Habari za Punde

Timu ya Malindi Sports Clum Zanzibar Yafanya Uchaguzi Mkuu na Kuchagua Safu ya Viongozi Watakaoiongoza Timu Hiyo Kongwe Zanzibar.

Na. Mwandishi Wetu Zanzibar.
Timu ya Soka ya Malindi Sports Club imefanya uchaguzi wake mkuu na kuwapata viongozi wapya watakaoongoza timu hiyo kwa miaka minne ijayo.
Katika Uchaguzi huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Empire Darajani Mjini Unguja, Mohd Abdallah Mohd amechaguliwa kuwa Mwenyekiti, Mohammed Masoud Rashid yeye ameshinda kuwa Katibu Mkuu ambapo Amir Saleh amechaguliwa kuwa Mhasibu huku Mshika Fedha Mkuu akichaguliwa kuwa Ali Majid na msaidizi Mshika Fedha ameshinda Rajab Said.

Wengine walioshinda katika uchaguzi huo ni Jaffar Hussein Babu (Jeff) kuwa Makamo Mwenyekiti ambapo Naibu Katibu ameshinda Sefu Mussa wakati Abdallah Thabit (Dulla Sunday) kuwa Katibu Mwenezi ambapo waliochaguliwa kuwa Wajumbe wa kamati Tendaji ya timu hiyo ni Nassir Seif, Mustafa Ramadhan na Mahmoud Hamza.

Akitangaza matokeo hayo msimamizi mkuu wa kamati ya Uchaguzi huo Omar Mohd Omar amesema Uchaguzi ulikuwa wa haki na huru ambapo wanachama wa timu hiyo walipata haki yao ya msingi kuchaguwa viongozi wao wapya watakayoingoza timu hiyo ambayo itashiriki ligi kuu Soka ya Zanzibar kwa msimu mpya wa mwaka 2018-2019.

Akizungumza mara baada ya kumalizika uchaguzi huo Mwenyekiti mpya wa timu hiyo Mohd Abdallah Mohd amewataka Wanachama na Mashabiki wote wa Malindi kuwa kitu kimoja ili timu yao kufanya vyema kwenye ligi kuu soka ya Zanzibar na kupata nafasi ya kuiwakilisha Zanzibar katika Mashindano ya Kimataifa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.