Habari za Punde

Watalii Walazimika Kuongeza Siku Katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Kushuhudia Tukio la Kuhama Kwa Makundi ya Nyumbu Wakitokea Kenya.

Watalii wakiwa kando ya Mto Mara katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ,eneo la Kogatende wakishuhudia tukio kubwa la kuhama kwa Makundi Makubwa ya Nyumbu wakivuka mto kutoka Hifadhi ya Masai Mara nchini Kenya kuingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Kundi la Nyumbu likijiandaa kuvuka Mto Mara katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Nyumbu wakivuka Mto Mara kuingia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti .
Baadhi ya Watalii wamelazimika kuongeza siku za kukaa katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa ajili ya kushuhudia tukio hilo la aina yake ambalo hutokea kila mwaka .
Kundi kubwa la Nyumbu likiwa katika maandalizi ya kuvuka Mto Mara kuingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Magari yaliyobeba Watalii yakiwa yameegeshwa kando ya Mto Mara kusubiri tukio la kuvuka kwa Makundi ya Nyumbu katika Mto Mara kuingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mamba wakiwa Mto Mara katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakiwa katika mawindo ya Mnayama Nyumbu wakati akivuka.
Mnyama Pundamlia wakiwa upande wa pili mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ,tunaweza sema ni kama wako hapo kwa ajili ya mapokezi ya Nyumbu wanarudi kutoka katika Hifadhi ya Masai Mara nchini Kenya.
Eneo la Mto Mara ambapo Watalii wakingojea tukio la kuvuka kwa Makundi ya Nyumbu.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini .
Hifadhi ya Taifa ya Serengeti iliyopo Mkoani Mara,imeendelea kuwa maarufu Duniani na kuvutia watalii wengi zaidi kutoka maeneo mbalimbali ya Dunia kwa ajili ya kujionea tukio la kila mwaka la kuhama kwa Makundi makubwa ya Nyumbu kutoka Hifadhi ya Masai Mara nchini Kenya na kuingia Serengeti.

Tukio hili ambalo hutokea kuanzia mwezi Julai na wageni kulipa jina la  “Great Wildebeest Migration” mwaka huu linatajwa kuvutia watalii wengi zaidi huku wengine wakilazimika kuongeza siku za kukaa katika Hifadhi ya Serengeti wakingojea kushuhudia tukio hilo.

Michuzi blog imeshuhudia Msururu wa Magari ya kubeba watalii yakiwa  na wageni kando ya Mto Mara kusubiri kujionea hali inavyokuwa wakati wanyama hao wakivuka kwa makundi kutoka upande mmoja wa mo kuingia Hifadhi ya Serengeti.

Eneo la Mto Mara ambapo Wanyama hawa wamekuwa wakivuka linatajwa kuwa na Vivuko 10 hali inayochangia waongoza watalii kufuata mwenendo wa Nyumbu kwa sababu si rahisi kufahamu wapi wataelekea kuvuka jambo ambalo hutumia zaidi ya saa 5 hadi 7 kungojea tukio hilo.

Tukio la  misafara ya makundi  ya  wanyama  hao  kuhama  na kurudi hubadilika  kila  mwaka  kutokana na mabadiliko  ya  hali  ya  hewa  na kiwango  cha maji  katika  mto  mara  hata hivyo   limeendelea  kuwa   kivutio  kikubwa kwa wageni .

Kivutio  kikubwa  katika  misafara ya  wanyama hao  ambao  wamekuwa  wakiondoka  nchini  kila  mwaka   kuanzia mwezi  mey  na  kurudi  kuanzia  mwezi  julay  ni  namna  wanavyovuka  mto  mara  na  jinsi  wanavyokabiliana  na wanyama wengine  ndani  ya  mto  huo   wakiwemo  Mamba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.