Habari za Punde

Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Zinatekeleza Kwa Vitendo Falsafa ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Kusisitiza Kufanya Kazi Kwa Bidii.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akitoa hutuba yake katika sherehe za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa,Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius K.Nyerere na Wiki ya Vijana zilizofanyika leo katika Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga, [Picha na Ikulu.] 14/10/2018. 



RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zinatekeleza kwa vitendo falsafa ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yenye kusisitiza kufanya kazi kwa bidii.

Dk. Shein aliyasema hayo leo katika shughuli ya kilele cha mbio za mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pamoja na wiki ya Vijana Kitaifa, zilizofanyika katika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri Mkuuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Kassim Majaaliwa.

Katika maelezo yake, Rais Dk. Sheina alisema kuwa falsafa hiyo ndio iliyopelekea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia Dk. John Pombe Magufuli asisitize kwua “Hapa kazi tu” na kwa upande wake amekuwa akisisitiza kutofanya kazi kwa mazoea.

Alisema kuwa Serikali zote mbili zimejidhatiti katika kuzisimamia rasilimali ili ziwanufaishe watanzania  wote kwa kuwaletea maendeleo.

Rais Dk. Shein alieleza kuwa kumeanzishwa mikakati maaluma ya kuendeleza sekta ya viwanda ili kuongeza fursa za ajira kuwa na matumizi bora ya rasilimali zilizopo na kuifanya nchi kuwa na uchumi imara kwa kuleta Mapinduzi ya Viwanda.

Aliongeza kuwa jitihada zinazochukuliwa na Serikali zote mbili katika kukabiliana na vitendo vya rushwa na uhujumu wa uchumi ni miongoni mwa jitihada za kuendeleza fikra za Mwalimu.

Alisema kuwa pale inaposemwa kwamba zinafuatwa falsafa za Mwalimu, inapaswa kuonesha kwa vitendo kwamba rushwa inachukiwa na watu hawajihusishi na vitendo vya utoaji na upokeaaji rushwa.

Akieleza jinsi anavyokumbukwa Baba wa Taifa, Rais Dk. Shein alisema kuwa atakumbukwa kwa alivyowaunganisha Watanzania kwa kuviongoza na kuvihamasiha vikosi vya ulinzi na usalama hadi lwa pamoja akaweza kungolewa Nduli Idd Amin baada ya kuivamia nchi mnamo mwaka 1978.

“Kwa hivyo kila wakati tunamkubuka Mwalimu tuwe tunazingatia umuhimu wa kutoisaliti nchi yetu.... tuyapende na kuyathamaini mamabo yetu na wala tusiyabeze... marehemu Mzee Abeid Karume alituhimiza umuhimu wa kupenda vyetu kwa kusema “Kithamini kiulichochako mpaka usahau cha mwenzako”,alisema Dk. Shein.

Aidha, Rais Dk. Shein alisema kuwa ana amini kwamba endapo kila Mtanzania ataamua kwa dhati wa moyo wake kuyaenzi mambo mazuri ya Mwalimu Nyerere, Tanzania itapata maendeleo makubwa tena kwa haraka sana.

Dk. Shein alisema kwua dhamira kubwa ya kukimbiza Mwenge wa Uhuru ni kuendelea kukumbushana misingi na mambo muhimu kwa maendeleo ya nchi sambamba na kutoa fursa ya kukutana na kukumbushana nafasi ya Tanzania mbele ya diplomasia ya Kitaifa.

Alisema kuwa amevutiwa sana na kauli mbiu ya Mbioo za Mwenge ya wmaka huu isemayo’ Elimu ni ufunguo wa maisha, Wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa letu” na kusema kuwa kauli mbiu hiyo inakwenda sambamba na Dira ya Maendeleo ya Taifa  ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar zinazotilia mkazo umhimu wa kuipa kipaumbele sekta ya elimu.

Alisisitiza kuwa kwa kuzingatia kwua elimu ndio ufunguo wa maisha Serikali zote mbili zimejidhatiti kuendeleza hatua ya viongozi waasisi wa Taifa hili Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Marehemu Mzee Abeid Amani Karume ya kutoa elimu bila ya ubaguzi kuanzia ngazi ya msingi hadi Sekondari.

Alsiema kuwa lengo la Serikali zote mbili ni kujenga uchumi imara  kwa mnasaba huo anaendelea kuwahimiza kuwashirikisha wananchi na washirika wa maendeleo kuwekeza katika sekta ya elimu.

Dk. Shein alisema kuwa kauli aliyoitoa Rais Magufuli kwenye kilele cha mbio za mwenge tarehe 14.10.2017 katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar kwamba katika kipindi cha uogozi wake na wa Rais Dk. Shein watahakikisha mwege wa uhuru unaendelea kuwepo.

Sambamba na hayo alieleza kuwa Serikali zote mbili zitazingatia sana na zzimeweka mipango mipango maalum katika kuimarisha maendeleo ya vijana  na kuwashirikisha katika kuzitafutia ufumbuzi wa changamoto zzinazowakabili na hasa ukosefu wa ajira.

Aliwtaka vijana wapende kufanya kazi  za halali ili washiriki vyema katika shughuli za ujenzi wa Taifa na wajibu wao kukumbuka kuwa hatma ya Taifa hili iko mikononi mwao.

Mapema Rais Dk. Shein alitembelea mabanda ya Maonyesho ya vijana katika viwanja  vya Tangamano mjini Tanga na kuona shughui mbali mbali zinazofnywa na vijana pamoja na kupata maelezo juu ya shughuli hizo pamoja na sekta nyengine za maendeleo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera. Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama alisema kuwa vija sita waliokimbiza Mwenge wa uhuru wakiongozwa na Charles Francis Kabeho waliukimbiza kilomita 28,283.8 katika Mikoa 31 na Halmashauri za Wilaya 195 kwa siku 195 kwa kipindi hicho cha miezi saba.

Alizitaja Halmashauria 64 zimekutwa na kasoro katika utekelezaji na usimamizi wa miradi ya maendeleo na kusisitiza kwua Serikali imechukua na itaendelea kuchukua hatua stahiki kwa kila aliyehusika na kasoro hizo kupitia Ogfisi ya Rais TAMISEMI na mamlaka nyinginezo.

Sambamba ba hayo Waziri Mhagama alisema kuwa kwa mwaka 2019 uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru utafanyika Mkoani Songwe wakatui maadhimisho ya Kilele cha mbio za mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya Kifo cha Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana Kitaifa yatafanyika Mkoani Lindi.

Wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa  mwaka 2018 ni Isaa Mahamoud Abasi kutoka Mkoa wa Kusini Pemba, Dominick Rweyemamu Njunwa kutoka Mkoa wa Kigoma, Augusta Paul Safari Kutoka Mkoa wa Geita, Riziki Hassan Ali Kutoka Kusini Unguja, Ipyana Alinuswe Mlilo kutoka Tanga na Charles Francis Kabeho kutoka Dar-es-Salaa.

Nao viongozi wakuu waliohudhuria katika hafla hiyo walitoa salamu zao kwa wananchi akiwemo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika Job Ndugai kwa niaba ya Bunge, Waziri wa Vijana, Utamaduni Sanaa na Michezo Balozi Ali Karume kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigella kwa niaba ya Mkoa wake
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.