Na Said Abrahaman,
Pemba.
JESHI la Polisi Mkoa
wa Kaskazini Pemba, limesema kuwa litadumisha amani na utulivu katika kipindi
hichi sikukuu ya Pasaka.
Akizungumza na Gazeti
hili Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Haji Khamis Haji, alisema kuwa
jeshi hilo limejipanga vizuri ili kuhakikisha amani iliyopo inadumishwa.
Alieleza wamedhamiria
kufanya doria za miguu pamoja na kutumia gari katika maeneo mbali mbali ambayo
yatatumika kwa sherehe hizo.
"Tumepanga
kufanya doria katika maeneo yote, ambayo yatakuwa yakitumika kwa sherehe hizo
hasa katika nyumba za ibada pamoja na fukwe,",alifahamisha Kamanda.
Mbali na hayo lakini
pia Kamanda huyo alisisitiza kuweka askari wake barabarani ili kulinda usalama
wa barabarani.
Hata hivyo kamanda
huyo aliwataka wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi hilo ili liweze
kufanya kazi zake inavyotakiwa.
Wakati huo huo Jeshi
hilo linamshikilia kijana, Mohammed Salim Suleiman mkaazi wa Pandani Wete kwa
tuhuma za kupatikana ng'ombe anasadikiwa ni wa wizi.
Kamanda Haji, alithibitisha hilo na kusema kuwa mtuhumiwa huyo alipatikana na tuhuma hizo usiku wa kuamkia leo huko Pandani.
Kamanda Haji, alithibitisha hilo na kusema kuwa mtuhumiwa huyo alipatikana na tuhuma hizo usiku wa kuamkia leo huko Pandani.
"Ni kweli kuna
kijana mmoja kwa jina anaitwa Mohammed Salim Suleiman wa Pandani alikamatwa
akiwa na ng'ombe watatu wa wizi"alifahamisha Kamanda.
Hata hivyo alisema
kuwa kwa sasa mtuhumiwa huyo yuko chini ya ulinzi na upelelezi unaendelea.
No comments:
Post a Comment