Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndugulile (mwenye kofia, kushoto), akikabidhiwa taarifa ya Hospitali na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita Dkt. Brian Mbawala (kulia) alipokuwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita kwenye ziara ya kikazi mkoani Geita
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndugulile (mwenye kofia), akitoa maelekezo baada ya kukagua chumba cha kutolea dawa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita kwenye ziara ya kikazi mkoani Geita tarehe 28.07.2018, upande wa kushoto ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita Dkt. Brian Mbawala
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndugulile (mwenye kofia) akikagua fomu za mgonjwa kama zimeandikwa muda halisi tangu amepokelewa hadi ametibiwa kwenye wodi ya watoto alipokuwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita kwenye ziara ya kikazi mkoani Geita
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndugulile (mwenye kofia) akisema na watumishi baada ya kukagua fomu za mgonjwa kama zimeandikwa muda halisi tangu amepokelewa hadi ametibiwa kwenye wodi ya mama na mtoto alipokuwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita kwenye ziara ya kikazi mkoani Geita
Naibu Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb)
amemaliza ziara yake ya kikazi Mkoani Geita iliyodumu kwa siku tatu akiwa amehaidi
kuzifanyia kazi changamoto alizozipokea kutoka kwa uongozi wa Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Geita tarehe 28.07.2018.
Amesema, miongoni mwa
masuala ambayo Wizara imejipanga kuyafanya katika kuboresha huduma za afya
kwenye Hospitali za Rufaa za mikoa ni pamoja na kutengwa kwa bajeti ya Shilingi
Bilioni Thelathini (30,000,000,000/=) ambazo zitawezesha hospitali hizo ikiwemo
ya Mkoa wa Geita.
Kuwa na kitengo cha dharura (emergency), chumba kizuri cha
upasuaji (Theatre), jengo la mama na mtoto, ICU za watoto pamoja na watu
wazima, bila kusahau watumishi wa kutosha ambapo hospitali ya rufaa ya mkoa
imepewa jumla ya watumishi sabini (70) wakiwemo madaktari (16) na kusisitiza
wapokelewe na wapewe ushirikiano kwa kuwa figisu figisu hazina nafasi kwa awamu
hii.
Kwa upande wa huduma
ya mionzi (X-Ray) amesema, “kwa sasa
serikali ina mpango wa kuingia kwenye teknolojia mpya kwa kutumia utaratibu
uitwao
“Placement” yani tunaangalia mahitaji ya hospitali zetu kisha kutangaza
zabuni ambapo vifaa vya kisasa vitafungwa sisi tutachangia huduma na endapo
vifaa vitaharibika litakua jukumu la mzabuni kutengeneza. Sambamba na hilo,
madaktari bingwa watakaa sehemu moja baada ya kuunganishwa mfumo ambapo mgonjwa
atapigwa picha ya mionzi (x-ray) Geita, tafsiri inatoka mbali kupitia huo mfumo”.
Kuhusu dawa, Dkt. Ngudulile amewahakikishia
watanzania kuwa, dawa zote muhimu mia moja sitini na saba (167) zipo hivyo
hakuna changamoto isipokua ameagiza uandikaji wa dawa kwa majina ya kitaalam
(Generic) mfano (paracetamol) na siyo ya kibiashara (Branded) mfano (Panadol,
Sheladol, n.k ), jambo ambalo laweza msababisha mwananchi afikiri hakuna dawa
fulani ilhali ipo hivyo kwa kufanya hivyo ni kuwakosea watanzania.
Lakini pia
akatumia muda huo kumtaka mganga mfawidhi Dkt.
Brian Mawala kuhakikisha kuanzia jumatatu wiki ijayo orodha ya dawa zote
zinarekodiwa na kupelekwa OPD na wodini.
Ametoa agizo kwa vituo
vya kutolea huduma za afya kuhakikisha wanaandika muda sahihi/halisi
anapopokelewa mgonjwa, anapokwenda maabara hadi wakati wa matibabu. Mfano saa
12:03, saa 01:16 na siyo kila mtoa huduma kuandika muda wa majumuisho mfano saa12
PM, saa 1 AM hii itasaidia hata kuangalia chanzo inapotokea tatizo.
Ameonya kuhusu kuacha
utaratibu wa kutuma mialiko ya watumishi kwa majina badala yake, mialiko
iandike kuomba mtumishi wa sifa fulani ili hiyo fursa ya mafunzo itumike kwa
kuzingatia mahitaji ya hospitali kwakua uongozi ndio unajua nani anastahili
kwenda mafunzo.
Pia ameagiza kutumika utaratibu wa kubadili wanaokwenda mafunzo
siyo kila siku mtu mmoja pekee na kuongeza kuwa mfumo uimarishwe kuasidia
ukusanyaji wa mapato.
Amehaidi kuyafanyia
kazi maombi kutoka hospitali hiyo yakiwemo madai ya watumishi, gari la kubebea
wagonjwa (ambulance), ukamilishaji wa jengo la mama na mtoto ambalo lililopewa shilingi
milioni ishirini (tshs.20, 000,000/=) na Mhe.
Rais, pamoja na mchango wa mifuko mia moja ya saruji (100) kutoka kwa
Mbunge wa Geita mjini Mhe. Constantine
Kanyasu, na Mwenyekiti wa bodi aliyetoa milioni moja (tshs.1, 000,000/=)
kwakuwa jengo lilipo ni dogo ukilinganisha na mahitaji.
Amekemea suala la
watumishi wa afya kupigwa, na kusema “kama ikitokea mtumishi wa afya amekosea
kuna taratibu zake na mamlaka za nidhamu, hivyo awe mwananchi au mtumishi
mwingine haruhusiwi kumpiga mtumishi wa afya, hivyo kwa ambayo yalitokea
uchunguzi unaendelea na wale wote watakaobainika, hatua za kisheria
zitachukuliwa dhidi yao”aliahidi.
Mbunge wa Jimbo la
Geita, Mhe. Constantine Kanyasu,
Diwani wa Kata ya Kalangalala mahali hospitali ilipo, Kaimu Mganga Mkuu wa
Hospitali na Mganga Mfawidhi kwa niaba ya watumishi na wananchi wamemshukuru
sana kwa ujio wake Naibu Waziri na kuhaidi kupokea na kutekeleza maagizo
aliyoyatoa, kisha naibu waziri kuendelea na safari yake.
Awali Naibu waziri
alipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Eng. Robert Gabriel tarehe 26.07.2018
katika ofisi za Mkoa wa Geita
Boaz L Mazigo
Information Officer
Geita RS
+255 763 245 259
+255 763 245 259
No comments:
Post a Comment