Habari za Punde

Taarifa ya Idara ya Forodha na Ushuru wa Bidhaa Kwa Umma.



ISO 9001: 2015 CERTIFIED

IDARA YA FORODHA NA USHURU WA BIDHAA
TAARIFA KWA UMMA

UTOAJI WA TAARIFA KUHUSU FEDHA TASLIMU NA HATI ZA MALIPO ZINAZOSAFIRISHWA KUINGIA NCHINI AU KUTOKA NJE YA NCHI

Taarifa inatolewa kwa umma kwamba Sheria namba 10 ya 

mwaka 2009 inayohusu utakatishaji wa fedha haramu na 

kanuni yake ya mwaka 2015 imeipa uwezo ofisi ya Zanzibar 

ya TRA kusimamia kazi ya kupokea taarifa zinazohusu 

usafirishaji wa fedha na Hati za malipo zinazoingia nchini na 

kusafirishwa nje ya nchi.

Taarifa hii inahusu usafirishaji wa fedha taslimu au hati za malipo (Bearer Negotiable Instruments) zinazofikia au kuzidi dola za kimarekani elfu kumi (USD10,000) au fedha nyingine yoyote yenye thamani sawa na hiyo, iwapo fedha au hati hizo zitasafirishwa kwa njia zifuatazo

(a)  mtu yeyote anayesafiri akiwa nazo au katika mizigo anayoambatana nayo
au katika chombo cha usafiri;
           (b) katika makontena ya kubebea mizigo, na
           (c) kwa njia ya vifurushi.

Kutokana na uwezo iliyopewa kisheria, ofisi ya Zanzibar ya 

TRA inachukua fursa hii kuutaarifu umma kuwa, kuanzia 

tarehe 13 Agasti 2018, mtu yeyote atakaesafirisha fedha 

taslimu au hati za malipo zinazofikia kiwango kilichotajwa 

na kanuni hizi atalazimika kutoa taarifa wakati wa kusafirisha kwa kujaza fomu maalum zitakazopatikana kwa maafisa forodha waliopo uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume, Bandari ya Malindi, Bandari ya Mkoani, Bandari ya Wete na uwanja ndege wa Pemba.

Wananchi wote wanajulishwa kuwa kutotoa taarifa 

au kutoa taarifa zisizo sahihi kuhusu usafirishaji 

huo ni kosa kisheria

Kwa taarifa au ufafanuzi zaidi tafadhali wasiliana na TRA-Zanzibar kwa namba za simu 0242232923,0242232837/8 au Barua pepe: trazanzibar@tra.go.tz

 Ifahamike kuwa, utaratibu huu haukusudii kuzuia 

usafirishaji wa fedha taslimu na hati za malipo 

kuingia au kutoka nchini.

‘Pamoja Tunajenga Taifa Letu’

IMETOLEWA NA:
NAIBU KAMISHNA
TRA-ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.