Habari za Punde

Gwaride la Punda lilivyonogesha Tamasha la Utalii, Utamaduni na Biashara lililofanyika Pujini

MSAFARA wa Punda 15 wakiwa katika Gawaride maalumu la Punda, kutoka Chanjaani hadi Pujini wakati wa Tamasha la Utalii, Utamaduni na Biashara lililofanyika Pujini


(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA

KWA mara ya kwanza wananchi wa Kisiwa Cha Pemba wameshuhudiwa Gwaride lan Punda, lilianzia Chanjaani hadi Pujini Wilaya ya Chake Chake.

Gwaride hilo lilianza saa nane za mchana katika uwanja wa Zimamoto Chanjaani, kupitia barabara ya Pujini hadi katiak uwanja wa dodo Punji, huku punda wakiwa wamefolini mistari na waendeshaji wake wakiwa wamevaa kanzu na miemvuli.

Baada ya kufika katika uwanja wa Pujini, punda hao waliweza kukimbia raundi mbili kwa kuzunguruka kila mmoja kuonyesha umahiri wake katika kwenda mbio.

Gwaride hilo lilijumuisha jumla ya Punda 15 kutoka maeneo ya Matale na Pujini, huku baadhi yao wakiongozwa na watoto wadongo na watu wazima.

Gwaride hilo maalumu na mara ya kwanza katika Kisiwa Cha Pemba, limeweza kuvuta hisia za wananchi wengine kujikuta wanashangiria kutokana na aina ya uchezaji wake.

Baadhi ya wananchi waliokuwa wakishuhudiwa walisikika wakisema kuwa, hili ni jambo la faraja kufanyika kwa gwaride hilo, kwani wamezoea kuona mashindano ya farasi tu.

Walisema kama mchezo huo utakuwa unafanyika kila kipindi, basi punda watakuwa na thamani kuliko walivyozoeleka tu kutumika kwa kupakia mizigo.

Saidi Khamis Omar mwenye umri wa miaka 14 mkaazi wa Matale, alisema ni mara ya kwanza kwake kucheza gwaride la Punda, huku akiwaomba waandaaji kuendelea kufanyika maonyesho hayo mara kwa mara, ili kuweza kupata nafasi ya kujitangaza na kuutangaza mchezo huo.

Khamis Omar Khamis alisema kwake amezoea kuona mchezo wa ngombe na mashindano ya farasi, kushiriki katika gwaride hilo la Punda ni mara ya kwanza katika maisha yake.

“Tokea kuzaliwa kwaku sijawahi kushiriki hata mara moja, hii kwangu ndio mara ya kwanza, tumekua tukiona mashindano yam bio za Farasi kumbe na punda nao wanaweza pale wakiwezeshwa waendeshaji wake”alisema.

Alisema pindi mchezo huo kama utaendelezwa basi utaweza kuvuta mashabiki wengi, hata wataalii kutoka maeneo mbali mbali kufika kujionea, kitu ambacho kitakitangaza Kisiwa Cha Pemba.

Salum Haji Khamis aliiomba Wizara ya Habari Utalii na 
Mambo ya Kale, kuuendeleza mchezo huo nao kuweza kuchezwa kila kipidni cha matamasha kama ilivyo mchezo wa ng’ombe.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.