Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, Amtumia Salamu za Pongezi Rais wa Msumbiji


 
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                                                                           26.06.2018
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein amemtumia salamu za pongezi Rais wa Msumbuji, Felipe Nyusi kwa kutimiza miaka 43 tokea kupata Uhuru kwa Taifa hilo.

Salamu hizo zilieleza kuwa kwa niaba yake Dk. Shein, wananchi pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wanaungana pamoja na ndugu zao wa Msumbuji katika kusherehekea siku hiyo adhimu ya uhuru wa Taifa hilo.

Aidha, katika salamu hizo, Dk. Shein alimuhakikishia Rais Nyusi kuwa Zanzibar itaendeleza uhusiano na ushirikiano mkubwa uliopo kati yake na nchi hiyo sambamba na kuimarisha udugu uliopo kati ya wananchi wa pande mbili hizo.

Pia, salamu hizo zilieleza namna ya Zanzibar itakavyoimarisha ushirikiano uliopo kati yake na Msumbuji kwa kukuza uhusiano mwema wa kikanda na kimataifa.

Pamoja na hayo, Dk. Shein alitumia fursa hiyo kumtakia Rais Nyusi afya njema yeye na familia yake na kumtakia maisha marefu yenye furaha pamoja na sherehe njema ya siku hiyo adhimu ya uhuru wa Taifa hilo kwa amani, utulivu na upendo kwa maendeleo endelevu ya wananchi wa Msumbiji.

Msumbiji ilipata uhuru wake Juni 25 mwaka 1975 kutoka kwa koloni la Wareno chini ya Jamedari wake Samora Machel ambaye hatimae ndiye aliekuwa Rais wa kwanza wa Msumbuji huru.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.