Habari za Punde

Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ya baraza la wawakilishi yakutana na wazazi na walezi wa watoto walioanguka katika mikarafuu

 AFISA Mdhamini Wizara ya Biashara Viwanda na Masoko Pemba, Abdalla Juma Khamis akizungumza katika kikao cha wajumbe wa Kamati ya Fedha, biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar na wananchi walioanguka mikarafuu msimu uliopita. .(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
 WAZAZI na walezi wa watoto walioanguka mikarafuu katika msimu uliopita, wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ya baraza la wawakilishi Zanzibar, katika kikao maalumu kilicho fanyika Makonyo Chake chake Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
  MJUMBE wa kamati ya Fedha Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, ambae pia ni mwakilishi wa jimbo la mkwajuni Ussi Yahya Haji, akichangia manda katika kikao na wakulima wa karafuu walioanguka mikarafuuni mwaka jana.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
MWENYEKITI wa Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ya Baraza la wawakilishi Zanzibar, Yussuf Hassan Iddi akizungumza na waathiria wa zoezi la uchumaji wa karafuu Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
 MWAKILISHI wa Jimbo la Mkwajuni na Mjumbe wa kamati ya fedha, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe:Ussi yahaya Haji, akiangalia moja ya madagaa yalioyohifadhi na wajasiriamali wa biashara hiyo huko Ndagoni Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
MWENYEKITI wa kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ya baraza la Wawakilishi na Mwakilishi wa jimbo la Fuoni, Mhe:Yussuf Hassan Iddi, akizungumza na wanaushirika wa biashara ya kukausha dangaa ndagoni Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.