Habari za Punde

KAMISHNA MKUU WA TRA ATEMBELEWA NA BALOZI WA SERIKALI YA JAMHURI YA KOREA KUSINI NCHINI TANZANIA

Balozi wa Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini nchini Tanzania Bw. Song Geum - Young (wa pili kushoto) akizungumza na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Charles Kichere (kulia) alipomtembelea Kamishna huyo ofsini kwake mapema leo kuzungumzia masuala mbalimbali ya kodi katika uwekezaji na biashara. Kulia ni Bw. Tiger Lee (Seung - Hoon) kutoka Ofisi ya Ubalozi wa Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini nchini Tanzania.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Charles Kichere (kulia) akizungumza na Balozi wa Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini nchini Tanzania Bw. Song Geum - Young (wa pili kushoto) alipomtembelea Kamishna huyo ofsini kwake mapema leo kuzungumzia masuala mbalimbali ya kodi katika uwekezaji na biashara. Kulia ni Bw. Tiger Lee (Seung - Hoon) kutoka Ofisi ya Ubalozi wa Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini nchini Tanzania.
Balozi wa Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini nchini Tanzania Bw. Song Geum - Young akimkabidhi zawadi Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Charles Kichere alipomtembelea Kamishna huyo ofsini kwake mapema leo kuzungumzia masuala mbalimbali ya kodi katika uwekezaji na biashara. Wa kwanza kushoto  ni Bw. Tiger Lee (Seung - Hoon) kutoka Ofisi ya Ubalozi wa Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini nchini Tanzania na wa kwanza kulia ni Bw. Said Athumani, Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti, Sera na Mipango wa TRA.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Charles Kichere na Balozi wa Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini nchini Tanzania Bw. Song Geum - Young wakipeana mikono baada ya kumaliza mazungumzo wakati Balozi huyo alipomtembelea Kamishna Mkuu ofsini kwake mapema leo kuzungumzia masuala mbalimbali ya kodi katika uwekezaji na biashara. Wa kwanza kulia ni Bw. Said Athumani, Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti, Sera na Mipango wa TRA.
(Picha na Veronica Kazimoto).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.