Na. Abdi Shamna.
WIZARA ya
Nchi (OR), Katiba, Sheria na Utawala Bora, imesema imeanza mchakato wa ujenzi
wa jengo la Mahakama kuu Zanzibar, unaotarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2020.
Ramani na
michoro ya Ujenzi wa jengo hilo la Ghorofa tisa, utakaofanyika katika eneo la
Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja, umeanza chini ya Kampuni ya Landmark Consultants
Limited ya Zanzibar.
Akizungumza
na vyombo vya habari, Waziri wa Wizara hiyo, Haroun Ali Suleiman (bila ya
kutaja gharama halisi za ujenzi huo), alisema hatua hiyo ya Serikali inalenga
kuleta ufanisi katika suala zima la upatikanaji wa haki, kuimarisha huduma za
kisheria pamoja na kutoa fursa kwa vijana wengi zaidi.
Alisema
katika hatau za awali, tayari Serikali imetenga kiais cha Shilingi Bilioni tano
kwa ajili ya matayarisho ya ujenzi huo, ambapo miongoni mwa fedha hizo
zitakazotumika kwa usafishaji wa eneo, michoro na mambo mengineyo.
Alisema
Wizara yake itahakikisha inasimamia vyema agizo la Serikali la kufanikisha
ujenzi huo, ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Aidha,
Waziri Haroun alitowa wito kwa mrajis wa Mahakama Kuu Zanzibar kuwa program
maalum ya kusomesha vijana wengi zaidi katika fani ya sheria ili waweze kwenda
sambamba na mahitaji ya kuwepo kwa jengo hilo.
Mapema Mkurugenzi
wa Landmark consultants Ltd ,Ali Mbarouk Juma alisema jengo hilo la kisasa
litakalojengwa ndani ya eneo la hekta nne,
litakidhi mahitaji yote muhimu na kuendana na maadili ya kisheria.
Alisema
katika eneo hilo pia kutakuwa na msikiti, Jengo la Jenereta, maegesho ya magari,
sambamba na eneo lililotengwa kwa ajiili ya ujenzi wa “law school”.
Alisema eneo
la chini ya jengo hilo limeandaliwa maalum kwa ajili ya maktaba na uhifadhi wa
vielelezo, hususan vile ambavyo kesi zake zitachukuwa muda mrefu kumalizika.
Aidha,
alisema ndani ya ene hilo zitapatikana huduma za kibenki, ili kuwawezesha wenye mahitaji ya kulipia huduma za kisheria
kuondokana na usumbufu wa kufuata huduma hiyo mjini au maneo mengine ya mbali.
No comments:
Post a Comment