Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,
Mhe. Japhet Hasunga akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dodoma kuwa
Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli, anatarajia
kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Mwezi wa Urithi linalotambulika kama
‘’Urithi Festival, Celebrating Our Heritage’’ litakalozinduliwa rasmi kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini
Dodoma Septemba 15, 2018
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,
Mhe. Japhet Hasunga akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dodoma kuwa
lengo la tamasha hilo ni kuenzi, kudumisha, kuburudisha na kujifunza masuala
muhimu yanayohusu Urithi wa Mtanzania hususani tamaduni zetu, historia,
malikale na maliasili.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Urithi Festival walioshiriki kwenye mkutano
wa Waandishi wa Habari uliofanyika leo jijini Dodoma. Tamasha hilo
linalotarajiwa kuzinduliwa Septemba 15, 2018 na kuenzi, kudumisha,
kuburudisha na kujifunza masuala muhimu yanayohusu Urithi wa Mtanzania hususani
tamaduni zetu, historia, malikale na maliasili.
Baadhi
ya Wajumbe wakiangalia nembo ya Urithi
Festival inakayotumika kwenye Tamasha hilo.(Picha zote na Lusungu Helela-WMU)
Na. Lusungu Helela - Dodoma.
Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe
Magufuli, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Mwezi wa Urithi
linalotambulika kama Urithi Festival, Celebrating Our Heritage
litakalozinduliwa rasmi kitaifa katika
uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma Septemba 15, 2018
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini
Dodoma, Naibu Waziri wa Maliasili na
Utalii, Mhe. Japhet Hasunga amesema lengo la Tamasha hilo ni kuenzi, kudumisha, kuburudisha na kujifunza
masuala muhimu yanayohusu Urithi wa Mtanzania hususani tamaduni zetu, historia,
malikale na maliasili.
Aidha, Amesema kwa kutambua hazina kubwa ya malikale na
utamaduni wa makabila zaidi ya 128 yaliyopo nchini, tamasha hilo litaongeza
wigo wa mazao ya utalii kwa kukuza utalii wa utamaduni wa malikale hatua ambayo
itaongeza ushindani wa Tanzania kama kituo bora cha utalii kwenye masoko
mbalimbali duniani.
Ameongeza kuwa Urithi
Festival itasadia kukuza utalii wa ndani kwa kuongeza muda wa watalii wa
kimataifa kukaa nchini kwa vile Tamasha hilo lifanyika katika kipindi ambacho
watalii wengi wanatembelea Tanzania
Naibu Waziri huyo amesema kutokana na watalii kuongeza muda
wa kukaa nchini kutaleta faida kwa wananchi na uchumi wa nchi kwa ujumla
Aidha, Naibu Waziri huyo ametaja mikoa sita pamoja na
tarehe zake ambayo Tamasha hilo linafanyika kitaifa wa upande wa jiji la Dodoma tamasha hilo litafanyika
Septemba 15 hadi tarehe 22 na kwa Zanziba litafanyika Septemba 23 hadi 29.
Pia, kwa upande wa Dar es Salaa na Mwanza tamasha hilo
litafanyika Septemba 29 hadi Oktoba 6.
Aidha, kwa upande wa
Wilayani Karatu tamasha hilo litafanyika Oktoba 8 hadi 12, huku Jijini Arusha tamasha hilo
linatarajiwa kutafanyika Oktoba 8 hadi
13 mwaka huu.
Amesema tamasha hilo kutakuwa na shughuli mbalimbali kama
vile sherehe za uzinduzi na kilele, kuenzi lugha adhimu ya Kiswahili na kutoa
tuzo kwa wasanii na wadau wa Urithi.
Ameongeza kuwa Tamasha hilo litapambwa na shamrashamra za
carnival ya mirindimo ya urithi, burudani za ngoma za asilil, muziki na kwaya
pamoja n asana na maonesho ya bidhaa ya wadau.
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri huyo amesema kuwa
Tamasha hilo litahusisha makongamano ya wataalamu, usiku wa urithi, ziara ya
kutembelea vivutio vya utalii pamoja na kunadi urithi katika mitandao ya
kijamii na vyombo vya habari kupitia themes za Mvalishe, Misosi ya Kwetu na
Michongo ya Urithi.
Tamasha la Urithi Festival litakuwa linafanyika kila
mwezi Septemba ya kila mwaka kuanzia mwaka huu.
No comments:
Post a Comment