara ya
mazingira Pemba, Mwalim Khamis Mwalimu, alisema jumla ya Mikoko
412,436 imepandwa na lengo ni kupanda miti 400,000 katika Kisiwa Panza, Maeneo
123 yamevamiwa na maji chumvi katika Kisiwa Panza, ambayo ni sawa na hekta 200, Matarajio ni
kupanda miti ya juu 2000.
Mtaalamu wa uhifadhi
wa miti ya mikandaa Pemba, Salum Khamis Haji, anasema kuwa
Kisiwa Panza kinavamiwa na watu kutoka maeneo mbali mbali ikiwemo, Nungwi na
Mkokotoni ambao wanakata miti ya kujengea kutoka kisiwani hapo.
Katika jitihada za
kuhakikisha kisiwa kinaendelea kuwepo, wastaniwa miti 335,000 imepandwa katika
hekta 67 hadi sasa, “Suala la upandaji
miti na uhifadhi wa mazingira ni jukumu letu sote, hivyo mikakati
madhubuti inahitajika kuhakikisha kisiwa cha Pemba, kinaendelea kuwepo katika
ramani ya dunia kwa kupanda miti kabla ya kukata mti.”
MWANDISHI WA MAKALA HAYA ANAPATIKANA
KWA EMAIL:abdisuleiman33@gmail.com
SIMU:+255718968355.
No comments:
Post a Comment