Habari za Punde

AFATAH YATOA SOMA KWA AKINA MAMA ,YASEMA DHULMA NI ADUI WA MAISHA


Na.Salmin Juma , Zanzibar
Waisilamu Zanzibar na duniani kwa ujumla wametakiwa kuwa makini katika maisha yao kwa kutojiingiza katika   dhulma kwani ni tendo lililoharamishwa na lisilo takiwa kabisa kwa  muisilamu yoyote yule.

Hayo yamesemwa leo  na mkurugenzi wa jumuiya ya Afatah Charitable Association Sh:Rashid Salim Mohd  katika ukumbi wa S.H.A Timber hall Mombasa Zanzibar kupitia mhadhahara uliyowakutanisha wanawake kutoka sehemu tofauti ya Zanzibar.
Akizungumza na umma uliyojitokeza katika muhadhara huo Sh Rashid , amesema katika maisha ya leo, jambo la kushangaza  dhulma inaonenkana kama maji ya kunywa (jambo la kawaida) na baadhi ya watu huwashangaa wengine kisa tu maisha yao wanajiepusha na tendo hilo chafu.

‘’dhulma katika maisha ya leo imekua ni jambo la kawaida kufanywa, watu wanaiba waziwazi, hata wanawake wanaonekana kuiba madukani  ’’ alisema sh Rashaid

Akiifafanua zaidi Dhulma amesema kitaalamu ipo katika sehemu tatu na zote hizo zimekua ni kawaida katika maisha ya waisilamu wa leo.

Amesema aina moja  ni ile dhuluma ya mja kumdhulumu mola wake ‘’katika dhuluma hii waisilamu wengi wanajisahau mfano, kumshirikisha mungu na kitu chengine, wapo wanaoabudu waganga wa kienyeji, kila kitu ni kwa kutizamia , haamini kudra za mungu wake hili ni tatizo kubwa sana’’ alisema Sh Rashid

Aina ya pili ya dhuluma, amesema ni dhuluma ya mtu kujidhulumu nafsi yake ‘’kuipelekea nafsi katika mambo ambayo Mungu ameyakataza, wapo wasiofunga na kula mchana wa ramadhani kwa makusudi, wapo wasio Sali na wengineo’’ alisema

Ni aina ya mwisho ya dhulma Sh Rashid amesema ni dhuluma kubwa ambayo watu wamekua wakijiingiaza huko wengine kwa makusudi , ni dhuluma ya kudhulumiana mtu na mtu .

Amesema , ni hali ya kuhuzunisha mno kumuona mtu anaendesha maisha yake yote kupitia dhuluma hii, wapo wanaowadhulumu mayatima kuendesha maisha yao, inafikia  hatua mtu hali mpaka akadhulumua.

‘’dhulma mbaya sana kila mmoja ni lazima ayatazame maisha yake la si hivyo huwezi kuepuka adhabu za Alla SW na tufahamu kuwa yoyote anaekula mali ya haramu dua yake haikubaliwi’’ alisema

Akimalizia kuzungumza na umma huo Sheikh.Rashid amesema kuwa , matukio mabaya makubwamakubwa yanayoonekana kutokea duniani kama vile wizi, unyang’anyi wa nguvu, na mabalaa mengine mengi yao huchangiwa na watu kula mali za dhuluma, amesema hata watoto wengine wanazaliwa katika misingi ya dhuluma hivyo ndio maana maisha yanakuwa magumu na ya mitihani kila siku.

Kwa upande wao wanawake waliyoshiriki katika muhadhara huo wamesema kuwa, kutokana na hali za kimaisha zilivyo hivi sasa bila shaka mada iliyozungumzwa inakwenda sawa na mazingira yalivyo.

Sulha Maulid Ali amesema , unapozungumzia dhuluma , huwa unagusa maisha ya watu wengi hasa wanawake katika kipengele cha dhuluma ya mja kwa mja ‘’muhadhara ni mzuri sana na napendekeza uendelee hadi ramadhani imalizike kwani mengi yanatugusa wanawake’’alisema Sulha.

Mwanajuma Mussa Seif kwaupande wake amesema kuwa, awali alikua hajui mambo mengi lakini mara baada ya kuhudhuria mhadhara huo amejifunza mengi na atakua ni mwenye kubadilika kutokana na mawaidha hayo.

Kwa pamoja wametoa wito kwa waisilamu nchini kujitathmini katika njia zao za kujipatia kipato kusiwe na chembe ya dhulma kinyume na hapo maisha yatazidi kuwa magumu na mitihani.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.