Habari za Punde

Shirika la Posta Tanzania Laadhimisha Siku ya Posta Duniani Lakabidhi Zawadi na Vyeti Kwa Washindi wa Uandishi wa Barua.

Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang'ombe akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani, jijini Dar es Salaam leo, ambapo washindi wa shindano la kimataifa la uandishi wa barua walizawadiwa zawadi mbalimbali pamoja na vyeti. Kushoto ni Meneja Rasilimali za Shirika Macrice Mbodo. 
Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang'ombe, akimkabidhi zawadi  mshindi wa tatu wa uandishi wa barua, Anna Malagi, kutoka Shule ya Umoja Primary and Nursery ya Mbeya katika hafla hiyo. Anayeshudia katikati ni Meneja Rasilimali za Shirika Macrice Mbodo.  
Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang'ombe, akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa pili wa uandishi wa barua, Hajra Mustafa Kaniki, kutoka Shule ya Sekondari ya St. Mary's Mazinde Juu ya Lushoto, mkoani Tanga. Kushoto ni Meneja Rasilimali za Shirika Macrice Mbodo na wapili kushoto ni mwalimu wa shule hiyo, Josephine Mashare.  
Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang'ombe (wapili kulia), akimkabidhi zawadi mshindi wa kwanza wa uandishi wa barua, Dorine John Massawe, kutoka Shule ya Sekondari ya Joyland Girls ya Same, mkoani Kilimanjaro. Kushoto ni mwalimu wa shule hiyo, John Lwanga na kulia ni Kaimu Meneja Mkuu Uendeshaji Biashara wa TPC, Mwanaisha Ali Saidi.
Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang'ombe, akiwa katika picha ya pamoja na washindi watatu walioshinda shindano la uandishi wa barua, Anna Malagi (wapili kushoto), Hajra Mustafa Kaniki (wa tatu) na Dorine John Massawe. Kushoto ni Meneja Rasilimali za Shirika, Macrice Mbodo na kulia ni Kaimu Meneja Mkuu Uendeshaji Biashara, Mwanaisha Ali Saidi.  
Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang'ombe (wapili kulia) na baadhi ya viongozi waandamizi wa shirika hilo, wakiwa katika picha ya pamoja na walimu, waliofuatana na  wanafunzi walioshinda shindano hilo. Kutoa kushoto ni Mwalimu John Mistry (wapili) kutoka Shule ya Umoja Primary and Nursery, Mwalimu John Lwanga (wa tatu) kutoka Shule ya Sekondari ya Joyland Girls ya Same, mkoani Kilimanjaro na Mwalimu Josephine Mashare (wa nne), kutoka Shule ya Sekondari ya St. Mary's Mazinde Juu ya Lushoto, mkoani Tanga.
Baadhi ya viongozi waandamizi wa Shirika la Posta wakiwa katika hafla hiyo. 
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari, wakifuatilia hafla hiyo. 
Baadhi ya wafanyakazi wa Shirika wakifuatilia hafla hiyo. 
Mshindi wa kwanza wa uandishi wa barua, Dorine John Massawe, akiisoma barua yake iliyompatia ushindi wakati wa hafla hiyo. 
Meneja Rasilimali za Shirika, Macrice Mbodo, akizungumza wakati akifafanua kuhusu masuala ya uandishi wa barua mbalimbali ambazo hadi sasa zinaendelea kuhudumiwa na shirika hilo. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la Posta, Elia Madulesi, akitoa matokeo ya washindi wa shindano la Kimataifa la uandishi wa barua, katika hafla hiyo.   
Kaimu Meneja Mkuu Uendeshaji Biashara, Mwanaisha Ali Saidi (wapili kulia), akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa shindano hilo, nchini.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.