Habari za Punde

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Imelihakikishia Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Watoto Duniani UNICEF ltaendelea Kuthamini Mchango Wake Kuhakikisha Watoto Zanzibar Wanaendelea Kupata Haki Zao Zote za Msingi.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Ussi Haji Gavu, akizungumza wakati wa kumuaga Afisa Mkuu wa (UNICEF) Zanzibar Bi Francesca Morandini aliyemaliza muda wake wa kazi hapa Zanzibar.Hafla hiyoimefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Park Hayyt Shangani Zanzibar. 
Afisa Mkuu wa (UNICEF) Zanzibar Bi Francesca Morandini aliyemaliza muda wake wa kazi hapa Zanzibar.akitowa neno la shukran kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa Ushirikiano wao wakati wote alipokuwa akifanya kazi zake Zanzibar kupitia Taasisi ya UNICEF, kulia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Issa Haji Gavu.

Afisa Mkuu wa (UNICEF) Zanzibar Bi Francesca Morandini aliyemaliza muda wake wa kazi hapa Zanzibar.akizungumza na kutowa shukrani wakati wa hafla ya kumuaga iliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Park Hayyt Shangani Zanzibar.


SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imelihakikishia Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia watoto duniani (UNICEF) kuwa litaendelea kuthamini mchango mkubwa wa Shirika hilo katika kuhakikisha watoto wa Zanzibar wanaendelea kupata haki zao zote za msingi.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Ussi Haji Gavu aliyasema hayo huko katika ukumbi wa Hoteli ya Park Hayat, Shangani mjini Zanzibar wakati wa hafla fupi iliyotayarishwa na Ofisi ya Rais kwa ajili ya kumuaga Afisa Mkuu wa (UNICEF) Zanzibar Bi Francesca Morandini aliyemaliza muda wake wa kazi hapa Zanzibar.

Katika maelezo yake Waziri Gavu alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inathamini sana mashirikiano makubwa yaliopo kati yake na Shirika hilo huko akitumia fursa hiyo kumpongeza na kumshukuru Afisa Mkuu huyo kwa mashirikiano yake katika kipindi chote alichofanya kazi Zanzibar.

Alieleza kuwa katika muda wake wote wa Kazi hapa Zanzibar, Afisa Mkuu huyo aliweza kutoa mashirikiano mazuri kwa Wizara na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar jambo ambalo limeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kufikia malengo yaliokusudiwa.

Aidha, Waziri Gavu alitumia fursa hiyo kumueleza Afisa Mkuu huyo wa UNICEF kuwa Serikali ya Mapnduzia ya Zanzibar itaendelea kutoa ushirikiano wake kwa Shirika hilo pamoja na mashirika mengine yote ya Umoja wa Mataifa kwa kutambua umuhimu wake mkubwa katika maendeleo ya nchi pamoja na wananchi wake.

Nae Afisa Mkuu wa (UNICEF) Zanzibar Bi Francesca Morandini alitoa shukurani na pongezi kwa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kumuandalia hafla hiyo fupi ya kumuaga na kueleza kuwa tukio hilo limeonesha wazi kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi inavyothamini juhudi za Shirika hilo.

Hivyo, aliihakikishia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Shirika hilo la (UNICEF) litaendelea kuiunga mkono Zanzibar katika juhudi zake za kujiletea maendeleo endelevu pamoja na kuwahakikishia watoto wanapata haki zao zote za msingi.

Sambamba na hayo, Afisa Mkuu huyo alizipongeza juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inazozichukua katika kuwahudumia watoto kwa kuweka mikakati madhubuti ambayo imekuwa chachu katika kuwaenzi, kuwalinda na kuwatunza watoto pamoja na akina mama wa Zanzibar kwa jumla.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.