Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Ali Mohamed Shein, akijumuika na Waumi wa Kiislam Zanzibar katika sherehe za Maulidi ya Kuzaliwa Mtume (S.A.W) akiitikia dua ikisoma na Mufti Mkuu wa Zanzibar kulia Sheikh Saleh Omar Kabi, yaliofanyika katika viwanjavya maisara suleiman Zanzibar jana usiku.19-11-2018.
Na.Abdi Shamnah.Ikulu Zanzibar.
RAIS wa
Zanzibar na Mwenyektii wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein, jana
amejumuika na mamia ya waumini wa Dini
ya kiislamu kutoka Mikoa yote ya Unguja, kuadhimisha uzawa wa Mtume Muhammad
(SAW).
Maadhimisho
hayo yalifanyika katika viwanja vya Maisara mjini hapa, ambapo Viongozi mbali
mbali wa Dini na Serikali, Mabalozi na wanafunzi kutoka Madrasa na Vyuo vya
Qraaan walishiriki.
Uzawa wa
Mtume Muhammad (SAW), huadhimishwa kila ifikapo mwezi 11, Rabi - Ul -Awal ya
kila mwaka.
Akitoa
waadhi kwa waislamu waliohudhuria Maulid hayo, Mstahiwa Naibu Kadhi Mkuu Khamis
Othman Kombo alitowa wito kwa waumini wa Dini hiyo kuendeleza wajibu wa kufuata
maadili na mwenendo mwema aliokuja nao
Mtume, akibainisha kuwa hatua hiyo ni
ukamilifu wa imani.
Alisema kuja
kwa utandawazi Duniani, kumeifanya jamii ya Wazanzibari na hususan vijana
kujiingiza katika mambo maovu, ikiwemo
udhalilishaji wa kijinsia na hivyo kwenda kinyume na miongozo wa dini .
Aliwakumbusha waislamu wajibu wa kutekeleza kwa dhati yale
yote aliyokuja nayo Mtume kwa kuwa yeye ndio kigezo chema kutoka kwa Mola muumba.
Aidha,
aliishukuru Serikali kwa kudumisha amani n utulivu nchini muda wote, hali inayotowa
nafasi kwa wananchi kupata fursa adhimu
ya kuabudu.
Nae, Sheikh
Mohammed Kassim kutoka Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana, alikemea tabia iliojengeka miongoni mwa waumini ya
kushindwa kufuata maadili na tabia njema
alizokuwanazo Mtume Muhammad (SAW).
“Inatupasa
kubadili nyendo na tabia zetu na kufuata maadili na mwenendo mwema aliokuwa nao
mtume wetu”, alisema.
Alisema
jamii ya kizazi kiliopo imeyapa kisogo mafunzo aliyokuja nayo Mtume kwa
kushindwa kuwaheshimu na kuwatii wazee, hivyo kwenda kinyume na mwenendo aliodumu nao ikiwa ni kigezo cha unyenyekevu.
Alibainisha
kuwa Mtume Muhammad (SAW) amesifiwa na Mwenyezi Mungu kwa kuwa na tabia nzuri,
hivyo aliwataka waumini kufuata mwenendo wake pamoja na kushinda changamoto mbali mbali
zinazotokana na utandawazi.
Aidha,
Sheikh Kassim aliwataka waislamu kujikita katika utamaduni wa kumsalia Mtume
pale anapotajwa, kuvuta tasbikh pamoja na kufanya istifar ili kupata fadhila, huku akiwaonya baadhi ya waumini (walioibuka katika
siku za hivi karibuni) wanaopinga ibada
hizo.
Maadhimisho ya Maulid ya uzawa wa Mtume Muhammad (SAW), yalifunguliwa
kwa Qoraan tukufu, iliyosomwa na Ustadhi Mtumwa Juma Kombo kutoka Pwani
Mchangani, Mkoa wa Kaskazini Unguja .
Aidha, yaliambatana
na usomaji wa Milango sita (6) ya Barazanji, Maulid ya Homu kutoka Mtendeni
mjini Unguja pamoja na usomaji wa Kaswida kutoka Madrsa mbali mbali.
No comments:
Post a Comment