Habari za Punde

Best of Zanzibar yazindua kampeni yake ya Valisha Mtoto Viatu Mbuyu tende na Kijini Wilaya ya Kaskazini A Unguja

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Zanzibar. Mhe. Vuai Mwinyi, akizinduz Kampeni ya Uvaaji wa Viatu kwa Watoto wa Vijiji vya Kijini na Mbuyu Tende Mkoa wa Kaskazini Unguja, akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Pennyroyal Zanzibar Limited Mr. Saleh Mohammed Said, uzinduzi huo umefanyika katika Viwanja vya Skuli ya Sekondari ya Kijini Matemwe Mkoa wa Kuskazini Unguja.


Best of Zanzibar yazindua kampeni yake ya Valisha Mtoto Viatu (Pair for Every Child Campaign) katika shule za Mbuyu Tende na Kijini wilaya Kasikazini A Unguja. Watoto wa vijiji hivi wana tembea muda mrefu shuleni bila viatu na wengi wao hutembea zaidi ya kilomita 5 kwenye ardhi kavu ya mawe iwe masika au kiangazi.

Kutokana na hali hiyo watoto wengi wanaweza kupata maradhi wakati wanakwenda chooni ama kukanyaga vitu vya hatari vinavyoweza kuwadhuru.

“Best of Zanzibar imeshafanya elimu ya afya na usafi wa mwili na mazingira, elimu hii isingekamilika kama tusingewavisha watoto hawa viatu na ndio maana tumeanzisha kampeni hii. Lengo letu ni kuhakikisha kila mtoto anakwenda shule na viatu kwa ajili ya afya yao na kuboresha ufanisi wao katika masomo. Tuna hamashisha makampuni, watu binafsi na sekta mbali mbali kuungana nasi katika kampeni hii. Tumeanza na Kijini na Mbuyu Tende lakini shabaha yetu ni kuwavisha watoto wote wanaokwenda shule bila viatu Zanzibar nzima.”  alisema meneja wa huduma za jamii Aminata Keita.


“Leo tuna Furaha kubwa kuzinduliwa kwa kampeni hii katika shule yetu ya Kijini. Wazazi na walimu wa Kijini wana furahia kuvishwa watoto wao viatu na kuonekana wamependeza na kuhifadhika miguu yao” Mwalimu Mkuu wa Sekondari Kijini, Ulimwengu Mkadam

Uzinduzi huu uliadhimishwa na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Vuai Mohamed akiambatana na Mkurugenzi wa Elimu Maandalizi na Msingi Zanzibar Bi Safia Rijal, alitoa wito kwa wengine kuunga mkono kampeni hii sio tu kwa watoto wa Kijini na Mbuyu Tende bali kwa Zanzibar vijijini kote.

 “Tunaipongeza Best of Zanzibar kwa kazi nzuri na program zao zote kwa nia ya kuongeza ufanisi na ubora wa elimu Kijini na Mbuyu Tende. Kwa hakika wamekuwa mfano bora wa kuigwa na taasisi nyengine katika kuleta mabadiliko bora ya kielimu nchini.

Uzinduzi wa kampeni hiyo uliambatana na kupewa zawadi kwa wanafunzi takriban 45 ambao wamefanya vizuri katika Program ya masomo ya ziada ijulikanayo “After-hours Tutoring Program” pia kutambua mwanafunzi Makame Kidawa Mwiga aliyefaulu michupuo na Vuai Ali Haji aliyeweza kufaulu kuendelea A-Level.

Best of Zanzibar inawakaribisha wadau wote kuungana nao katika Kampeni hii kusaidia kuwavisha viatu watoto hawa, ili kuwafanya waweko salama kutokana na kudhurika miguu yao na matatizo mengine ya kiafya ambayo yanaweza kuwaathiri katika masomo yao.

Unaweza kuungana nasi kubadilisha maisha ya watoto hawa kwa kuwasiliana kupitia mitandao ya kijamii



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.