Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba , Hemed Suleiman Abdalla, akisubirikupatiwa Chakula cha Futari iliondaliwa na Benk ya CRDB huko katika Wilaya ya Mkoani Pemba , wakati akijumuika na Benk hiyo kwa ajili ya kuwafutarisha Wananchi wa Wilaya hiyo.
Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa katika futari ya pamoja ilioandaliwa na Benk ya CRDB Tawi la Pemba , kwa ajili ya Wananchi wa Wilaya ya Mkaoni
Meneja wa Benk ya CRDB Tawi la Pemba, Ahmed Abuu Bakar , akitowa maelezo machache juu ya kuwepo kwa Benk hiyo na umuhimu wa Wananchi kujiunga nayo.
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Hemed Suleiman Abdalla, akitowa nasaha zake kwa Waumuni wa Dini ya Kiislamu juu ya kusaidiana na kufanya mambo mema katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani , wakati akijumuika pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Wilaya ya Mkoani Pemba katika futari ilioandaliwa na Benk ya CRDB Tawi la Pemba.
(Picha na Habiba Zarali -Pemba)
Na.Habiba Zarli -Pemba.
Wananchi kisiwani Pemba wametakiwa kusaidiana katika mambo mema nayenye kheri kwao kama Mwenyeezi Mungu (SWT),
alivyoamrisha katika kitabu chake kitukufu cha Quraan.
Mkuu wa Mkoa
wa Kusini Pemba, Hemed Suleiman Abdalla, alitowa nasaha hizi huko Mkoani
Kisiwani humo wakati alipokuwa katika futari ya pamoja ilioandaliwa na Benk ya
CRDB Tawi la Pemba kwa Wanachama wake na Wananchi kwa ujumla.
Alisema
iwapo Waumini wa Dini ya Kiislamu watazingatia na kuyafuata yale ambayo
Mwenyeezi Mungu , amewaambrisha na kuyawacha yale aliowakataza ni wazi kuwa
watafanikiwa katika mambo yao yote ikiwa ni hapa Duniani na kesho mbale yake.
“Waumini wa
Dini ya Kiislamu na Wananchi kwa ujumla niwaombeni muendelee kufanya mambo mema
hata pale Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa sababu sisi Wanaadamu tumeumbwa kwa
dhamira kubwa ya kumcha Mwenyeezi Mungu hivyo katika Mwezi huu ni wa
kukithirisha Ibada kwani malipo yake ni makubwa ,” alisema.
Alifahamisha
katika mwezi mtukufu wa Ramadhani Waumini wa Dini ya Kiislamu wanatakiwa
kukithirisha ibara kwa kusoma Quraan , kuswali Swala mbali mbali zikiwemo za
Faradhi na Sunna na kuswali Taraweikh na kusimama usiku kwa ajili ya kumuomba
Allah SWT, na mengi mengineyo ikiwemo kuwasaidia wasiojiweza.
Alieleza
kufutarisha kwa Benk ya CRDB ni moja
katika jambo muhimu sana hasa pale Mwenyeezi Mungu alipo sisitiza kuwa kuwa
kumfutarisha mwenzako tone moja la maji kuna fadhila kubwa.
Mkuu huyo wa
Mkoa wa Kusini Pemba , aliwataka Wananchi kuitumia Benk ya CRDB kwani kuna
fursa nyingi na kusema kuwa imedhamiria
kufunduwa utowaji wa huduma kwa misingi ya Kiislamu hivyo ni ni fursa kubwa ya
kuitumia.
Aliwahakikishia
Watendaji wa Benk hiyo kuwa Serikali itaendelea kutowa ushirikiano ili
kuhakikisha wanaendelea kufanyakazi walizokusudia .
Alisema ujio
wa Benk ya CRBD, Mkoani itakuwa ni chachu ya kuleta maendeleo hasa ukizingatia
ndio ndio Wilaya inayochangia zaidi ya asilimia 50 katika zao la Karafuu.
Mapema Meneja wa Bank ya CRDB, Tawi la Pemba, Ahmad
Abuubakar, alisema lengo la ujio wa Benki hiyo ni
kumkombowa Mwananchi na kumuinuwa Mkulima wa Karafuu .
Alifahamisha
Benk hiyo itahakikisha Mkulima huyo anaondokana na Unyonge kwa kuwapatia Vifaa
mbali mbali wanavyostahiki wakati wa
uvunaji wa zao la Karafuu.
Meneja huyo,
alieleza kuwepo kwa Bmk nyingi sio ugomvi lakini ni sababu moja ya kuleta
ushindani wa kibiashara ambao utaweza kusukuma mbele Shughuli za Kimaendeleo
katika nchi.
“Wananchi
karibuni katika Benk hii ili muweze kuzitumia fursa zilizopo ambazo zitatolewa
kwa ajili ya manufaa yenu na Taifa kwa ujumla,” alieleza Meneja.
Kwa upande
wao Wananchi waliohudhuria katika futari hiyo waliishukuru Benk ya CRDB kwa kuona umuhimu wa kufutari
pamoja na Wananchi wa Wilya ya Mkoani ambapo wameanza kuonesha mwanga kwa
Wananchi w kuhusu upatikanaji wa huduma za Kibenk.
“Tunaushukuru Uongozi wa benk hii kwa kuonesha kutujali na kuamuwa kukaa nasi
pamoja katika jambo hili muhimu kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani na sisi
tunawaahidi tutakuwa pamoja nanyi,”walisema.
CRDB ni Benk
Kongwe nchini Tanzania ambayo ina Matawi yasiopunguwa 152 ambapo kwa Afrika
Mashariki inatowa huduma zake katika nchi ya Burundi .
No comments:
Post a Comment