Habari za Punde

Changamkia ajira Afisi ya Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Unguja na Pemba

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI AFISI YA MAMLAKA YA KUZUIA RUSHWA NA UHUJUMU WA UCHUMI ZANZIBAR

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa ajili ya Afisi ya Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Unguja na Pemba kama ifuatavyo:- 

1.Afisa Uchunguzi Daraja la II “Nafasi 14 Unguja” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Shahada ya Kwanza ya Uchumi, Ukaguzi wa Hesabu, Sheria au Uhandisi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 


2.Afisa Takwimu Daraja la II “Nafasi 1 Unguja” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Shahada ya Kwanza ya Takwimu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 


3.Afisa Ufuatiliaji na Tathmini Daraja la II “Nafasi 1 Unguja” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Shahada ya Kwanza ya Uchumi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 


4.Afisa Utumishi Daraja la II “Nafasi 1 Pemba” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Shahada ya Kwanza ya Utawala au Rasilimali Watu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 


5.Msaidizi Afisa Uhusiano Daraja la III “Nafasi 1 Unguja” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Stashahada ya Uhusiano wa Umma (Public Relation) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

6.Karani Masjala Daraja la III “Nafasi 1 Pemba” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Stashahada ya Utunzaji Kumbukumbu (Record Manangment) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

7.Dereva Daraja la III “Nafasi 1 Pemba” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Form IV na kupata Cheti cha Udereva na leseni hai class C kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

8.Wahudumu Daraja la III “Nafasi 2 Unguja” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Form IV. 

9.Mtunza Ghala Daraja la III “Nafasi 1 Pemba” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Stashahada ya Utunzaji ( Material Management) Ghala kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 


10.Katibu Muhtasi Daraja la III “Nafasi 1 Unguja” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Stashahada ya Uhazili kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

11.Telephone Operators Daraja la III “Nafasi 3 Unguja” 

Sifa za Muombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Elimu ya Stashahada ya Mawasiliano ya Simu (Telecommunication Engeniering) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

Jinsi ya Kuomba: 
•Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:- 

KATIBU, 
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI, 
S. L. P 1587 - ZANZIBAR. 

•Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba. 

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:- 
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo 
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari) 
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa. 
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari. 
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni. 
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa. 
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 15 Mei, 2018 wakati wa saa za kazi. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.