Habari za Punde

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli Anatarajiwa Kuwa Mgeni Rasmin Kwenye Uzinduzi wa Tamasha la Urithi Festival Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dodoma kuwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli, anatarajia kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Mwezi wa Urithi linalotambulika kama ‘’Urithi Festival, Celebrating Our Heritage’’ litakalozinduliwa rasmi  kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma Septemba 15, 2018 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dodoma kuwa lengo la tamasha hilo ni kuenzi, kudumisha, kuburudisha na kujifunza masuala muhimu yanayohusu Urithi wa Mtanzania hususani tamaduni zetu, historia, malikale na maliasili.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya   Urithi Festival walioshiriki kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari uliofanyika leo jijini Dodoma. Tamasha hilo linalotarajiwa kuzinduliwa Septemba 15, 2018 na  kuenzi, kudumisha, kuburudisha na kujifunza masuala muhimu yanayohusu Urithi wa Mtanzania hususani tamaduni zetu, historia, malikale na maliasili.

Baadhi ya Wajumbe wakiangalia  nembo ya Urithi Festival inakayotumika kwenye Tamasha hilo.(Picha zote  na Lusungu Helela-WMU)



Na. Lusungu Helela - Dodoma.
Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Mwezi wa Urithi linalotambulika kama Urithi Festival, Celebrating Our Heritage litakalozinduliwa rasmi  kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma Septemba 15, 2018
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma,  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga amesema lengo la Tamasha  hilo  ni kuenzi, kudumisha, kuburudisha na kujifunza masuala muhimu yanayohusu Urithi wa Mtanzania hususani tamaduni zetu, historia, malikale na maliasili.
Aidha, Amesema kwa kutambua hazina kubwa ya malikale na utamaduni wa makabila zaidi ya 128 yaliyopo nchini, tamasha hilo litaongeza wigo wa mazao ya utalii kwa kukuza utalii wa utamaduni wa malikale hatua ambayo itaongeza ushindani wa Tanzania kama kituo bora cha utalii kwenye masoko mbalimbali duniani.
Ameongeza kuwa Urithi  Festival itasadia kukuza utalii wa ndani kwa kuongeza muda wa watalii wa kimataifa kukaa nchini kwa vile Tamasha hilo lifanyika katika kipindi ambacho watalii wengi wanatembelea Tanzania
Naibu Waziri huyo amesema kutokana na watalii kuongeza muda wa kukaa nchini kutaleta faida kwa wananchi na uchumi wa nchi kwa ujumla

Aidha, Naibu Waziri huyo ametaja mikoa  sita pamoja na  tarehe zake  ambayo Tamasha hilo  linafanyika kitaifa wa upande wa  jiji la Dodoma tamasha hilo litafanyika Septemba 15 hadi tarehe 22 na kwa Zanziba litafanyika Septemba 23 hadi 29.
Pia, kwa upande wa  Dar es Salaa na Mwanza tamasha hilo litafanyika Septemba 29 hadi Oktoba 6.
Aidha, kwa upande  wa Wilayani Karatu tamasha hilo litafanyika Oktoba 8 hadi  12, huku Jijini Arusha tamasha hilo linatarajiwa  kutafanyika Oktoba 8 hadi 13 mwaka huu.
Amesema tamasha hilo kutakuwa na shughuli mbalimbali kama vile sherehe za uzinduzi na kilele, kuenzi lugha adhimu ya Kiswahili na kutoa tuzo kwa wasanii na wadau wa Urithi.

Ameongeza kuwa Tamasha hilo litapambwa na shamrashamra za carnival ya mirindimo ya urithi, burudani za ngoma za asilil, muziki na kwaya pamoja n asana na maonesho ya bidhaa ya wadau.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri huyo amesema kuwa Tamasha hilo litahusisha makongamano ya wataalamu, usiku wa urithi, ziara ya kutembelea vivutio vya utalii pamoja na kunadi urithi katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kupitia themes za Mvalishe, Misosi ya Kwetu na Michongo ya Urithi.
Tamasha la Urithi Festival litakuwa linafanyika kila mwezi Septemba ya kila mwaka kuanzia mwaka huu.  


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.