Naibu Waziri Wizara
ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza (wapili kulia) akitizama
mitambo iliyopo Lushoto, (watatu kulia)Meneja
wa Shirika la Utangazaji Taifa Kanda ya Kaskazini Bw.Gerald
Uisso akimwonyesha mitambo ya
kurushia matangazo ya TBC iliyoko katika
eneo la Kijiji cha Kwemashai alipofanya ziara yake aliyoifanya leo ya kukagua
maeneo yaliyisimikwa mitambo ya TBC kutokana na kuendelea kuwepo kwa kero ya
usikivu katika eneo hilo.
Naibu Waziri Wizara
ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza akiwashauri viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya
ya Lushoto kuuendeleza uwanja wa michezo
wa Sabasaba kwa kuomba wataalamu Wizarani wa kuwapa ushauri wa kiutalamu wa
namna ya kuboresha uwanja huo alipotembea uwanja huo leo,wa kwanza kulia ni
Mwenyekiti wa CCM Wilayani Lushoto
Bw.Amiri Shekelata .
Naibu Waziri Wizara
ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Julianna Shonza akitoa maelekezo ya
mambo ya kuzingatia kabla ya kusimika mitambo ya usikivu kwa Meneja wa
Shirika la Utangazaji Taifa (TBC)
Kanda ya Kaskazini Bw.Gerald Uisso (hayupo
pichani) leo katika Kijiji cha Kwemashai
alipotembelea eneo hilo walilosimika mitambo yao wakati wa ziara yake ya
kukagua maeneo iliyoko mitambo ya TBC kwa Kanda ya Kaskazini.
Mtambo wa kurushia
matangazo ya Shirika la Utangazaji Taifa
(TBC) uliyopo katika Kijiji cha Kwemashai
Wilayani Lushoto ambapo Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa
na Michezo Mhe.Julianna Shonza alitembelea eneo hilo leo ikiwa ni ziara yake ya
kukagua maeneo iliyopo mitambo ya TBC kufuatia changamoto ya usikivu katika
maeneo hayo ya Kanda ya Kaskazini.
Na Anitha Jonas –
WHUSM,Lushoto.Tanga
Naibu Waziri Wizara
ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo amewataka
viongozi wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC )kusikiliza ushauri wa
wazawa wa maeneo wanayoenda kusimika mitambo yao pale wanapofanya utafiti wa maeneo
yatakayofaa kulingana na Jiografia ya eneo husika.
Mheshimiwa Shonza
ametoa kauli hiyo leo Wilayani Lushoto alipotembelea eneo lililowekwa mitambo
ya TBC iliyoko katika eneo la Kwemashai
kwa lengo la kutaka kubaini changamoto zinazosababisha kutokuwepo kwa
usikivu kwa baadhi ya maeneo Wilayani hapo.
“Changamoto kubwa
katika Wilaya hiyo ya Lushoto ni
Jiografia ya eneo hilo kwani inamilima mingi sana kati maeneo yake yote hivyo
ni vyema mkashirikiana na Halmashauri katika kuelekezana eneo abalo itakuwa na mlima mrefu zaidi
kushinda yote ambao utawafaa kwakuweza kusimika mtambo wenu utakao rusha
matangazo katika maeneo yote ya Wilaya hii,”alisema Mhe.Shonza.
Akiendelea kuzungumza
katika ziara hiyo Naibu Waziri huyo aliusisistiza uongozi wa TBC kanda ya
Kaskazini kuhakikisha wanafanya utafiti huo haraka na kusimika mitambo hiyo
mapema kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha inakamilisha usikivu kwa mikoa
iliyoko karibu na maeneo ya mipakani kabla ya mwaka 2020 na ndiyo maana fedha
za bajeti ya kuboresha usikivu zinatolewa kila mwaka.
Naye Mkuu wa Wilaya
ya Lushoto Bw.January Lugangika alimwomba Naibu Waziri huyo kuzungumza na
uongozi wa TBC kuweza kuwapatia mwandishi kwa Wilaya hiyo ya Lushoto kwani
kuhusu suala la ofisi tayari wamekwisha muandalia ipo.
“Tumekuwa tunapata
changamoto kubwa ya mwandishi wa TBC kwani inatulazimu kumtumia mwandishi
aliyeko Tanga ambaye inamlazimu kusafiri kwa basi kwa mwendo wa masaa matatu
hii changamoto kwetu na Wilaya hii inafursa nyingi ya kuzitangaza na tunaamini
kuwa TBC wanawza kushirikiana nasi katika kufanikisha hili,”alisema
Mhe.Lugangika.
Kwa upande wa Meneja
wa Shirika la Utangazaji Taifa (TBC) Bw.Gerald Uisso alieleza kuwa amapokea maelekezo yote na
ofisi yake itahakikisha inazingatia ushauri na kufanikisha zoezi hilo la
kuboresha usikivu mapema .
Pamoja na hayo nae
Mwenyekiti wa Chama cha CCM Wilaya ya Lushoto alimweleza Naibu Waziri huyo kuwa
chama hicho kimeanzakutafuta mwekezaja wa kuendeleza uwanja wa michezo wa
Sabasaba ilikuweza kuuweka katika hali nzuri itakayo faa kwa kutumika katika
michezo mbalimbali.
No comments:
Post a Comment