NA ZUHURA JUMA, PEMBA
JESHI la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, limeingiza jumla
ya Tshs, Milion 8,450,000/=baada ya kukamata
makosa 1107 ya usalama barabarani kuanzia Januari hadi April 13 mwaka huu.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi, Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Haji Khamis Haji,
alisema makosa ya magari yalikuwa 714, vespa na pikipiki 346 na baskeli 47.
Alisema
Jeshi hilo limekamata makosa 1107, ikiwemo
makosa ya mwendo kasi, kutokuvaa kofia ngumu, kutotii sheria za njia, kuzidisha
abiria, kutokuwa na leseni, baskeli na kutumia gari zisivyoruhusiwa.
“Makosa
hayo yalipelekwa mahakamani, ambapo kati ya kesi hizo, wengine walionywa, kesi
nyengine kufutwa na nyengine kupatiwa hukumu”, alisema Kamanda huyo.
Kamanda
Haji, alisema wamekuwa wakifanya doria
za miguu na vyombo vya moto, ili kuhakikisha wanadhibiti makosa ya usalama
barabarani, ambayo yanaweza kusababisha athari mbali mbali kwa watumiaji wa
njia kwenye Mkoa huo.
Aliwataka
madereva kukata leseni, ili kuweza kuondosha migogoro na kusema kuwa Jeshi hilo
litakuwa barabarani wakati wote na kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaokaidi
kutii sheria zilizowekwa.
“Elimu
tunatoa kwa madereva, ili wajue sheria zao lakini wapo baadhi yao wanakaidi,
hivyo hatutowaachia madereva wa aina hiyo”, alisema.
Hivyo
Kamanda huyo aliwataka madereva kufuata sheria bila ya shuruti, ili kuweza
kuepusha changamoto zinazoweza kuepukika, ikiwepo ajali.
No comments:
Post a Comment