Habari za Punde

Serikali yaagizwa kufanya jitihada za makusudi kufufua michezo ya asili

 WACHEZAJI wa Ngombe wakimpiga ngea (Chenga) ng'ombe, wakati wa tamasha la Utalii, Utamaduni na Bishara lilifanyika katika uwanja wa Dodo Pujini Wilaya ya Chake Chake Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
WACHEZAJI wa Ngombe wakimpiga ngea (Chenga) ng'ombe, wakati wa tamasha la Utalii, Utamaduni na Bishara lilifanyika katika uwanja wa Dodo Pujini Wilaya ya Chake Chake Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA

NG’OMBE mwenye jina la Toba Roho yangu na Kiburungo, ambao hupendwa kuchezwa katika mchezo wa Ng’ombe, ameendelea kuwavutia hisia za mashabiki wa mchezo huo Kisiwani Pemba.

Ng’ombe wengine ambao wameweza kutumika katika mchezo huo ni pamoja na Baruti na Ubamba, ambao ni Ng’ombe wapya kuingia katika mchezo huo.

Ngombe hao wamekuwa maarufu katika mchezo huo, ambapo mchezo huo umefanyika katika viwanja vya Pujini ikiwa ni kuelekea kilele cha Tamasha la Utalii, Utamaduni na Biashara Pemba, lililo chini ya Kamisheni ya Utalii Zanzibar.

Mchezo huo umeweza kushuhudiwa na wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Kisiwa Cha Pemba, wakiwemo Mji wa Chake Chake na maeneo jirani.

Mchezo huo ulioanza saa 11:00 jioni huku mashabiki wengi wakijitokeza katika mchezo huo, akizungumza mara baada ya kumaliza kwa mchezo huo Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman Abdalla, alisema mchezo wa ng’ombe ni Utamaduni Pekee wa nanchi wa Kisiwa Cha Pemba.

Alisema serikali yake ya Mkoa itahakikisha inashirikiana kikamilifu wa Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale, katika kuhakikisha michezo yote ya utamaduni iliyokuwa ikifanyika inafufuliwa upya na kuchezwa katika vipindi vyote na sio kwenye matamasha pekee.

“Mchezo huu unaonekana unapendwa sana leo hebu angalieni watu waliojitokeza, vizuri tukafufua michezo yetu yote ya asili tuliokuwa tukiicheza”alisema.

Alisema kufanyika kwa michezo hiyo itaweza kuvutia watalii kupenda kutembelea kisiwa cha Pemba, pale itakapokuwa na vipindi maalumu na kuweza kukitangaza kisiwa cha Pemba ndani na nje ya nchi zao.

Mkuu huyo alisema kuongezeka kwa watalii wataweza kuongeza pato la nchini, hata uchumi wa Zanzibar nao pia utaweza kuongezeka na vijana kupata ajira kupitia sekta hiyo.

Kwa upande wao wachezaji wa Ng’ombe Kisiwani Pemba, wamesema tayari mchezo huo umeshaanza kupoteza uhalisia wake kutokana na kutokufanyika mara kwa mara.

Walisema mchezo huo hapo awali ulikuwa ukifanyika katika maeneo mbali mbali, hasa baada ya mavuno muda wa jioni kwa lengo la kupongezana, hivyo ipo haja kwa taasisi husika kujipanga kikamilifu kuurudisha utamaduni wa mchezo huo wa asili ya kisiwa cha Pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.